Trump asema atajiondoa katika mazungumzo na Kim Jong-un iwapo hayana matunda

 Rais Donald Trump aonya kujiondoa katika mazungumzo na Kim Jong Un

Rais wa Marekani Donald Trump anasema kuwa iwapo mazungumzo yake na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong un hayazai matunda 'atainuka na kuondoka katika mazungumzo hayo'.


Katika mkutano wa pamoja na vyombo vya habari, yeye na waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe walisema kuwa shinikizo dhidi ya Korea Kaskazini ni sharti iendelee kwa kukataa kusitisha utengezaji wa silaha za nyuklia.
Bwana Abe yuko katika mgahawa wa rais Trump wa Mar-a-Lago resort mjini Florida kwa ,mazungumzo.
Mapema , bwana Trump alithibitisha kwamba mkurugenzi wa CIA Mike Pompeo alifanya ziara ya kisiri hadi Korea Kaskazini ili kukutana na Kim Jong Un.

Alisema kuwa bwana Pompeo aliweka uhusiano mzuri na bwana Kim ambaye bwana Trump alimuita 'mtu mdogo' na kwamba mkutano wao ulifanyika vizuri.
Ziara hiyo iliadhimisha mawasiliano ya juu kati ya Marekani na Korea Kaskazini tangu 2000.
Mkutano huo kati ya Trump na bwana Kim unatarajiwa kufanyika kufikia mwezi Juni. Maelezo ikiwemo eneo litakaloandaa mkutano huo bado yanaendelea kufanyiwa kazi.

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa atangaza baraza jipya la mawaziri

South Africa's deputy President Cyril Ramaphosa at a press conference in London 2017 

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa 

Waziri wa zamani wa fedha Nhlanhla Nene amerejeshwa tena katika nafasi hiyo.
Nene alifukuzwa Disemba 2015 na Rais wa zamani Jacob Zuma na nafasi yake ikachukuliwa na Des van Rooyen.
Palipotokea anguko la thamani ya randi alilazimika kumfukuza Rooyen na kumchagua Pravin Gordhan, siku nne baadae ambaye pia alimfukuza kazi siku za mbeleni.
Katika baraza la Ramaphosa, Gordhan amerejea kama waziri wa masuala la biashara.
Aliyekuwa mke wake Zuma, Nkosazana Dlamini-Zuma, ameteuliwa kuwa waziri wa ofisi wa rais.
Bw Ramaphosa, ambaye ni mfanya biashara wa umri wa miaka 65, katika hotuba yake ya taifa awali mwezi huu, aliahidi kupambana na rushwa na kuboresha uchumi wa nchi hio.
Aliingia madarkani baada ya mtangulizi wake kuondoka katika hali tete, akikataa shinikizo kubwa ya yeye kujiuzulu.
Utawala wa miaka tisa ya Bw Zuma ulikumbwa na misukosuko ya shutuma za ufisadi wakati nchi ilikuwa ikipambana na madeni ya ndani pamoja na viwango vya juu vya ukosaji ajira.

Kabwe: Tutaendelea kupambana dhidi ya sheria kandamizi Tanzania

Zitto Kabwe,Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo 

Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Zitto Kabwe ameachiliwa huru kwa dhamana asubuhi hii baada ya kukamatwa na polisi usiku wa kuamkia Februari 23mkoani Morogoro, karibu kilomita 200 kutoka Dar es salaam.
Sababu ikitajwa ni kufanya mikutano bila kibali alipokuwa akifanya ziara ya kutembelea viongozi wa chama chao cha ACT Wazalendo maeneo mbalimbali nchini Tanzania.
Alipokamatwa Bw Zitto aliweka ujumbe katika akaunti yake ya Twitter, "Ninasindikizwa hadi kituo cha polisi cha Mgeta wilayani, Mvomero.... Sijaambiwa kwa nini nimekamatwa."
Mbunge Zitto Kabwe ameachiwa kwa dhamana ya maneno yenye thamani ya shilingi milioni 50 fedha za kitanzania na kudhaminiwa na wakaili wake ndugu Emmanuel Lazarus Mvula.
Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo alikuwa kwenye ziara ya chama chake mkoani humo.
Ametakiwa kuripoti Polisi Kituo Kikuu cha Polisi cha Mkoa wa Morogoro Jumatatu, Machi12, 2018.
Baada ya kuachiwa kwa dhamana, Zitto Kabwe na viongozi wengine wa kitaifa wa chama hicho wamesema wataendelea na ziara ya kutembelea kata zinazoongozwa na chama hicho.
Vile vile Zitto akaelezea katika ukurasa wake wa Facebook " Baada ya kulala bure jana polisi Morogoro, tunaendelea na kazi yetu ya kutembelea kata zote ambazo Wananchi walitupa dhamana kwa kuchagua madiwani wa Act Wazalendo."
Katika eneo hilo hilo, taarifa za usiku wa kuamkia leo, zinasema mjumbe mwingine kutoka chama cha upinzani cha CHADEMA ameuwawa. Taarifa zinasema Diwani huyo wa kata ya Namwawala Godfrey Luena alikutwa nyumbani akiwa mauti baada ya kukatwakatwa kwa mapanga na watu wasiojulikana.

Magufuli na Kenyatta waagiza mawaziri watatue tofauti kati ya Kenya na Tanzania

Kenyatta na Magufuli walipokutana Kampala

 Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na mwenzake wa Tanzania Dkt John Magufuli wamekutana mjini Kampala, Uganda na kuahidi kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

Wawili hao wamewaagiza mawaziri wa nchi hizo mbili kutatua tofauti ndogondogo zinazojitokeza katika biashara kati ya nchi hizi mbili.
Marais hao wametoa maagizo hayo walipokutana hoteli ya Munyonyo mjini Kampala muda mfupi kabla ya kuanza kwa vikao vya mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulikuwa umeonekana dorora wiki za karibuni hasa kutokana na hatua ya Tanzania kuwakamata na kuwateketeza vifaranga kutoka Kenya na pia kuwapiga mnada ng'ombe wa watu wa jamii ya Wamaasai kutoka Kenya.
Wawili hao wamesema wanataka kuona biashara kati ya Tanzania na Kenya inazidi kukua na bidhaa zinauzwa na kununuliwa baina ya nchi hizo bila vikwazo vyovyote na hivyo kuagiza tofauti zilizojitokeza katika baadhi ya bidhaa zimalizwe
Kuna mambo madogomadogo yanakuwa yanajitokeza katika biashara kati ya Kenya na Tanzania, tunataka kwa haya yote Mawaziri wa Kenya na Mawaziri wa Tanzania mkae myatatue, sisi hatuna tatizo, mambo mengine madogomadogo mno, mambo ya viatu, nguo, ngano, gesi ni madogo sana, mnatakiwa myatatue nyinyi yasifike kwetu, sisi huku tuko sawasawa" amesema Dkt Magufuli, tamko ambalo limeungwa mkono na Bw Kenya.
Wametoa maagizo hayo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria wa Tanzania Prof. Palamagamba Kabudi upande wa Tanzania.
Upande wa Kenya, maagizo yametolewa kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Monica Juma na Waziri wa Afrika Mashariki na Maendeleo ya Ushoroba wa Kaskazini wa Kenya Peter Munya.

Mtangazaji ajifungua akiwa hewani Marekani

Cassiday Proctor, mtangazaji wa kipindi cha redio cha alfajiri katika kituo cha redio cha The Arch katika mji wa St Louis nchini Marekani alitangaza kujifungua kwake kupitia njia ya upasuaji siku ya Jumanne.

Mtangaza mmoja wa redio nchini Marekani amejifungua akiwa hewani wakati wa kipindi chake cha alfajiri.
Cassiday Proctor, mtangazaji wa kipindi cha redio cha alfajiri katika kituo cha redio cha The Arch katika mji wa St Louis nchini Marekani alitangaza kujifungua kwake kupitia njia ya upasuaji siku ya Jumanne.
Bi Proctor alianza kuhisi uchungu wa kujifungua siku ya Jumatatu .Kituo chake cha habari kilishirikiana na hospitali ambayo alijifungua ili matangazo yake kwenda moja kwa moja hewani.
Aliambia BBC kwamba alipata fursa ya kwenda hewani moja kwa moja alipokuwa akijifungua mtoto huyo wiki mbili kabla ya muda uliotarajiwa.
''Ilikuwa furaha kuweza kuwa hewani na wasilikizaji wetu katika siku muhimu ya maisha yangu'' , alisema bi Proctor kuhusu kipindi hicho.
Alisema kuwa kujifungua ukiwa hewani ni mwendelezo ya kile kinachoendelea kila siku katika kipindi hicho ,''mimi huwaambia watazamaji wangu kila kitu kinachoendelea katika maisha yangu.'' .
Mtoto huyo aliyekuwa na uzani wa 7lbs 6oz amepatiwa jina Jameson baada ya wasikilizaji kupendekeza jina la mtoto huyo katika shindano mwezi Januari.
Majina 12 ya kijinga pamoja na mengine 12 yaliochaguliwa na mtangazaji huyo na mumewe yaliwekwa katika sehemu moja .
''Tulipiga kura hadi tulipopata Jameson'', alisema mkurugenzi wa vipindi Scott Roddy .
Mtangazaji mwenza wa bi Proctor Spencer Graves aliambia BBC kwamba hatua hiyo ya kujifungua hewani ilikuwa ya kipekee.
Bi Proctor sasa atakwenda likizo ya uzazi.

Wafanyakazi wa nyumbani waandamana kulalamikia mazingira ya kikazi Kenya

Maadamano ya wafanyakazi wa nyumbani Nairobi 

Wafanyakazi wa nyumbani jijini Nairobi walijumuika na kuandamana wakitoa wito kwa serikali kuwatambua kama wafanyakazi wengine ili pia wao waweze kupata manufaa ya ajira kama vile bima ya afya, likizo ya uzazi na malipo ya uzeeni
Mara nyingi, mfanyakazi wa nyumbani anapokuwa mgonjwa, jambo la kwanza mwajiri anafikiria ni kumfukuza.
Ukizingatia sheria nchini Kenya, wafanyakazi wa nyumbani wana na haki sawa na mfanyakazi mwingine yeyote.
Wanapokuwa wagonjwa, wafanyakazi wa nyumbani wana haki ya kulipwa kikamilifu siku saba za likizo.
Likizo yao ya kila mwaka haipaswi kuwa chini ya siku 21. 

Kisheria, waajiri wanatakiwa kuchangia malipo ya bima ya afya na hazina ya malipo ya uzeeni.
Ruth Khakame, mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Wafanyakazi wa nyumbani anasema kwamba "wafanyakazi wa nyumbani wamekuwa wakifutwa kazi kwa sababu ya ugonjwa, kila siku tunashugulikia kesi za aina hii".

Kwa mujibu wa shirika la Kituo Cha Sheria, wafanyakazi wa nyumbani ni miongoni mwa makundi yanayokumbwa na changamoto zaidi.
Muungano wa wafanyakazi wa nyumbani, ambao umesajili zaidi ya wafanyakazi wa nyumbani 16,000, umekuwa ukiandaa vikao mara kwa mara kusikiliza malalamishi na kuwahamasisha wanachama.
Beatrice Atieno, amefanya kazi hii kwa miaka 15 na huwa anahudhuria vikao hivi "unaweza kupata kuwa unafanyia mtu kazi kwa nyumba yake na hakuheshimu, hakuamini, ikifika wakati wa chakula anakubagua, anakupatia chakula kidogo, huwezi kushiba, na wewe ndio unamtunza mtoto wake, na wewe ndio unachunga nyumba yake".
Kwa mujibu wa Shirika la Kazi la Kimataifa (ILO) asilimia 30 ya wafanyakazi wa nyumbani huwa ni watoto. Wanawake wanajumuisha asilimia kubwa.
Kenya peke yake, wafanyakazi wa nyumbani ni zaidi ya milioni 2.

 

Mwanamume atolewa uvimbe wa kilo 1.8 kwenye ubongo India

Mr Pal's brain tumour was larger than his head 

Madaktari nchini India wamefanya upasuaji wa kipekee na kuondoa uvumbe wa uzani wa kilo 1.8 kutoka kwa mwanamume wa umri wa miaka 31.
Wanasema huo huenda ukawa uvimbe mkubwa zaidi kuwahi kutolewa kwenye ubongo wa binadamu.
Upasuaji huo, ambao ulidumu saa saba, ulifanyika mnamo 14 Februari katika hospitali ya Nair mjini Mumbai magharibi mwa nchi hiyo.
Lakini taarifa za upasuaji huo hazikutangazwa moja kwa moja kwa sababu madaktari hawakuwa na uhakika iwapo ulifanikiwa.
"Sasa ni suala tu lake kupona, lakini maisha yake hayamo hatarini tena," Dkt Trimurti Nadkarni, mkuu wa upasuaji wa mfumo wa neva, ameambia BBC.
Santlal Pal, mwuzaji duka kutoka jimbo la Uttar Pradesh kaskazini mwa India, amekuwa akiishi na uvimbe huo kwa miaka mitatu.
Madaktari wanasema Pal alipoteza uwezo wake wa kuona kutokana na uvimbe huo.
Hata hivyo, kuna matum
Mke wake ameambia gazeti moja India kwamba alikuwa ameambiwa na madaktari katika hospitali tatu tofauti Uttar Pradesh kwamba uvimbe huo hauwezo kuondolewa.
"Visa kama hivyo huwa hatari sana," Dkt Nadkarni alisema, na kuongeza kwamba Pal alihitaji painti 11 za damu wakati wa upasuaji huo.
Aidha, alitumia mtambo wa kumsaidia kupumua kwa siku kadha baada ya upasuaji huo.
aini kwamba huenda akapata uwezo wa kuona tena baada ya kupona.
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kwamba kuwapatia walimu silaha kunaweza kuzuia mashambulio ya risasi katika shule kama lile lililowaua watu 17 wiki iliopita mjini Florida.

Baada ya mauaji ya watu 17 katika shule moja Florida 14 Februari, na mwaka jana kufuatia kuuawa kwa watu 59 jijini Las Vegas, Nevada watetezi wa udhibiti wa silaha nchini Marekani wameanza kuzidisha kampeni yao.
Ni kisa ambacho kinaonekana kuwa cha kawaida, kwani hilo hutokea kila baada ya mauaji kutekelezwa kwa kutumia bunduki.
Katika ngazi ya taifa, licha ya utafiti kuonyesha kwamba watu wengi wangependa kukazwa kwa sheria za kuwaruhusu watu kumiliki silaha, bado hakuna hatua iliyochukuliwa kutunga sheria kwa miongo kadha.
Miongoni mwa mambo ambayo hupendekezwa ni uchunguzi zaidi wa historia na maisha ya mtu kabla yake kuuziwa silaha.
Aidha, kupigwa marufuku kwa bunduki zenye uwezo mkubwa sawa na zile zinazotumiwa na jeshi.
Baada ya idadi kubwa ya watu kuuawa wakati huu, huenda shinikizo za kufanyika kwa mabadiliko zitazidi.
Hapa chini ni sababu nne ambazo zimezuia kufanyiwa mageuzi kwa sheria kuhusu silaha Marekani.

Tanzania kutengeneza ndege aina ya helikopta

Ndege aina ya helikopta
Raia nchini Tanzania wameamkia habari za kushangaza kwamba taifa hilo linaunda ndege.
Gazeti la Tanzania la Daily News limeripoti kwamba ndege hiyo aina ya helikopta inakaribia kukamilika na kwamba habari hiyo imekuwa ikisambaa barani Afrika kwa kasi.
Gazeti la Zambia, Observer linasema kuwa lengo la ndege hiyo itayokuwa ikibeba watu kwa bei rahisi itakabiliana na matatizo ya uchukuzi nchini humo.
Huku gazeti la Cameron, Concord likisema kuwa mradi huo ni wa kihistoria linaongezea kuwa lengo lake ni kutengeza ndege 20 kwa mwaka.
Ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba watu wawili inakaribia kukamilika katika chuo cha ufundi cha Teknolojia cha Arusha na itaanza kufanyiwa majaribio ya kuruka angani baada ya kuruhusiwa na mamlaka ya uchukuzi wa angani nchini Tanzania kulingana na Daily News.

Uingereza yaamua kujiondoa kwenye EU

Asilimia kubwa ya raia wa Uingereza wamepiga kura ya maoni wakiitaka ijiondoe kwenye muungano wa bara Ulaya EU.
Huku asilimia kubwa ya kura zikiwa zimekwisha hesabiwa, asilimia 52% ya raia wa Uingereza wamepiga kura ya kumaliza uanachama wa Uingereza ndani ya EU uliodumu miaka 43.
Watu wanaoishi katika mji London na Scotland ndio waliopiga kura kwa wingi kusalia ndani ya muungano huo.
Wandani wa maswala ya afisi ya waziri mkuu bwana David Cameron,wanasema kuwa sasa Britain imeingia katika eneo jipya.
Wadadisi wa maswala ya kisiasa wanahofu athari za kujiondoa kwa Uingereza kwenye muungano huo utabainika katika masoko ya hisa huku kukitarajiwa athari kubwa kiuchumi kisiasa ndani na nje ya bara Ulaya
Sarafu ya Euro imepanda katika masoko ya fedha huku Paundi ya Uingereza ikiendelea kuporomoka ikiwa ni ishara kuwa wafanyabiashara wanatarajia Uingereza kubakia ndani ya Umoja wa Ulaya.
Kwa mujibu wa ripoti waliojitokeza kupiga kura hiyo ya maoni inaonyesha kuwa wengi.
Hadi sasa ni majimbo machache ndio hayametangaza matokeo yao na inaonyesha mchuano ni mkali kati ya wanaotaka kubakia na wale wanaotaka Uingereza kujiondoa ndani ya Umoja huo wa Ulaya.

Marekani yakerwa na ziara ya Assad Moscow

Assad na Putin


Marekani imeshutumu Urusi kwa kumpa mapokezi ya taadhima Rais wa Syria Bashar al-Assad mjini Moscow.

"Tunatazama mapokezi ya zulia jekundu aliyopewa Assad, aliyetumia silaha za kemikali dhidi ya watu wake, kuwa kinyume na lengo lililoelezwa wazi na Urusi la kutaka kuwepo na shughuli wa mpito kisiasa Syria,” msemaji wa ikulu ya White House Eric Schultz amewaambia wanahabari.

Afisa wa wizara ya masuala ya ndani ya Marekani alisema taifa hilo halijashangazwa na ziara hiyo, lakini wasiwasi mkubwa kwa Marekani ni Urusi kuendelea kumsaidia kivita Assad.

Alisema hilo litaipa nguvu zaidi serikali ya Assad na hivyo kuendeleza mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

Ziara hiyo ya kiongozi huyo wa Syria Jumanne ilifanyika wiki tatu baada ya Urusi kuanza kushambulia kwa ndege ngome za wapiganaji wa Islamic State na makundi mengine yanayopinga utawala wa Assad.

Ilikuwa ziara ya kwanza kabisa kwa Assad nje ya nchi baada ya mapigano kuzuka Syria 2011. Mapigano hayo ya wenyewe kwa wenyewe yameua watu 250,000.

Akiwa jijini Moscow, Assad alitoa shukrani zake kwa Urusi kuingilia kati kijeshi nchini mwake.

Alisema operesheni hiyo ya Urusi ilikuwa imezuia ugadi kueneza zaidi na kuwa madhara makubwa Syria.

Kwa upande wake, Bw Putin alisema matumaini ya Moscow ni kwamba suluhu ya muda mrefu itapatikana kupitia mchakato wa kisiasa na kwa kushirikisha makundi yote ya kisiasa, kikabila na kidini.

Mwandishi wa BBC aliyeko Moscow Steve Rosenberg anasema kuwa kwa kumkaribisha kiongozi huyo wa Syria mjini Moscow, Putin alikuwa akituma ujumbe mkali kwa mataifa ya Magharibi kwamba Moscow ni mhusika mkuu katika mzozo huo Mashariki ya Kati na kwamba suluhu haiwezi kupatikana bila kuhusisha Urusi.

Daktari bandia aliwaambukiza Ukimwi watu 100


Mwanaume mmoja aliyejidai kuwa daktari na kuwaambukiza watu zaidi ya mia moja virusi amefikishwa mahakamani nchini Cambodia.

Yamkini daktari huyo bandia alikuwa akiwadunga wagonjwa wake kwa sindano aliyokuwa ameitumia kwa mgonjwa aliyekuwa na virusi vya Ukimwi.

Yem Chhrin anakabiliwa na kosa la kuua na kuambukiza watu ugonjwa huo kwa kukusudia.

Aidha Bw Yem anashtakiwa kwa kuwalaghai watu kuwa ni daktari ilhali hana vyeti halali vya kuhudumia umma.

Iwapo atapatikana na hatia mahakama ya nchi hiyo huenda ikamhukumu kifungo cha maisha jela.

Waathiriwa walioambukizwa maradhi ya Ukimwi wanatokea katika kijiji cha Roka kilichoko Kaskazini Magharibi.

Mmoja wao ni kiongozi wa kidini wa madhehebu ya Buddha na mtoto wa miaka mitatu.

Takriban 10 kati ya waathiriwa hao wanakisiwa kuwa wameshakata roho.

Kwa mujibu wa ripoti za mahakama daktari huyo bandia amekiri kuhudumu bila vyeti maalum ila anakana kukusudia kuwaambukiza watu hao 100 virusi vinavyosababisha maradhi ya Ukimwi.

Assad afanya ziara ya ghafla Moscow

Assad na Putin


Rais wa Syria Bashar al-Assad amefanya mashauriano na Rais wa Urusi Vladimir Putin baada yake kufanya ziara ya kushtukiza Moscow.

Msemaji wa Rais wa Urusi Dmitry Peskov amesema Assad "alikuwa kwenye ziara ya kikazi Moscow" Jumanne na alifanya mazungumzo na Bw Putin.

Mwishoni mwa mwezi jana, ndege za kijeshi za Urusi zilianza kushambulia maeneo yanayodhibitiwa na wapinzani wa Assad nchini Syria.

Urusi imejitetea na kusema inashambulia tu makundi ya kigaidi na wapiganaji wa Islamic State.

Bw Peskov ameambia wanahabari kwamba viongozi hao wawili walijadiliana kuhusu viva hivyo alivyosema ni dhidi ya magaidi.

Aidha, walizungumzia kuendelea kwa mashambulio ya ndege za Urusi na mpango wa Syria kuhusu wanajeshi. Haijabainika iwapo Bw Assad bado yuko Moscow au amerejea Damascus.

Hiyo ndiyo ziara ya kwanza kabisa kufanywa na Bw Assad nje ya nchi tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria 2011, runinga ya serikali nchini Syria imesema.

Taarifa kuhusu mazungumzo hayo iliyotolewa na Kremlin inaonyesha Bw Putin akieleza Syria kama “rafiki” na kusema Urusi iko tayari kuchangia “sio tu kijeshi…bali pia katika mchakato wa kisiasa” kurejesha Amani nchini humo.

MHE. CHIKU GALLAWA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUSISITIZA AMANI NA UTULIVU WAKATI WA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 25

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=15089a284161b429&attid=0.1&disp=inline&realattid=f_ifzdor3g0&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ_0ZZFy9et6HUs4A6LKnhB0gMl8R03ISTH3JaXIkzS_f_rNqCgm78qTlFe1R8Etle97KfC71-WjtTejLJO0ppkcW8c3xU91bzFRYtHunPaLygsQcOslphtJo_a_xnk0d7NsuAFYOMWPLeIJUZgvx0mnOGx8wqD94WdGnU6LVcOQYJqEHZgX9IQzbo8-M3YQPjfXUn3Pj4yeznRC7jhuYMJNAMmj4OFkix0qxaqLkLxl7KUn8Q87aeIIA_L4Qs9GMc8Mr1jiCqMwjiw5qCZcXSKN9jhPXZyaF5LdLwuZJqp4hSFgLyobTwWFmViOpbpiBZwGvAiXz0hnR2ZxtzvVrgbJItnw2ijad2mgz9HFsiuJ3_dPFtxnI84vd4CX0d9xAmlNMI52zJdJoBQP2NdDbE_0AQt9Fz5GccxYJycWfAr-Dgst0Z4Ts2ZdclBoI2spcg_9IP04t7AcdP8RS4c5a-6v0obwrKJfXSkQuzys_MVv7szXcZqm06Z4DIcnYltQ5rpKVzzhzgqXXC0RrVkzdpoDsOA6ELRsdepveyYFiaGmgQ_oyF6UbnXnUzwfvrNBdY9yx4A-VwxpOR6qiuzHIEScMeazgtJjjy5aVgJGvWO41rYqf74p2FYXCBwMkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Gallawa akifungua Mkutano wa viongozi wa dini mkoani humo uliojadili masuala ya amani na utulivu wakati wa  uchaguzi Mkuu Oktoba 25


 https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=15089a284161b429&attid=0.2&disp=inline&realattid=f_ifzdorfh1&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-keXo4YPC0GMZkmLS5Ay-RJJx4XLvLnK7lilTnOmiCzjNf3rZKySnO1ZzlkrxeKgO2WVZfTAfvBdE1TTohDVWhdtHm_f4pc8yREFzf8RaaO-nZBUbINjOFL-E2jOwNF9f7TKk0MpgWeLfy0nJcFDoZpqQoMGARtm-SgkMWm0HKcv0UlqAokuCFBHDVsg8mkfwTCnfwMT01UU7805RXaKG26gU1-vh-UhbSOg5kEEkrRUcYhxwH9bNGeAPO-cxFf4P_-FacbK9arLtXHtzkfhN9V80DU6NaI_gw_QlwQxrsiOPKmPkzb-FL2gKL7ujfKZUkAfBN_FF45mnkI4j57UKJ07OWnhzYHHArFRDY1iLz4v5pTqtEwRhk1piOL-mwF1P5yF7IczaCYkEE_tj_4E7R3WwyiLDtFQ-4CJUVB52Kt2gAS1T9zpEuJeG4WiC8Ls7LIW9xNXSfMDeJ9Wm0P3AB0XpS057usoXp1mGKfY9yu5KHzPYVDkFaTR-AqWFzl6u-GoYemzSPDU1zAMhvsUjNU3HD14mA9vevRAvZ_fiZ6FfPrnaR5cj7p3_DZq0ZtqiuYMwPU1LpispmCSjGn_aKf8QvfeU9Tfq7PzolMBJnimCtaG6EubnPMCwhttps://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=15089a284161b429&attid=0.3&disp=inline&realattid=f_ifzdorjo2&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-_xxcQ2x-xSoOR8-XHgkoiwGksjtxX_NaOGRNG2Lq5iWzkrO045rCj6MXO3zJCDnmRPrxK2UP3PWRXtFpoal28qE3-Tzw7AIRl6vWk9nY04jRqXBVs038Zm5pQuMVSY_-JZBsaoFO00YHSEqa0PjxYxpPWs_cZCKKSvBrVW9qBku4SZQCKkrBXR9amrJHm5FjyT3QV5oRcQ_hXz6X3Li4cbFI1YuKYNhtD9pf4-ZK_27M2zZPxHqXm-jQqnh95ZsPWIRvgSN3tm9x4gJvL_39QtYzKcojP_IGV-HRvfyKE6rO8U5QJAXBvcFD9mZVIXoZ-1td189-JBVghbvnx2nam9nWvIIOrIf6OrSOQMqdspNaT2Co5rCBhEdO35_rTiUjlhVPa9n5v6rWlvWdNfiVo6GeP95rTwnKlTN7zJ4HMCRwZ2-FIlXfX-CxzE3-U8I22qQ7hJLF1sr2c4eoWeotMK37W-lJQVB8EhAyQSCuAqpkP8a6ntW3LacdCugrW4uZICItPQClFWy-t20BKxN3vNfLsj6ny7ywoWMNi4QcgeCmqs0DUZn8Lk9D9K-1nZZrX2qZp-A4v1g-QhYsHiGRFPSBW5zQ4yDJb7MasI58uj0WxVU3CsXbMkck Viongozi wa dini waliohudhuria Mkutano ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mapema leo kujadili masuala ya amani na utulivu wakati wa  uchaguzi mkuu oktoba 25.

 
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=15089a284161b429&attid=0.4&disp=inline&realattid=f_ifzdormw3&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ92_ttW4lvyP1IWNyJCL0VtQgLnZbVyb70wOEvPyieWZ9GJff5igHNi3c5lN2FSOHxq91SlGwqRjT0Q04yTkZjlXSOFZwqkHdfjaC-_I2bpTgSeK3kK2pGWJZzJQORqcVjmtR8k52v9wGVXF8uTTzD6pwOJ3qu8Yip__aWMF-NuXnSEKDbbbmLn1O-1Q1f2UogTLK2rXoweuu2I6Bff_2U_RY4D0OFpXKpjfEfO4mzt33vu0kjT84dbqlJ7ghYgkcsoHuc4yATA2gh7xttGI_HlZp-iHKIlBJkh0QEQzSBh6UlFgI-fAbBRtE6uvUqiVwfjd6YJDpmwD_DOgL6YSVE81qhgK_bksKLZvgalS_QPnR16gIOT9LgQTZ5oAGjh6dXyJAcGb-ItoGZBPurK9hdaiQYjWFO38q4RVsXRW3Qu88N1EBH1HBFjG33xwDtSw06WvfbuB5_rTZMKiYfbf_v3-WLpmmQM9MrdYvtgiUB3fLle2XFIGTv3qKrQvCGyMeAtS8XB1-_-6R5g5vJYV3gGBRS5aPbCLLZc9cE2NLDbEI5O9WV2lqiF3l6hFn1pwh-gi2ECSe0PGzZ4TAfuAU2A07ZZckBT1JMc95VigWg-gUZKgMtUvi3-rPE 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma SACP David Misime akifafanua jinsi jeshi la polisi Dodoma lilivyojipanga kusimamia amani na utulivu wakati wa uchaguzi mkuu oktoba 25 mapema leo kwenye kikao cha viongozi wa dini kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

 

MGOMBEA WA NAFASI YA UBUNGE JIMBO LA DODOMA MJINI KUPITIA CCM ANTHON MAVUNDE AMECHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA NAFASI YA UBUNGE

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.8&disp=inline&realattid=f_idk1tyua7&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ8gtH7LnENcq6iQD9J0xV0QJ_zlqMGR5mSd4T00uci0soRiiMSfScQ1r37a0GlCnh527rEIEM-FA65FZqyJ82hdLB3daZ8dxd32gsgqCg7NtAyHZLSOvXx7IfEa5cbN0wOnFfU7MjyfvLNd2ShWdI44rsihergcBe0wstch-G54uVp2-6oPMv-fTSZ7C8wfQfQtURR4C3qnTbrY2_WFG5C_2-5Qji9hLoVvwlpF5816ZALcCCE6rKrkDGL9qbJNKVS3kTLkVL6I6A-YRxK2p1IXmHmPa9tkF0NN3StCkyuNATseZ5b-MeUrCqsiMXSW6aSw6myHYbKbTDmA23x99x8dw_m9naTMuUGVPMz-ZpnvUSk5JYHTtAfm8l22NTrsV6WAiVjqxXl3OqnrQTjdMkIpe3auqVFpT7xXDlaCJQGOHHPu4xLWcImgh5LUrpwdzKubJpGILn7m-lYE1kxyTyaW_Mgo6nzRXMhIAZM-Tv0N3h0jXuvXjRVhoen1bILhMOaTcq6Cno2HmTgW7pnd-f_-gvzg_KtEuLVNxzXOk9jlsdQevwn1GMIE-mrrlBkv9oZU384FAsCRnVIe
 https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.10&disp=inline&realattid=f_idk1tyum9&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ8XV-ybd1gZvDloZ6RlOGffROG2F42W2COfFRzdON6-qHoxmcqUbw3NV1jY9mmkS2iHgDXc4v-0vnvkeOo0GfjNWYGw2Rxh9wdFy7f1rh-OhCfmH3E81ZUEuchd_MycTOmmbZO86OJIdeoNiPOl2sqDL3ZutjOP6rIAUZrtdUquOHl1G1ILoi65hmumjY7za97RxsF4TEOYP9hiNZ1gV_StQvVAQd8T4cYsdIVRTcNRhzYF25rHDhCj5pERJeiqE-goLY0_eLFJmEZUmOSSBbWPvbMGTsV5-DEvd-7J3rPom-2V7xe-pkP80hTtS2r9KJMGTywkZLT0iYSyTgX_3rzIIpAU7aa8L5u_w7G6DzpTijo5wjXubDap8vV8SmyNrHKdtxcQx30YXZAOIrqtc7vYVJgOyBgEvBVzaaGFjooAp__bNd80B1VYQl6VBQk7xBdYQGqIMLFgg929SH-jVZqQvSfBrUQ4f1WcEXT5iOmyXerW2Zp_P86TqcxQAdyDTmb_OvNKhg5YIqOfsFSRICGdF3Fyv6KWR_iNtcZpWHH-HgATDGJNWbJLzIIohdJWbbk43uPt3eX6BOLa

 Mgombea ubunge kupitia chama cha mapinduzi [CCM] Jimbo la Dodoma Mjini  Anthon Mavunde akipokea Fomu za kugombea nafasi ya ubunge Toka kwa Afsa Uchaguzi Manispaa ya Dodoma Elizabert Gumbo mjini Dodoma jana.

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.3&disp=inline&realattid=f_idk1tysy2&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ_r0hIUapbZ75usLfih3crOKxFRITHheyW7iGsaD-aAaqX1jS8kLZ8i83uLg2uVbpKlPpOztaMKOAGg7urSODlfPuektSpGR0El6h4t9cYOLBEHtf1nFrQpY9d6xmp88hKVJuv2xeoUM8Knzlezf79VLDe2112_kxydiKqNPZNFQVp7-3a5N87-w1KepjqHzHDx6UbG92N2mbmH2wZti_ouPL38duHm5exDz4Ec-YzzaHEXGmdbzuiatGJXNT3ogtzlckMOn6NCWieOLRU0sElS9fRXVhg1lLVMZYLYCgCRpQyPg3OWKozrrzMJkdPiD-538VRdGu7iftvcROgx9_DItASfwEIPNSxhO_OJg96fER9BQeTg2wNv8TW3ePskzaIwt7thzKIi3zGqM3a2ExSwI1SVEPhnkR_P_uFvEYd74BSm6KU2dgd67fJgHSjgVHdmkCoU1ePyiDczQ7MOiX9i1in2oycFMfnW2ZNcgdhCTuTNp9PITMWbPYdXYqiqUBcer-Fg6nvrARe3c-PJvryf5udtwujSeynUDSMc5UWq7KS5y8PGHJPX_6Las0SAQx5A_ismM2WQXvVi

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.2&disp=inline&realattid=f_idk1tyso1&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ8wNhUbab6K6hxP1-tQKvE7RQUjpKLJPVL0xCrBNntgB6Z0qJGqzhV4s_NbzVdtOWKcSQQJTbzntqlyr_ILqTnLp2mvZljuzBO92WqpDBtEsJmb9cDuhMBzFqF-Iy_rl1KToTYsrHKXsYH_6L1MabrovWE0qeLBINY_UUJiQ-J1TF--FDUF1mx4dMzbfcQktk57R7TIWY9rNFTv6by-x2DjWGUXZSVjZV6xvWZw2_5b66zoMhAmzBllekXRSrGgxqhUjRyw-KwSQgFO-juisbJYhiJVcDviqn1Kvh7g8b1giVVQfwKY8I-wVrIjioSN9YSJLNBBmbb7AV1RLgypdDXG6CfYyNgAYUAyu9w_ovxEZaVmmB6fPt7Swj2t2oT3Yu0kd_Tm5NNt3VwoCfSg661ioN81XQCJLfONtjy8tO6T5IkN-BHBs-q74FOclKETC07RPN-IiKluWoi-QaHF8gH2tIFuwyTAQFclJ3m_3heUZS0FAaID0HjcPM4S7mlNe6EC9QAIiTfeJS7EreIiCTXUvH1UAn6DHFcOTeQtMoC7t6gYDrEugus6fWnTQxpeEV2vS776Vz0xSOSQMavunde akionyesha Fomu hizo baada ya kuzichukua katika ofisi za manispaa ya Dodoma  jana.

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.7&disp=inline&realattid=f_idk1tyu46&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ8Aw0yl7KwiQpIX84CHU-lK-3WfldADbyOT6yrWVWZTKXDdsOjF9hJT1uiGKb7aTXmtCt0GDxKyFDlGLW2kfOImwqknHEiL5TPgj8tY-GF9p0kA0ZG21ukarw-DFr_jSuczKgpcRXD_NIqLemfNXISZDyLjcdmIeaZU-fSFWWnyUO1OkpIQcup7T6gmWNeArl7bGsp75fhHIUNb8LSjUry76_kOoASi97QfKRVFbf5sG7FrZX8l4ARlrzobIcgby0zTqN2QWoIxNb4q_EnI8QC4o_C0wf6J7XH4S0ourptOcq19ORbUTAhbRqCUxkwexuPbYBu_6WPg9Lv7LNukakrMBAI4LhHr-ZqvTkhckHPvar9Ky6iNdAgaM1tMZX5ZqHkFEXSO7PBreWgxED6ieKl9AkwTrdKcTMw1JhsVTQIbYobIOZmFxu-8vmqgkPD5TDkrJJ_03FRHX5Pr4DGsoCNcRxROVGrenZC2eVUKWeCFm6QnEjQnAFWHoVt-zpsresMO34lCcnjPVdmQB0jTMWLXNZ2QxMy9lZ4JbzevTYEz5XZUrE5I6lVq3H5VeLh6YizhF9VTBfwExdkYBaadhi ya wafuasi wa Chadema wakionyesha ishara ya vidole viwili ambayo ni alama ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini wakati msafara wa Mgombea Ubunge Kupitia CCM Anthon Mavunde ulipokuwa ukipita kwenda kuchukua Fomu za kugombea nafasi hiyo katika barabara kuu eneo la Nyerere Square, hivi karibuni kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma alikitaja kitendo hicho cha kuingiza itikadi ya chama kingine pasipohusika kama viashiria vya uvunjifu wa amani.

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.4&disp=inline&realattid=f_idk1tyt63&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ9h2Hw3M5pCg5PGv4DyY_0eSdFY_Db6CYmwfHywZ7E8e5uhM2B2D-wlkL0SdREE847ADscjx7sIJdx5OlFiWNfjwoGpTfOGYdtU6NuMuiz1GMMIbjp1-jjFh06JuyKSJYYkSb-8nRwoARnOppi3d7FuIO1tUp6-9yUa74RDOLVV5gUOk44ZswszP1GM-1RgLUcVZs8IlpVtMXXXZaFMMGYrI30DqOn-F8VD1kftKkXZYV_u7Y5Fjy4XAEBOCo5Ghi7cYDsy1wiv0PT_pfrrBqhH4MF6Yi65j-pZD2XjZVpUGgCXJS-5s77wz71jWDhHO2YLvPnlqbHiL2kDlkLotulWtkTRAe81yrgjJpP7NbfE7XFnt8D1EHssbFYiou7KUMZE0x7HVKeU_WoXJNnHvDCpjh9-7AwTQKTfTGWNRppz9gZgk2vNKQ_pXL2qPOu4tka8ODjN87AClvIITXD3jz7w0rWC4KCshn4aD2hcRkSieqXDX1oZfUtPJseCyZIKUI_nWPyJ-5O81fL2hGgFSxjYM1JF4NOxtgWE70TsUlR37IrkfNpn5zDWvnoHSleBeBeniTsDFmB606n4 

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.9&disp=inline&realattid=f_idk1tyug8&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-Bdk9_sbHhkqOg9u5VYkVCk0qmugvAZwUbcKwfOOdZst4HBODfDqoQYAhiYs2hBE1I8BgT1-PLekf5lB5nGJW4bXAtNseXYG1yODujwcp0yNj-Bq9JYA8sSVTANZlydq9ZxNFssIMD7aOig8kQBiHeBT32owGWlr-Qm5Rp1Q7_9pOq1lqp4KX-3MFji0Cf2y6-z6XncRpRHJp2Vvm2L7qRZaY7awiKjF4EkxZLeTWUJi8-vgCDWBRacRjyCSgU5eFiOzDJ_Yyg-Tkx_S-VaJCyFwVrgFH-xs2n1sNAnJSodFfGduvBD9pqc1cYJ9SrMD79qJH-fVl7HMMLx3deW9T3m4SCA1TvPUnJSj6th7qtDYjjJBiQ3pHN9AFWqwlRVybRA293XC4Kk_MeWgYnRQ32bBY55A8-6pQTv8LRQ1ce3OETebFOtUqPEBLj17gh_2Lv1_OF1RTZt0WiUI3nVFI4lUbgjDngMotEobbqEd7nSZ1TEJDDtZ2P9xNBd4ZHf83vJgEBEHXDQyux_iGGn88op_GbvRcNBvGxfHn_cmVqsXFgEqtt2-9eRf-B1yQhBOvL7iRRx27HHAma 
Mgombea Ubunge jimbo la Dodoma mjini kupitia CCM Anthon Mavunde akiwapungia watu Mikono juu ya Gari wakati alipokuwa akienda kuchukua Fomu za kugombea nafasi hiyo.

PICHA NA JOHN BANDA