Boti la wakimbizi lazama Ziwa Albert


Mili 25 imepatikana Ziwa Albert baada ya boti iliyokuwa imebeba wakimbizi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuzama.

Wakimbizi wa mapigano mashariki mwa Congo

Wakimbizi hao walikua wakitoroka kutoka kambi ya wakimbizi ya Kyangwali wilayani Hoima magharibi mwa Uganda, wakirejea kwao.

Kwa sasa Jeshi la polisi linaendelea na jitihada za kutafuta miili zaidi. Kamanda wa polisi wa eneo hilo John Ojukuna amesema watu 43 wameokolewa. Boti iliyozama inadhaniwa kuwa ilikua imebeba zaidi ya wakimbizi 100.

Wengi wa wakimbizi hao ni wale waliokimbia mapigano mashariki mwa Congo mwaka jana.

Mwendeshaji wa boti hiyo amekamatwa na jeshi la polisi na inadaiwa kuwa alikua amelewa. Wakimbizi waliookolewa wameambia polisi kuwa alikuwa mlevi na alikua akiendesha boti hiyo kwa kasi sana.

Hii sio mara ya kwanza ajali ya boti kuua watu katika Ziwa Albert kutokana na kujaza abiria na mizogo kupita kiasi.Miaka minne iliyopia boto nyingine ilizama na kusababisha vifo vya watu 70.

No comments:

Post a Comment