Bunge hatarini kuvunjika,adai mjumbe

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mustapha Akunaay.

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mustapha Akunaay, amesema kuna hatari kubwa la Bunge hilo kuvunjika kutokana na kauli iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akihutubia wajumbe wa bunge hilo.

Akunaay ambaye pia ni Mbunge wa Mbulu (Chadema), alisema bila tahadhari, kuna hatari kubwa ya Bunge hilo kuvunjika.

Alitoa kauli hiyo, kufuatia Rais Kikwete kuzungumzia kwa undani na kusema muundo wa serikali tatu haufai na hauwezi kutekelezeka.

Alisema wao kama wajumbe na wabunge hawakutakiwa kulizungumzia suala la serikali mbili au tatu kwa sababu suala hilo lilishaamuriwa na wananchi.

“Rais Kikwete amezungumzia sana kuhusu serikali mbili kwa hiyo amewachanganya watu kuhusu muundo wa serikali mbili au tatu, sasa hali hii itakuwa ngumu zaidi kwenye kufanya uamuzi,” alisema.

“Maana dakika za mwisho kaja kusema kwamba msije mkaanza kung’ang’ania mambo ya kura, lazima mfanye mambo ya makubaliano...kwa hiyo mimi nimeachwa asilimia 30 kwa 70, alisema.

No comments:

Post a Comment