Lugola: JK amemziba mdomo Warioba

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Kangi Lugola.

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Kangi Lugola amesema hotuba iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete imemziba mdomo Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.

“Tulitarajia itakuwa hivyo na ndiyo maana kulikuwa na ubishi kwa nini Rais Jakaya Kikwete asingetangulia kwa mujibu wa kanuni halafu ndiyo aje Mwenyekiti wa Tume wa Mabadiliko ya Katiba, Jaji  Warioba,” alisema.

Alisema hotuba  iliyotolewa na Rais Kikwete imekwenda mbali zaidi kwa sababu na yeye alikuwa anachangia katika utungaji wa katiba kutokana na kuchambua kifungu kwa kifungu.

“Nimemsikiliza...nimeyatafakari yale yote ambayo ameyatoa kwenye hutuba yake...kwa sababu alitoa msamiati kwamba tumia akili ya kuambia na uchanganye na ya kwako...basi ametuambia na sisi tutaenda kuchanganya na akili yetu katika kutunga katiba ya wananchi,” alisema.

Naye, Mjumbe wa Bunge hilo, Aden Rage alisema watahakikisha kwamba wanachukua ushauri wa Rais Kikwete ikiwa ni pamoja na kuweka maslahi ya taifa mbele.

“Tutaweka maslahi ya taifa mbele...interest (maslahi) ya nchi kwanza...tutashindana kwa hoja, na kuwahakikishia wananchi kupata katiba inayofaa,” alisema.

No comments:

Post a Comment