Waponea kifo mikononi mwa Boko Haram


Jeshi linaendelea kuwasaka wapiganaji wa Boko Haram

Wasichana waliotekwa nyara na kundi lenye itikadi kali za kidini, Boko Haram nchini Nigeria, wameielezea BBC ukatili walio upitia mikononi mwa kundi hilo.

Wakati wakizuiwa, wasichana hao walishuhudia watu kadhaa wakiwemo baadhi wanaotoka kijiji kimoja na wapiganaji wa kundi hilo, wakikatwa shingo.

Msichana mmoja mwenye umri wa miaka 23, ameiambia BBC kwamba ameona kiasi ya raia hamsini wakiuawa mbele yake na Boko Haram.

Hili limefanyika miezi kadhaa iliyopita katika kambi moja katika eneo la mashambani, la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Wakati huo huo msichana mwingine alieleza jinsi wapiganaji hao walivyo mlazimisha kumuua mwenziwe ambaye pia alitekwa nyara.

Wote walifanikiwa kutoweka kutoka kambi hizo na sasa wanaishi mafichoni.

Jeshi la Nigeria linasema linaendelea kuwasaka wapiganaji wa kundi la Boko Haram katika eneo hilo lililo mashinani.

Wapiganaji hao wanaendelea kuyashambulia miji na vijiji katika kiwango cha kushtusha ambapo zaidi ya raia mia tano wameuawa katika wiki za kwanza za mwaka huu.

No comments:

Post a Comment