Mgomo mwengine wapamba moto A Kusini

Wanachama wa NUMSA
Wachimba migodi wa Afrika Kusini wamekataa nyongeza ya mishahara iliyopendekezwa na makampuni ya migodi.

Chama cha wachimba migodi, NUMSA, chama kikubwa kabisa cha wafanyakazi Afrika Kusini, piya kimetishia kuwaomba maelfu ya wafanyakazi katika sekta mbalimbali kujiunga na mgomo wao.

Wanachama wa NUMSA, katika sekta ya chuma cha pua na kutengeneza mashini walianza mgomo kama wiki mbili zilizopita - na kusababisha kiwanda kimoja cha kutengeneza zana za magari kufungwa; na kuzusha hofu kuwa uchumi wa Afrika Kusini unaweza kuzorota tena.

Mgomo huu wa sasa umeanza punde baada ya wachimba dhahabu nyeupe kurudi makazini baada ya mgomo wa miezi mitano.

No comments:

Post a Comment