Wapalestina wakimbia Gaza kaskazini

Wapalestina wahama Gaza kaskazini
Mamia ya Wapalestina wamekuwa wakikimbia sehemu za kaskazini za Gaza, baada ya Israel kuonya kuwa italenga sehemu hiyo katika mashambulio yake ya sasa.

Umoja wa Mataifa umenukuliwa ukisema kuwa watu kama 4,000 tayari wameomba hifadhi katika hifadhi ya muda.

Jumamosi usiku mashambulio ya ndege za Israel yaliendelea Gaza.

Wapalestina zaidi ya 160 wameuwawa hadi sasa.

Hamas imerusha makombora zaidi dhidi ya miji ya Israel pamoja na Tel Aviv; hakuna mtu aliyekufa Israel.

Israil ilisema wanajeshi wane walijeruhiwa waliposhambulia eneo ambapo makombora yakirushwa.

Hamas inasema wanajeshi wa Israil hawakuwahi kufika ardhini.

No comments:

Post a Comment