Watu 17 wa familia moja wafariki Gaza

Makombora ya Israel yalipua majumba katika eneo la Gaza

Maafisa wa Palestina wanasema kuwa watu kumi na saba wa familia moja wameuawa baada ya makombora ya Israel kuharibu nyumba moja ya ghorofa tatu ya mkuu wa polisi wa Hamas.

Tayseer Al-Batsh anadaiwa kujeruhiwa katika shambulizi hilo.

Mashambulizi hayo yanajiri baada ya wapiganaji wa Hamas kurusha makombora ya masafa marefu katika miji ya Israel ikiwemo Tel Aviv.

Maafisa wa Israel wanasema kuwa makombora mawili ya Roketi yalirushwa kutoka lebanon lakini yakaanguka katika eneo lililo wazi kazkazini mwa Israeli.

Na katika hatua ya kulipiza kisasi ,Israel ilirusha makombora nchini Lebanon na kuzidisha hofu kwamba huenda mzozo huo ukapanuka.

Takriban raia 150 wa Palestina wameuawa katika mashambulizi hayo huku ikiwa hakuna vifo vyovyote vilivyoripotiwa nchini Israel.

No comments:

Post a Comment