MGOMBEA WA NAFASI YA UBUNGE JIMBO LA DODOMA MJINI KUPITIA CCM ANTHON MAVUNDE AMECHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA NAFASI YA UBUNGE

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.8&disp=inline&realattid=f_idk1tyua7&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ8gtH7LnENcq6iQD9J0xV0QJ_zlqMGR5mSd4T00uci0soRiiMSfScQ1r37a0GlCnh527rEIEM-FA65FZqyJ82hdLB3daZ8dxd32gsgqCg7NtAyHZLSOvXx7IfEa5cbN0wOnFfU7MjyfvLNd2ShWdI44rsihergcBe0wstch-G54uVp2-6oPMv-fTSZ7C8wfQfQtURR4C3qnTbrY2_WFG5C_2-5Qji9hLoVvwlpF5816ZALcCCE6rKrkDGL9qbJNKVS3kTLkVL6I6A-YRxK2p1IXmHmPa9tkF0NN3StCkyuNATseZ5b-MeUrCqsiMXSW6aSw6myHYbKbTDmA23x99x8dw_m9naTMuUGVPMz-ZpnvUSk5JYHTtAfm8l22NTrsV6WAiVjqxXl3OqnrQTjdMkIpe3auqVFpT7xXDlaCJQGOHHPu4xLWcImgh5LUrpwdzKubJpGILn7m-lYE1kxyTyaW_Mgo6nzRXMhIAZM-Tv0N3h0jXuvXjRVhoen1bILhMOaTcq6Cno2HmTgW7pnd-f_-gvzg_KtEuLVNxzXOk9jlsdQevwn1GMIE-mrrlBkv9oZU384FAsCRnVIe
 https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.10&disp=inline&realattid=f_idk1tyum9&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ8XV-ybd1gZvDloZ6RlOGffROG2F42W2COfFRzdON6-qHoxmcqUbw3NV1jY9mmkS2iHgDXc4v-0vnvkeOo0GfjNWYGw2Rxh9wdFy7f1rh-OhCfmH3E81ZUEuchd_MycTOmmbZO86OJIdeoNiPOl2sqDL3ZutjOP6rIAUZrtdUquOHl1G1ILoi65hmumjY7za97RxsF4TEOYP9hiNZ1gV_StQvVAQd8T4cYsdIVRTcNRhzYF25rHDhCj5pERJeiqE-goLY0_eLFJmEZUmOSSBbWPvbMGTsV5-DEvd-7J3rPom-2V7xe-pkP80hTtS2r9KJMGTywkZLT0iYSyTgX_3rzIIpAU7aa8L5u_w7G6DzpTijo5wjXubDap8vV8SmyNrHKdtxcQx30YXZAOIrqtc7vYVJgOyBgEvBVzaaGFjooAp__bNd80B1VYQl6VBQk7xBdYQGqIMLFgg929SH-jVZqQvSfBrUQ4f1WcEXT5iOmyXerW2Zp_P86TqcxQAdyDTmb_OvNKhg5YIqOfsFSRICGdF3Fyv6KWR_iNtcZpWHH-HgATDGJNWbJLzIIohdJWbbk43uPt3eX6BOLa

 Mgombea ubunge kupitia chama cha mapinduzi [CCM] Jimbo la Dodoma Mjini  Anthon Mavunde akipokea Fomu za kugombea nafasi ya ubunge Toka kwa Afsa Uchaguzi Manispaa ya Dodoma Elizabert Gumbo mjini Dodoma jana.

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.3&disp=inline&realattid=f_idk1tysy2&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ_r0hIUapbZ75usLfih3crOKxFRITHheyW7iGsaD-aAaqX1jS8kLZ8i83uLg2uVbpKlPpOztaMKOAGg7urSODlfPuektSpGR0El6h4t9cYOLBEHtf1nFrQpY9d6xmp88hKVJuv2xeoUM8Knzlezf79VLDe2112_kxydiKqNPZNFQVp7-3a5N87-w1KepjqHzHDx6UbG92N2mbmH2wZti_ouPL38duHm5exDz4Ec-YzzaHEXGmdbzuiatGJXNT3ogtzlckMOn6NCWieOLRU0sElS9fRXVhg1lLVMZYLYCgCRpQyPg3OWKozrrzMJkdPiD-538VRdGu7iftvcROgx9_DItASfwEIPNSxhO_OJg96fER9BQeTg2wNv8TW3ePskzaIwt7thzKIi3zGqM3a2ExSwI1SVEPhnkR_P_uFvEYd74BSm6KU2dgd67fJgHSjgVHdmkCoU1ePyiDczQ7MOiX9i1in2oycFMfnW2ZNcgdhCTuTNp9PITMWbPYdXYqiqUBcer-Fg6nvrARe3c-PJvryf5udtwujSeynUDSMc5UWq7KS5y8PGHJPX_6Las0SAQx5A_ismM2WQXvVi

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.2&disp=inline&realattid=f_idk1tyso1&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ8wNhUbab6K6hxP1-tQKvE7RQUjpKLJPVL0xCrBNntgB6Z0qJGqzhV4s_NbzVdtOWKcSQQJTbzntqlyr_ILqTnLp2mvZljuzBO92WqpDBtEsJmb9cDuhMBzFqF-Iy_rl1KToTYsrHKXsYH_6L1MabrovWE0qeLBINY_UUJiQ-J1TF--FDUF1mx4dMzbfcQktk57R7TIWY9rNFTv6by-x2DjWGUXZSVjZV6xvWZw2_5b66zoMhAmzBllekXRSrGgxqhUjRyw-KwSQgFO-juisbJYhiJVcDviqn1Kvh7g8b1giVVQfwKY8I-wVrIjioSN9YSJLNBBmbb7AV1RLgypdDXG6CfYyNgAYUAyu9w_ovxEZaVmmB6fPt7Swj2t2oT3Yu0kd_Tm5NNt3VwoCfSg661ioN81XQCJLfONtjy8tO6T5IkN-BHBs-q74FOclKETC07RPN-IiKluWoi-QaHF8gH2tIFuwyTAQFclJ3m_3heUZS0FAaID0HjcPM4S7mlNe6EC9QAIiTfeJS7EreIiCTXUvH1UAn6DHFcOTeQtMoC7t6gYDrEugus6fWnTQxpeEV2vS776Vz0xSOSQMavunde akionyesha Fomu hizo baada ya kuzichukua katika ofisi za manispaa ya Dodoma  jana.

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.7&disp=inline&realattid=f_idk1tyu46&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ8Aw0yl7KwiQpIX84CHU-lK-3WfldADbyOT6yrWVWZTKXDdsOjF9hJT1uiGKb7aTXmtCt0GDxKyFDlGLW2kfOImwqknHEiL5TPgj8tY-GF9p0kA0ZG21ukarw-DFr_jSuczKgpcRXD_NIqLemfNXISZDyLjcdmIeaZU-fSFWWnyUO1OkpIQcup7T6gmWNeArl7bGsp75fhHIUNb8LSjUry76_kOoASi97QfKRVFbf5sG7FrZX8l4ARlrzobIcgby0zTqN2QWoIxNb4q_EnI8QC4o_C0wf6J7XH4S0ourptOcq19ORbUTAhbRqCUxkwexuPbYBu_6WPg9Lv7LNukakrMBAI4LhHr-ZqvTkhckHPvar9Ky6iNdAgaM1tMZX5ZqHkFEXSO7PBreWgxED6ieKl9AkwTrdKcTMw1JhsVTQIbYobIOZmFxu-8vmqgkPD5TDkrJJ_03FRHX5Pr4DGsoCNcRxROVGrenZC2eVUKWeCFm6QnEjQnAFWHoVt-zpsresMO34lCcnjPVdmQB0jTMWLXNZ2QxMy9lZ4JbzevTYEz5XZUrE5I6lVq3H5VeLh6YizhF9VTBfwExdkYBaadhi ya wafuasi wa Chadema wakionyesha ishara ya vidole viwili ambayo ni alama ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini wakati msafara wa Mgombea Ubunge Kupitia CCM Anthon Mavunde ulipokuwa ukipita kwenda kuchukua Fomu za kugombea nafasi hiyo katika barabara kuu eneo la Nyerere Square, hivi karibuni kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma alikitaja kitendo hicho cha kuingiza itikadi ya chama kingine pasipohusika kama viashiria vya uvunjifu wa amani.

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.4&disp=inline&realattid=f_idk1tyt63&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ9h2Hw3M5pCg5PGv4DyY_0eSdFY_Db6CYmwfHywZ7E8e5uhM2B2D-wlkL0SdREE847ADscjx7sIJdx5OlFiWNfjwoGpTfOGYdtU6NuMuiz1GMMIbjp1-jjFh06JuyKSJYYkSb-8nRwoARnOppi3d7FuIO1tUp6-9yUa74RDOLVV5gUOk44ZswszP1GM-1RgLUcVZs8IlpVtMXXXZaFMMGYrI30DqOn-F8VD1kftKkXZYV_u7Y5Fjy4XAEBOCo5Ghi7cYDsy1wiv0PT_pfrrBqhH4MF6Yi65j-pZD2XjZVpUGgCXJS-5s77wz71jWDhHO2YLvPnlqbHiL2kDlkLotulWtkTRAe81yrgjJpP7NbfE7XFnt8D1EHssbFYiou7KUMZE0x7HVKeU_WoXJNnHvDCpjh9-7AwTQKTfTGWNRppz9gZgk2vNKQ_pXL2qPOu4tka8ODjN87AClvIITXD3jz7w0rWC4KCshn4aD2hcRkSieqXDX1oZfUtPJseCyZIKUI_nWPyJ-5O81fL2hGgFSxjYM1JF4NOxtgWE70TsUlR37IrkfNpn5zDWvnoHSleBeBeniTsDFmB606n4 

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=14f4aadbd00999ff&attid=0.9&disp=inline&realattid=f_idk1tyug8&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-Bdk9_sbHhkqOg9u5VYkVCk0qmugvAZwUbcKwfOOdZst4HBODfDqoQYAhiYs2hBE1I8BgT1-PLekf5lB5nGJW4bXAtNseXYG1yODujwcp0yNj-Bq9JYA8sSVTANZlydq9ZxNFssIMD7aOig8kQBiHeBT32owGWlr-Qm5Rp1Q7_9pOq1lqp4KX-3MFji0Cf2y6-z6XncRpRHJp2Vvm2L7qRZaY7awiKjF4EkxZLeTWUJi8-vgCDWBRacRjyCSgU5eFiOzDJ_Yyg-Tkx_S-VaJCyFwVrgFH-xs2n1sNAnJSodFfGduvBD9pqc1cYJ9SrMD79qJH-fVl7HMMLx3deW9T3m4SCA1TvPUnJSj6th7qtDYjjJBiQ3pHN9AFWqwlRVybRA293XC4Kk_MeWgYnRQ32bBY55A8-6pQTv8LRQ1ce3OETebFOtUqPEBLj17gh_2Lv1_OF1RTZt0WiUI3nVFI4lUbgjDngMotEobbqEd7nSZ1TEJDDtZ2P9xNBd4ZHf83vJgEBEHXDQyux_iGGn88op_GbvRcNBvGxfHn_cmVqsXFgEqtt2-9eRf-B1yQhBOvL7iRRx27HHAma 
Mgombea Ubunge jimbo la Dodoma mjini kupitia CCM Anthon Mavunde akiwapungia watu Mikono juu ya Gari wakati alipokuwa akienda kuchukua Fomu za kugombea nafasi hiyo.

PICHA NA JOHN BANDA   

Majimbo Ukawa hadharani, 12 bado moto

Wananchi wa Unguja wakimshangilia mgombea urais
Wananchi wa Unguja wakimshangilia mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa hadhara yuliofanyika katika Uwanja wa Demokrasia Kibanda Maiti, Zanzibar jana. Picha na Othuman Michuzi  

Dar es Salaam. Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimetangaza mgawanyo wa majimbo 253 kati ya 265 ya ubunge huku 12 yaliyokuwa kwenye mvutano yakibaki kiporo.

Katika mgawanyo huo uliotangazwa kwa wanahabari jana, Chadema kimepata majimbo 138, sawa na asilimia 73 ya majimbo yote huku CUF ikichukua 99, NCCR – Mageuzi 14 na NLD matatu.

Hiyo ni pamoja na kujumlisha majimbo 51 ya Zanzibar ambayo yote yalikwenda kwa CUF isipokuwa moja lililoachwa kwa Chadema.

Mgawanyo huo ambao umechapishwa katika ukurasa wa 36 wa gazeti hili, umetangazwa wakati mgombea urais wa Ukawa akihutubia mkutano wake wa nne wa kujitambulisha kwa wananchi katika Uwanja wa Demokrasia, Kibandamaiti, Zanzibar; baada ya kufanya hivyo katika mikoa ya Mbeya, Arusha na Mwanza.

Majimbo hayo yalitangazwa na wawakilishi wa makatibu wakuu wa umoja, John Mnyika (Chadema), Nderakindo Kessy (NCCR – Mageuzi), Shaweji Mketo (CUF) na Masudi Makujunga (NLD) waliokutana katika Ofisi za Makao Makuu ya za NCCR – Mageuzi.

Miongoni mwa majimbo ambayo hayajagawanywa ni, Segerea, Kigamboni, Mbarali, Geita Vijijini, Gairo, Mtwara, Mpwapwa na Geita Mjini, Mwanga na Serengeti ambalo Katibu Mkuu wa NCCR – Mageuzi, Mosena Nyambabe jana alichukua fomu kuliwania.

Taswira ya mgawanyo

Chadema ambacho katika uchaguzi uliopita kilipata majimbo 24 dhidi ya manne ya NCCR-Mageuzi na mawili ya CUF Bara, kimeachiwa majimbo karibu yote katika mikoa ya Mara, Shinyanga, Geita, Njombe, Rukwa, Arusha, Manyara, Singida, Katavi huku Cuf ikibeba mkoa wote wa Lindi na NCCR-Mageuzi ikibeba ngome ya Kigoma.

Katika mgawanyo huo, NLD ambayo haikuwa na jimbo hata moja imeachiwa majimbo matatu tu ya Lulindi, Masasi na Ndanda mkoani Mtwara.

Katika mkutano huo, Kessy alisema uamuzi huo umefikiwa baada ya majadiliano ya muda mrefu, kuhusu kuachiana majimbo ya ubunge kwa vyama vinavyounda Ukawa.

Mnyika alisema katika uchukuaji wa fomu za Tume ya Uchaguzi, hatatambuliwa mgombea kutoka vyama hivyo, nje ya makubaliano yaliyofikiwa na Ukawa.

Akizungumzia mvutano wa baadhi ya majimbo, mfano Segerea, Mnyika alisema wananchi wanatakiwa kuvuta subira.

Vigezo

Mketo alitaja vigezo sita vilivyotumika katika mgawanyo huo kwa chama husika kuwa ni matokeo ya Uchaguzi wa Serikali Mitaa, matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, kukubalika kwa mgombea, hali ya kisiasa ndani ya jimbo na mtandao wa chama husika.

“Taarifa hii ni rasmi kutoka CUF kwani kila chama kilitoa mapendekezo ya majimbo ndani ya vikao vya Ukawa na yalijadiliwa kupima vigezo hivyo kwa hivyo tunaomba viongozi wote waheshimu uamuzi uliofikiwa,” alisema Mketo.

Agosti 2014, viongozi wakuu wa vyama vinavyounda Ukawa walisaini makubaliano (MoU) ya kusimamisha mgombea mmoja kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na urais wa Muungano na Rais wa Zanzibar.

Lowassa Zanzibar

Wakati huohuo, mgombea urais kupitia Chadema na Ukawa, Edward Lowassa jana alitambulishwa Zanzibar na kusema umefika wakati wa kuikomboa nchi dhidi ya mfumo kandamizi wa CCM.

Alisema jukumu la awali ni kuiondoa CCM madarakani na kutoa nafasi kwa rais kupitia Ukawa ili kuikwamua Tanzania kimaendeleo.

“Mkituchagua mimi na Maalim Seif (mgombea urais wa Zanzibar) mtaiona Tanzania inakwenda kasi ya ajabu, haijawahi kutokea. Hatuwezi kushindwa na Rwanda! Hatuwezi kuachwa na Malawi! Hatuwezi kushindwa na Kenya na Uganda! Tupeni nafasi tuikwamue nchi yetu kutokana na ufukara na umaskini,” alisema.

Kama ilivyokuwa katika mikoa ya Mbeya, Arusha na Mwanza, Lowassa alionya kuhusu mwenendo aliouita wa hujuma na ubadhirifu wa CCM hasa katika uchaguzi, akisisitiza kuwa hakuna msaada wowote wa kukinusuru chama hicho kikongwe kwa sasa kisiondoke madarakani kwa kuwa muda wake umekwisha.

“Ninawasihi ndugu zangu wale mliobaki CCM njooni haraka muungane nasi kuikomboa nchi hii, wakati ni huu, hakuna namna ya kuzuia wimbi hili la umma katika safari hii ambayo inaelekea katika ushindi wa kihistoria na mwisho wa utawala wa CCM,” aliongeza.

Lowassa aliweka msisitizo juu ya azma ya kusimamia kikamilifu mapendekezo ya Katiba kwa mujibu wa maoni ya wananchi kama yalivyowasilishwa na Tume ya Jaji Joseph Warioba.

“Hatuhitaji kusimama na batili ambayo haikuwa chaguo wala mapendekezo ya wananchi walio wengi, tutalinda masilahi ya Zanzibar katika Muungano kama nchi kamili yenye heshima yake,” alisema Lowassa.

Alisema iwapo atachaguliwa, Serikali yake itahakikisha haki za masheikh waliopo kizuizini zinapatikana haraka iwezekanavyo.

Mgombea mwenza, Juma Duni Haji alisema upepo mkali wa mabadiliko na nguvu isiyozuilika ya Ukawa dhidi ya CCM ni ujumbe tosha kwamba mwisho wa chama hicho umewadia.

“Someni yaliyojiri Urusi, Ukraine, Misri na kila pembe ya mabadiliko duniani, muangalie ni wapi dola iliposhinda nguvu za umma,” alihoji Duni ambaye hivi karibuni alijivua uanachama wa CUF, alikokuwa Makamu Mwenyekiti na pia kujiuzulu uwaziri katika Baraza la Mawaziri Zanzibar.

Maalim Seif

Akizungumza katika mkutano huo, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad alimtahadharisha Rais Jakaya Kikwete juu ya matumizi mabaya ya vyombo vya dola.

“Ndugu yangu, rafiki yangu kipenzi, Rais Kikwete nakuomba umechukua nchi kwa amani ondoka kwa amani,” alisema huku akilaumu tabia ya watu aliowaita “Janjaweed”, waliodaiwa kumpora Abdi Seif Hamad fomu ya kugombea Ubunge kupitia CUF katika Jimbo la Shaurimoyo jana.

Abdi ni miongoni mwa watu waliohama CCM siku za karibuni na kujiunga CUF kwa matarajio ya kuungwa mkono na Ukawa.

Mamia ya mashabiki jamii wa Kimasai walimiminika katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume kumlaki Lowassa na katika hali ambayo haikuzoeleka, walionekana kupiga saluti wakiwa wamejipanga barabarani wakati msafara wa viongozi wa Ukawa ukipita Barabara ya Kiembe Samaki, Mwanakwerekwe kuelekea Kibandamaiti.

Wamasai hao walimiminika kwa wingi uwanjani hapo na kupata fursa ya kuburudisha umati wa watu kwa wimbo wa Kimasai wenye maana ya ‘tunampenda Lowassa’.

Freeman Mbowe

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema safari ya Ukawa ni ndefu, imepitia majaribu mengi lakini bado umoja huo uko imara hivyo wananchi hawana budi kujitokeza kwa wingi kuunga mkono umoja huo kuelekea ukombozi wa pili wa Tanzania.

“Ndugu zangu tumetoka mbali tutasimama imara kuhakikisha safari yetu inafikia tunakohitaji katika mafanikio na ushindi na hatimaye kushika uongozi wa nchi,” alisema.

James Mbatia

Mwenyekiti wa NCCR, Mageuzi, James Mbatia alisema: “Tumeshawaagiza mawakili wetu kurekodi kila tukio kila udhalimu na kila uonevu, tunamuomba Bensouda (Fatou, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa) kufutilia namna zote za uvunjaji wa haki na ifikapo Novemba tunampeleka yeyote ICC.”

Khamis Mgeja

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja aliwahamasisha Wana-CCM kujiunga na Ukawa na kumpigia kura Lowassa, wakielewa kwamba hatima ya chama hicho kikongwe imewadia.

Wengine wachukua fomu za uraisi

Wakati mkutano wa Ukawa ukiendelea, wagombea wengine wa urais Zanzibar walijitokeza jana katika Ofisi za Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kuchukua fomu za kugombea nafasi hizo.

Waliojitokeza ni Juma Ali Khatib wa Tadea na Said Soud Said wa Chama cha Wakulima (AFP). Khatib ni Katibu Mkuu wa Tadea na Soud ni mwenyekiti wa AFP.

Imeandikwa na Kelvin Matandiko, Borrice Bwire (Dar) na Hussein Ali (Zanzibar).

Shambulizi la Thailand lalaaniwa

Shambulizi la Thailand lalaaniwa

Waziri mkuu wa Thailand ametaja shambulizi la bomu ambalo limewauwa zaidi ya watu ishirini mjini Bangkok hapo jana jumatatu kuwa kisa kibaya zaidi kuwahi kutokea nchini humo.

Prayuth Chan-o-cha amesema kuwa mtu ambaye mienendo yake sio ya kawaida ametambuliwa kwenye picha za kamera za usalama kabla ya mlipuko huo kutokea.

 
Shambulizi la Thailand lalaaniwa

Naye Waziri wa ulinzi nchini Thailand amesema kuwa mlipuko wa bomu uliotokea kwenye makutano ya barabara yenye shughuli nyingi katikati mwa jiji la Bangkok ulilenga kimakusudi wageni wanaozuru taifa hilo kwa nia ya kuvuruga utalii na uchumi wa Thailand.

Bado haijabainika ni nani aliyetekeleza shambulizi hilo lakini mkuu wa majeshi amesema kuwa mbinu zilizotumiwa hazifanani na zile zinazotumiwa na waasi wanaotaka kujitenga kusini mwa taifa hilo.

Mgeja, Guninita wajiengua CCM, wajiunga Chadema

Kutoka kushoto  ni aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM
Kutoka kushoto  ni aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa    Dar es Salaam John Guninita na aliyekuwa mwenyekiti Mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja ambao leo wamehamia Chadema. 
By Louis Kolumbia, Mwananchi Digital

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja na aliyekuwa mwenyekiti mkoa wa Dar es Salaam John Guninita wametangaza leo kuachana na CCM na kujiunga Chadema.

Makada hao wa CCM wametangaza kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Dar es Salaam leo.

Wakizungumza katika mkutano huo, makada hao wamesema wamechukua uamuzi huo baada ya kubaini CCM imepoteza mwelekeo na kwamba kinaendeshwa kibabe tofauti na misingi ya kuasisiwa kwake.

Wametolea mfano wa kukiukwa kwa demokrasia kulikofanywa wakati wa mchakato wa kutafuta mgombea urais wa chama hicho ambapo Dr John Magufuli aliteuliwa kupeperusha bendera ya CCM.

Hatua ya makada hao imekuja ikiwa ni siku moja tu tangu aliyekuwa mbunge wa chama hicho jimbo la Sikonge, Said Nkumba atangaze kuachana na chama hicho na kujiunga na Chadema.

Huo ni mwendelezo wa matukio ya makada na wabunge chama hicho kuhamia upinzani hasa Chadema kwani awali aliyekuwa waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa aliachana na CCM baada ya jina lake kukatwa na kamati ya maadili ya chama hicho.

Wengine waliohama CCM ni aliyekuwa mbunge wa Arumeru Magharibi, Goodluck Ole Medeye, aliyekuwa mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga ambaye pia ni naibu waziri Kazi na Ajira, aliyekuwa mbunge wa Kahama, James Lembeli, aliyekuwa mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM, Mgana Msindai na mbunge wa viti maalumu anayemaliza muda wake Esther Bulaya.

Polisi yazuia msafara wa Lowassa

Polisi wakiwa wamefunga barabara katika Kijiji
Polisi wakiwa wamefunga barabara katika Kijiji cha Maroro wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro, walipokuwa wakizuia msafara wa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa aliyekuwa akielekea Usangi, Mwanga kuhudhuria mazishi ya mwanasiasa mkongwe nchini, Peter Kisumo yaliyofanyika wilayani humo jana. Na mpiga picha maalumu. 

Jeshi la Polisi, jana liliuzuia msafara wa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa kwenda Usangi, wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro kushiriki mazishi ya kada wa CCM, Peter Kisumo, likitaka kupunguzwa kwa idadi ya watu.

Mbali na kuzuia msafara huo, chombo hicho cha Dola kimepiga marufuku shughuli za kutafuta udhamini kwa wagombea urais wa vyama vya siasa kuambatana na misafara.

Lowassa, ambaye aliwasili Kilimanjaro jana asubuhi kabla ya kuanza safari ya kwenda Mwanga, alijikuta akikumbana na kizuizi cha polisi walioziba barabara kwa magari yao eneo la Kijiji cha Mroro, mita chache kutoka Mji wa Mwanga, wakati akielekea na msafara wake katika Tarafa  ya Usangi kuhudhuria mazishi ya mwanasiasa huyo mkongwe aliyefariki wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.

Lowassa hakukubaliana na agizo la polisi la kumruhusu aendelee na safari na kuwaacha wafuasi wake kwenye msafara huo, ambao awali walitakiwa wasibebe bendera, lakini baadaye wakazuiwa.

Kisumo alizikwa jana katika mazishi yaliyohudhuriwa na maelfu ya waombolezaji, wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete.

“Kwa kuwa tumezuiwa na polisi, kitendo hiki kimeondoa mwafaka wa kitaifa kwamba mpinzani hawezi kumzika mtu wa CCM na wa CCM hawezi kumzika mpinzani.... mpasuko huu ni mkubwa. Wameyataka wao,” alisema Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia baada ya polisi kuwazuia.

“Kwa kuwa wametuzuia kwenda kumzika Mzee Kisumo, sisi tunarudi lakini Watanzania wapewe taarifa kuwa CCM inalipasua Taifa.”

Alipoulizwa sababu za polisi kuwazuia, Mbatia alisema: “Wanahofia Mheshimiwa Lowassa na msafara wake. Magari mangapi? Magari 10 tu ya Mheshimiwa Lowassa! Magari gani hayo?”

Ilivyokuwa

Msafara huo ulikuwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani ambao ni pamoja na Mbunge wa Moshi Mjini, Phillemon Ndesamburo, Joseph Selasini (Rombo), Mbatia na na Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mremaambaye pia ni Mbunge wa Vunjo pamoja na viongozi wa Chadema ngazi ya mkoa na wilaya.

Msafara huo ulipofika Mroro, ulikutana na kizuizi cha polisi pamoja na askari wa kuzuia ghasia waliowataka watoe bendera na kuachana na msafara huo.

Kutokana na kauli hiyo, Mbatia, ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) aliwataka madereva wa bodaboda kutoa bendera zao na kutoongozana na msafara, agizo ambalo walilitii na kuondoka lakini polisi walikataa magari kuvuka kizuizi hicho.

Baadaye, Mbatia alizungumza kwa simu na Inspekta Jenerali wa Polisi, Ernest Mangu  kabla ya kumpelekea simu Lowassa ambaye naye alizungumza naye na kusema wameruhusiwa, lakini askari waliokuwa wameweka doria walikataa kuwaruhusu.

Kutokana na hali hiyo, Mbatia baadaye alizungumza kwa simu na kudai anawasiliana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Fulgence Mponji  lakini askari waliokuwapo walidai kuwa wamepewa maagizo kuzuia msafara huo.

Msafara huo ulikaa eneo hilo zaidi ya saa mbili na baadaye polisi waliruhusu  gari ya Lowassa, Mbatia na Ndesamburo kupita, lakini watu waliokuwa kwenye msafara wabaki kitendo ambacho viongozi hao walikipinga na kuamua kurudi Moshi.

“Tumeongea na IGP, RPC lakini tunaambiwa OCD amekataa, tunataka Watanzania wajue kuwa CCM wameanza kupasua amani ya Taifa hili,” alisema Mbatia.

Baada ya kukubaliana, Mbatia aliwataka wananchi waliokuwa wanakwenda kwenye msiba kwa msafara wao kuingia kwenye magari na kuanza safari ya kurejea Moshi  na baada ya kufika Njia Panda Himo, walikutana na wananchi wengi waliokuwa wakitaka kumuona Lowassa na kufunga barabara.

Polisi walilazimika kutumia bomu la machozi kuwatawanya, lakini wengi waligoma kuondoka na Lowassa alilazimika kusimama kwenye gari na kuwapungia ndipo walipokubali kusogea pembeni kupisha msafara uendelee na safari.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Kamanda Mponji alikiri jeshi lake kuzuia msafara huo, akisema kazi yake ni kuhakikisha Rais anamaliza safari yake Kilimanjaro kwa amani.

Mazishi ya mwanasiasa huyo mkongwe yalitarajiwa kumkutanisha Lowassa na Rais Kikwete, marafiki wawili wa muda mrefu ambao katika siku za karibuni wanaonekana kutofautiana baada ya jina la waziri huyo mkuu wa zamani kuenguliwa kwenye mchakato wa urais kwa tiketi ya CCM mapema Julai.

Lowassa, ambaye amepitishwa na Chadema kugombea urais na ambaye ataungwa mkono na vyama vinne vya NCCR-Mageuzi, NLD, Chadema na CUF, anatarajiwa kuanza kusaka wadhamini leo mkoani Mbeya na baadaye ataelekea Mwanza.

Maandamano yazuiwa Mbeya

Lakini wakati akianza ziara hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi amesema katika taarifa yake kwamba wamekubaliana na viongozi wa Chadema kwamba hakutakuwa na maandamano, bali utakuwapo msafara wa kawaida bila kuathiri shughuli za wakazi.

Msangi alisema sababu kubwa ya kuafikiana hivyo ni za kiusalama kutokana na ukweli kwamba barabara inayotumika ni moja.

Misafara kwenda NEC marufuku

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi limepiga marufuku maandamano ya aina yoyote ya vyama vya siasa wakati wa kwenda kuchukua fomu, kuzirudisha na kutafuta wadhamini mikoani.

Hatua hiyo ya polisi imekuja ikiwa ni siku kadhaa baada ya wafuasi wa vyama viwili vikubwa; CCM na Chadema kujitokeza kwa wingi kuwasindikiza wagombea wao kwenda kuchukua NEC na kusababisha msongamano katikati ya jiji.

Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi, Abdulrahman Kaniki alisema kutokana na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi walioshindwa kufika kwa wakati katika shughuli nyingine za kijamii, wameamua kusitisha utaratibu huo.

Alisema misafara hiyo ilisababisha usumbufu na malalamiko mengi kutokana na wananchi kutopata huduma kwa wakati, wagonjwa kushindwa kufika hospitalini kwa wakati, kuchelewa ofisini na watu kushindwa kupata huduma za kijamii kutokana na maduka kufungwa.

Alieleza kuwa hali hiyo ilijitokeza siku walipochukua fomu wagombea urais wa CCM na Chadema, hivyo kwa sababu za kiusalama, polisi imesitisha maandamano ya aina yoyote.

Kaniki alisema unaandaliwa utaratibu maalumu wa kuwakutanisha wadau wote wa siasa ili kuona namna bora ya kuhakikisha mchakato mzima wa uchaguzi unafanyika katika hali ya amani na utulivu.

Viongozi wa vyama walonga

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, baadhi ya viongozi wa vyama ambavyo wagombea wake wameshachukua fomu, walipinga hatua hiyo ya polisi, wakisema ni sawa na  kuwanyima wananchi haki ya msingi inayokubalika kikatiba.

Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena  Nyambabe alisema polisi ilipaswa kuchukua hatua mara baada ya CCM kufanya maandamano yao, lakini si kutoa tamko hilo baada ya Chadema.

Alikanusha kuwapo kwa sababu za kiusalama, akieleza kuwa kazi ya polisi ni kulinda usalama na hivyo wanaweza kupanga maandamano yaanzie wapi na kuishia wapi ili kupunguza vurugu.

Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi  Dovutwa alisema jeshi hilo lilijichanganya kwa kutoa taarifa awali kuwa linaruhusu maandamano hayo, lakini akasema kama limejiridhisha kuwa kwa kufanya hivyo linalinda usalama wa raia, haoni kama kuna tatizo.

“Wapo sahihi kabisa kuzuia, kwani kuna madai kuwa baadhi ya vijana walifanya vurugu, walilewa. Kuna dalili za kuhatarisha usalama kwa mwenendo huo, ” alisema.

Mgombea wa urais kupitia TLP, Maxmillian Lyimo alisema polisi wanapotoa kauli wawe makini wasije kuonekana wanapendelea upande fulani kwani wakati wa CCM walikaa kimya, lakini baada ya Chadema ndipo wametoa tamko. Alisema wao ndiyo wenye jukumu la kulinda usalama wa raia na mali zao, hivyo wanapaswa kuhakikisha mikusanyiko hiyo inalindwa.

Katibu Mkuu wa CCK, Renatus Muabhi alisema watu wanatumia vibaya uhuru waliopewa, lakini akataka ieleze sababu ya kuzuia na kama ni usalama, ni wajibu wa polisi.

Mgombea urais kwa tiketi ya Chaumma, Hashim Rungwe alisema hakuna haja ya kuwepo kwa maandamano wakati kuna kampeni ambazo wafuasi na wanachama watahudhuria hadi wachoke.

Kauli ya Kova

Mapema jana, Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam ilisema haitatumia mabomu na nguvu wakati wa uchaguzi na badala yake itashirikiana na viongozi wa vyama vya siasa ili kudumisha amani na utulivu.

Kamanda wa kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova alisema polisi imejipanga kikamilifu kudhibiti vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Chachu ya kutuliza maumivu yapatikana

Wanasayansi nchini Marekani wamesema kuwa wamefanikiwa kutengeneza chachu yenye vina saba vinavyoweza kupunguza maumivu kwa kiasi kikubwa.

Chachu hiyo inaweza kubadilisha sukari kuwa hydrocodone dawa inayofanana na morphine ndani ya siku tatu mpaka tano. Kwa sasa inachukua mwaka mzima kuzalisha kundi la dawa za kutuliza maumivu kama hayo kutoka kwenye mmea aina ya popi.

Hata hivyo, watafiti kutoka chuo cha Stanford wamesema kazi zaidi inahitajika kwa sababu utafiti wao umeegemea zaidi kwenye matumizi ya chachu nyingi kutengeneza kidonge kimoja pekee cha kutuliza maumivu

Fidel Castro aandika barua ya wazi Cuba

http://ichef-1.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/08/13/150813231608_fidel_castro_open_latter_512x288_bbc_nocredit.jpg

Rais wa zamani wa Cuba,Fidel Castro

Rais wa zamani wa Cuba Fidel Castro ametimiza umri wa miaka 89 kwa kuandika barua ya wazi kwa taifa lake.

Barua hiyo ilichapishwa katika gazeti la serikali la Granma ambapo hajazungumzia lolote kuhusu ufunguzi wa ubalozi mpya wa Marekani jijini Havana utakavyofanya kazi na waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry.

Badala yake ameituhumu Marekani kwa kuisababishia hasara ya mamilioni ya dola baada ya miaka mingi ya vikwazo vya biashara baina ya nchi hizo mbili.

lakini amezungumzia maridhiano ya kihistoria kati ya nchi yake na Marekani.

Wananchi wacharukia ushindi wa Nape Mtama

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi  (CCM) Nape  Nnauye. 
By Haika Kimaro

Lindi. Hali katika Jimbo la Mtama si shwari baada ya kundi la wananchi kufanya maandamano ya kukataa matokeo ya kura za maoni yaliyompa ushindi Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye huku wakimtaka mpinzani wake achukue uamuzi mgumu.

Katika kura za maoni, Nape alipata kura 9,344 wakati Suleiman Mathew alipata kura 4,766.

Wakiwa wamebeba mabango yaliyoandikwa ujumbe wa aina mbalimbali kumpinga Nape na kuonyesha kumkubali Seleman Mathew, ambaye wanaamini ndiye aliyeshinda, wananchi hao walimtaka mgombea huyo atangaze kujiengua CCM, kama makada wengine waliochomoka chama hicho kupinga matokeo ya kura za maoni.

“Karibu Mathew, sisi hatuchaguliwi kiongozi, tuna imani na Messi wetu,” liliandikwa bango moja la karatasi la boksi baada ya wananchi hao kumpokea Mathew na baadaye kumsindikiza kutoka Mnazi Mmoja hadi kijiji cha Mtama, Kata ya Majengo ambako kulikuwa na watu wamekusanyika kwenye uwanja ulio karibu na ofisi za mbunge.

Akizungumza katika eneo la Mnazi Mmoja ambako alipokelewa na wananchi hao waliomtaka ahamie chama chochote cha upinzani, Mathew, ambaye aliwahi kuwa mchezaji wa Yanga na timu ya Taifa, alisema kuwa amesikia wito wa wazee wa jimbo hilo pamoja na wananchi wengine waliomuita kutoka Dar es Salaam na kumshawishi ahame chama.

Mathew alidai kuwa kulikuwa na mchezo mchafu katika kura za maoni na kwamba uongozi wa CCM wa wilaya hiyo ulishiriki kumuhujumu, akisema katibu wa wilaya hakutangaza matokeo halisi, jambo ambalo alisema linawakosesha amani wananchi wa Mtama.

Wakati Mathew akidai kuibiwa kura, katibu wa Wilaya ya Lindi Vijijini, Christina Bukwi alisema uchaguzi ulifanyika na kumalizika salama kisha kutangaza matokeo mbele ya mkutano wa waandishi wa habari na wanachama wote.

Alisema wagombea wengine walioshindwa kwenye uchaguzi huo walikubali na kusaini fomu, isipokuwa Mathew aliyeamua kukataa.

“Kama alikuwa na malalamiko angekuja ofisini, lakini mpaka sasa sijapokea taarifa zake ofisini na kila mgombea alikuwa na wakala wake kwa ajili ya kulinda kura za wagombea wao, kwa hivyo mimi sitambui hayo malalamiko yake,” alisema Christina.

Lakini Mathew alisema ameshauriwa kutochukua hatua yoyote hadi vikao vya juu vya chama vitakapomaliza uchambuzi wa mwisho wa wagombea ubunge na udiwani, huku akieleza kuwa ana ushahidi kuwa ameporwa haki yake.

Kuhusu taarifa kwamba alifuatwa kushawishiwa awe na subira, Mathew alidai kuwa alifuatwa na viongozi wa Serikali, akiwamo mkuu wa mkoa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliyemtaka kuwa mvumilivu mpaka Kamati Kuu itakapotoa matokeo.

“Ni kweli waliniita nikazungumza nao kwa sababu hawa ni viongozi wetu na walitambua Mtama kuna tatizo. Nilipoitwa kuonana na Waziri Mkuu, kubwa nililoambiwa ni kuwa mstahimilivu hadi Kamati Kuu itakapotangaza matokeo ndiyo maana nimekuja hapa kwa sababu lengo letu ni moja tusubiri hiyo tarahe,” alisema Mathew.

Akizungumzia sakata hilo, Nape alisema: “Mimi sizungumzii mambo ya mtu anayepiga kelele barabarani. Halafu ninyi Mwananchi mbona mnapenda kukuza mambo. Ni kwa nini niliposhinda kwa kishindo hamkuandika leo mnataka mambo hayo?”

Polisi wavamia Chama cha Wanajeshi Myanmar

Polisi wavamia Chama cha Wanajeshi Myanmar

Polisi na wanajeshi wa Myanmar wamevamia makao makuu ya chama kinachoungwa mkono na jeshi cha Nay-Pyi-daw.

Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa lakini waandishi wa habari katika eneo hilo wamesema kuwa hali ya sintofahamu katika chama hicho imesababishwa na ushindani mkali wa kung'ang'ania madaraka katika chama hicho kinachotawala miezi kadhaa iliyopita.

Na habari zinazotufikia hivi sasa ni kuwa Spika wa Bunge la Myanmar ameondolewa  uwemwenyekiti wa chama kinachotawala miezi mitatu kabla ya uchaguzi Mkuu.

 
Sintofahamu katika chama hicho imesababishwa na ushindani mkali wa kung'ang'ania madaraka

Mndani wa chama hicho ambaye hakutaka kujulikana alisema kuwa spika huyo ameondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na mtu asiyependelea mabadiliko ajulikanaye kama Thein Sein.

Ban Ki moon afanya maamuzi magumu

Babacar Gaye

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon, amesema amemfukuza mkuu wa kulinda amani toka UN nchini Afrika ya kati baada ya kutuhumiwa kuhusika na madai ya unyanyasaji wa watoto kingono.

Bwana Ban amesema mwanadiplomasia wa Senegal Babacar Gaye angeachia ngazi kama mkuu wa ujumbe. Ban aliongeza kuwa alipatwa na hasira na aibu baada ya taarifa hizo za unyanyasaji wa ngono na ukandamizaji kwa watoto.

Taasisi ya kutetea haki za binaadam Amnesty International imewatuhumu wanajeshi hao wa kulinda amani wa UN kwa kumbaka msichana wa miaka kumi na miwili na kumuua kijana na baba yake katika mji mkuu wa nchi hiyo Bangui, mapema mwezi huu.

Uchunguzi pia unaendelea namna wanajeshi hao wa umoja wa mataifa kuhusika na madai ya unyanyasaji dhidi ya wanajeshi wa Ufaransa mwaka jana.

Moto mkubwa wazuka Tianjin-China

Mji wa viwanda ukiteketea

Kumetokea mlipuko mkubwa katika mji wa China Tianjin-ambao ni mji wa Bandari kuu na sehemu ya viwanda katika eneo la kusini kaskazini mwa mji mkuu Beijing.

Video zilizowekwa katika mitandao ya kijamii zinaonyesha moto mkubwa na wingu kubwa la moshi lililotanda angani. Shirika la habari la nchi hiyo, Xinhua limesema mlipuko huo umetokea katika mji wa Tianjin Binhai ukanda ulioendelea kiviwanda uliopo karibu na bandari na watu wanakimbia katika eneo hilo kunusuru maisha yao. Mpaka sasa bado hakijajulikana chanzo kikuu cha moto huo ni nini.

Vifungu vyote vya sheria ya mtandao vilivyolalamikiwa na wadau vimerekebishwa.

Mkurugenzi wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA Dk Ally Simba amesema vifungu vyote vilivyolalamikiwa na wadau kuhusu sheria ya makosa ya mtandao vimefanyiwa marekebisho huku akiwataka wananchi hasa watumiaji wa mitandao kujiandaa kuipokea sheria hiyo.

Rai hiyo imekuja zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kuanza kwa sheria hiyo ambayo inatarajiwa kuanza Septemba mosi mwaka huu ambapo amesema kuanza kwa sheria hiyo kutasaidia mambo mengi sana ikiwemo kulinda mifumo ya msingi ya tehama na kutolea mfano wa mitandao ya simu za mkononi.

Kwa upande wake mtendaji mkuu wakala wa serikali mtandaoni Bw Jabri Bakari kwa sasa serikali inajitihadi kushirikiana na wadau wa sekta binafsi hasa wataalam wanaoshughulikia mifumo ya komputa kuhakikisha wanakutana mara kwa mara kwa ajili ya kujadili na kubadilishana uzoefu wa suala la usalama wa mitandao.

Mwenyekiti wa CCM wilayani Sumbawanga Bw Emmanuel Kilindu ajiuzulu.

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wa wilaya ya Sumbawanga mjini Bw Emmanuel Selemani Kilindu, amechukua hatua ya kujiuzulu wadhifa wake huo kufuatia kuhitilafiana kwa kiwango kikubwa na mbunge anayemaliza muhula wake, na kudai kuwa licha ya kukabiliana na changamoto nyingi za kiutendaji lakini pia anayaweka maisha yake kwenye hatari kubwa.

Akiongea na waandishi wa habari mjini Sumbawanga mbele ya baadhi ya wanachama wa chama cha mapinduzi, mwenyekiti huyo wa CCM Bw Kilindu amesema mbunge anayemaliza muhula wake katika jimbo la Sumbawanga mjini Aeshi Hilal, amekuwa akikiuka kanuni nyingi za chama ikiwa ni pamoja na kuwatumia wapambe wake kufanya vurugu hadi kufikia kutaka kuichoma moto ofisi ya chama hicho kwa maslahi yake, huku mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi ya wilaya hiyo Bw Michael Chifunda akimuunga mkono naye kwa kuachia ngazi.

Kwa upande wao baadhi ya wanachama wa CCM wakiongea kuhusu sakata hilo, wamesema chama sasa kimefikia mahali pabaya kwa watu kutumia fedha zao kuwagawa wanachama na viongozi pia na kuwa kwenye makundi, hali ambayo inaelekea kukidhoofisha chama hivi sasa.

Mkimbizi wa Burundi mwenye dalili za ugonjwa wa Ebola afariki mkoani Kigoma.

Hofu imetanda kwa wakazi wa mkoa wa Kigoma baada ya mkimbizi mmoja toka nchini Burundi kufariki kwa ugonjwa wenye dalili zinazofanana na ugonjwa wa Ebola.

Hofu hiyo imetokana na mkimbizi Buchumi Joel kufariki baada ya kuugua kwa zaidi ya wiki moja na kuzikwa mjini Kigoma kwa kuzingatia taratibu za afya, ambapo wamesema ni muhimu serikali kudhibiti raia toka nchi jirani ambao wamekuwa wakiingia bila kuzingatia au kupimwa afya zao hali ambayo ni hatari.

Akizungumzia tukio hilo, kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Kigoma, Shija Ganai ambaye pia ni afisa afya wa mkoa, amesema mkimbizi huyo alianza kuugua akiwa katika kambi ya wakimbizi Nyarugusu na baadaye kupelekwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Kigoma baada ya kuugua ugonjwa wenye dalili za ugonjwa huo hasa baada ya kuanza kutokwa damu katika sehemu zote za matundu ya mwili.

Ameeleza kuwa kutokana na hali yake na licha ya kwamba hawajathibitisha kama ameugua ugonjwa wa Ebola, tahadhari zote zimechukuliwa na serikali na mashirika ya afya kimataifa ili kuhakikisha ugonjwa wowote aliokuwa nao hausambai.

Wadukuzi wailiza Marekani

Mamlaka nchini Marekani imewamefungulia mashtaka ya jinai watu tisa baada ya kuhusika na wizi wa mtandaoni kabla ya kuchapishwa kwa niaba ya wafanyabiashara wa fedha.

Waendesha mashitaka walisema wadukuzi hao, walitumia mbinu kutengeneza mamilioni ya dolla ambazo hazikua halali.Miongoni mwa wanaoshitakiwa ni wadukuzi wa mtandaoni, wafanya bishara za hisa pamoja na wafanyabiashara wakubwa, ambao Walikua na matawi yao nchini Ukraine na Marekani.

Kundi hilo la wadukuzi mtandaoni, linadaiwa kudokoa zaidi ya habari mia moja na hamsini kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Mdhibiti wa masuala ya fedha wa Maekani pia amewafungulia mashtaka watu tisa na watu wengine ishirini na tatu pamoja na makampuni binafsi yakiwemo pia ya Urusi, Malta, Ufaransa na Cyprus ambao inasemekana walihusika na udanganyifu.

Dk Slaa: Niko salama, nitazungumza muda ukifika

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa (wa

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa (wa tatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wa Moshi Mjini (Chadema), Philemon Ndesamburo (wa pili kulia) na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Japhary Michael (kushoto) na viongozi wengine wa chama hicho walipomtembelea Slaa nyumani kwake Dar es Salaam jana. Picha na Mtandao

Dar/Moshi. Siku tatu baada ya Baraza Kuu la Chadema kuridhia kumpumzisha kwa muda Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa baada ya kutofautiana na Kamati Kuu kwa kumkaribisha waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kiongozi huyo amesema yupo salama na wakati mwafaka ukifika atazungumza ya moyoni.
Akizungumza kwa mara ya kwanza na gazeti hili tangu Chadema imkaribishe Lowassa na hatimaye kumpitisha kuwania urais kupitia muungano wa Ukawa, Dk Slaa alisema amekuwa akisikia mengi yakisemwa juu yake lakini yote yamekuwa yakimchekesha tu.
Hakuhudhuria vikao muhimu vya chama hicho na vile vya Ukawa, vikiwamo; wakati Lowassa akitambulishwa rasmi, akichukua fomu, kikao cha Baraza Kuu na juzi Mkutano Mkuu na hakuwa akipatikana kwa simu yake ya mkononi.
Wakati kimya kikitawala juu ya hatima yake, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika kuwa amejivua uanachama Chadema.
Lakini jana alisema: “Naangalia mambo mengi yanayoendelea kwenye mitandao halafu ninacheka tu, usifikiri sifuatilii, nafuatilia kinachoendelea na ninabaki nikicheka.”
Kuhusu hatima yake kisiasa na madai ya kujiuzulu uanachama ndani ya Chadema, alisema hawezi kuzungumza lolote kwa sasa na atafanya hivyo wakati mwafaka ukifika. “Usijali wakati wangu wa kuzungumza ukifika nitasema tu, sasa hivi nawaachia mzungumze, lakini nitazungumza,” alisema.
Kadhalika, alipoulizwa kuhusu taarifa zilizozagaa kuwa maisha yake yapo hatarini kwa kuwa anatishwa, Dk Slaa alisema hata hilo pia atalizungumzia wakati mwafaka ukifika.
“Ndiyo hayohayo ninayosema, wala msijali nitazungumza wakati ukifika,” alisema na kusisitiza: “Nipo salama.”
Dk Slaa alisema kwa sasa yupo mapumzikoni nje ya jiji la Dar es Salaam ingawa hakutaka kueleza ni eneo gani.
Juzi, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alifafanua tofauti iliyojitokeza kati ya Kamati Kuu ya Chadema na Dk Slaa wakati wa mchakato wa kumpokea Lowassa.
Katika mkutano huo wa Baraza Kuu la Chadema, Mbowe alisema wamekubaliana katibu mkuu huyo apumzike kwa muda... “Nina hakika kwa tabia na hulka za Dk Slaa… kwa sababu anajua tunampenda na yeye anakipenda chama hiki, tunamwombea kwa Mungu ampe nguvu na ujasiri wa kuona kwamba kauli ya wengi ni kauli ya Mungu.”
Ndesamburo na siri nzito
Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo na makada wengine wa Chadema, jana walikwenda kuonana na Dk Slaa nyumbani kwake na kufanya naye kikao cha faragha.
Picha zilizomuonyesha Ndesamburo akiwa na Dk Slaa na makada wengine akiwamo Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Jaffar Michael, zilisambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii jana na kuibua mijadala.
Baadhi ya waliochangia mijadala hiyo walidokeza kuwa huenda Ndesamburo anayeheshimika ndani ya chama hicho alikwenda kujaribu kusawazisha hali ya mambo.
Mkuu wa Idara ya Habari wa Chadema, Tumaini Makene alikiri kuwa picha hizo ni halisi, baadhi zilipigwa juzi na nyingine jana mchana, lakini hakutaka kuingia undani wa mkutano wa wanasiasa hao.
Ndesamburo alithibitisha kukutana na Dk Slaa: “Ni kweli tulikwenda, kwani kuna tatizo gani? Si mzee mwenzangu? Halafu bado ni mwanachama wetu, hajatoka Chadema, hivyo tuna kila haki ya kwenda kumsalimia.”
Alipoulizwa kama alikwenda kumsihi Dk Slaa arejee kuendesha mapambano ya kuing’oa CCM, Ndesamburo alisisitiza kuwa walikwenda kumsalimia.
Michael alipoulizwa nia ya safari hiyo alijibu kwa kuuliza; “Dk Slaa ni katibu mkuu wetu kwani tunazuiwa kwenda kumsalimia?”
Dk Slaa aligombea urais mwaka 2010 na kushika nafasi ya pili baada ya Rais Jakaya Kikwete na ndiye aliyekuwa akitajwa kuwania tena nafasi hiyo kupitia Chadema na Ukawa kabla ya “kubadili gia angani” na kumteua Lowassa.

Japan yakumbuka shambulio la Hiroshima

Raia wa Japan wamefanya maombi leo
Raia wa Japan leo wanaadhimisha kumbukumbu ya miaka 70 tangu shambulio la kwanza la bomu la Atomiki kutekelezwa mjini Hiroshima.
Takriban watu laki moja na arobaini walikadiriwa kupoteza maisha baada ya Ndege ya Marekani kudondosha bomu ambalo liliuharibu mji huo tarehe 6 mwezi Agosti mwaka 1945.
Watu elfu sabini walipoteza maisha papo hapo, huku wengine wa idadi kama hiyo walipoteza maisha kutokana na athari za mionzi ya sumu.
Katika hotuba yake, Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe alisema kumbukumbu ya Heroshima inasisitiza uhitaji wa kufanya jitihada ya kupiga vita matumizi ya Nuklia.
Shambulio la Hiroshima lilifuatiwa na shambulio jingine la bomu la Atomiki katika mji wa Nagasaki.
Japan ilijisalimisha siku kadhaa baadae, hatua iliyomaliza vita ya pili ya dunia.

Hofu baada ya boti iliyojaa wahamiaji kuzama Libya

Hofu baada ya boti iliyojaa wahamiaji kuzama Libya
Waokoaji wanaendelea na shughuli ya kuwasaka mamia ya wahamiaji waliotumbukia baharini baada ya boti walimokuwa wakisafiria kwenda Ulaya kuzama majini katika bahari ya Mediterrania karibu na ufuo wa Libya.
Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa takriban watu 700 walikuwa kwenye mtumbwi huo uliozama baada ya kukumbana na mawimbi makali.
Wanajeshi wa majini kutoka Ireland wanakisia kuwa idadi kubwa ya watu wamekufa maji.
Aidha shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka Medecins Sans Frontieres (MSF) limeonya kuwa huenda kukazuka maafa makubwa kufuatia idadi kubwa ya abiria waliokuwa kwenye mtumbwi huo uliozama.
Inakisiwa kuwa takriban wahamiaji 2,000 walikufa maji kwanza mwanza wa mwaka huu wakijaribu kufika ulaya kupitia bahari hiyo ya Mediterranea
Meli nne za uokozi na ndege tatu zimetumwa huko kujaribu kunusuru maisha ya wahamiaji hao.
Takriban watu 700 walikuwa kwenye mtumbwi huo uliozama
Walinzi wa Ufuo wa bahari ya Uitaliano wamesema boti hiyo ya uvuvi iliyokuwa imebeba mamia ya wahamiaji.
Inavyoelekea boti hiyo ilikumbwa na dharuba lakini pia ilipenduka pale watu walipokurupuka upande mmoja walipoona chombo kingine kilichokuwa kikienda kuwasaidia.
Zaidi ya watu 150 wameokolewa lakini wengine wengi wanahofiwa wamekufa maji.
Msemaji wa shirika linalohusika na maswala ya wahamiaji IOM, Leonard Doyle ameiambia BBC kuwa
''Lazima tukumbuke kuwa hawa ni watu ambao hawajazoea usafiri wa baharini kwahivyo waliogopa.''
''Na wakati walipoona chombo kingine kinakuja kuwaokoa wakataharuki na kukurupuka upande mmoja''.
Zaidi ya watu 150 wameokolewa lakini wengine wengi wanahofiwa wamekufa maji.
Hilo ndilo tunalokariri kuwa hao walanguzi wa kusafirisha watu hawajali kabisa kuhusu maisha ya wahamiaji hao licha ya kuwa wamewalipa pesa nyingi kwa safari hizo hatari''.
Kwamba mkasa wa aina hii unaweza kutokea wakati ambao hata watu wamepelekewa chombo cha kuwaokoa karibu yao ni jambo la kusikitisha sana.

PICHA ZA UFUNGUZI WA MAONYESHO YA NANENANE NA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI KITAIFA INAYOFANYIKA MKOANI DODOMA


Wanafunzi wa shule ya msingi ya  Nhinhi wiyani Chamwino wakicheza ngoma ya kabila la kigogo wakati wa Uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya Unyonyeshaji maziwa ya mama kwa mtoto kwa miezi sita yaliyofanyika katika kijiji cha Nghwenda katika mfurulizo wa wiki ya hiyo inayofanyika kitaifa mkoani Dodoma

Mtoto Mwenye umri wa miaka saba akingoza kikundi cha nyota katika upigaji na uchezaji wa ngoma wakati kikundi hicho kilipokuwa kikiwatumbuiza wakili, wafugaji na watu mbalimbali wanaohudhuria maonyesho ya Nanenane yanayoendelea kikanda mkoani Dodoma kabla ya Mkuu wa mkoa huo kuyafungua Rasmi maonyesho hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Gallawa, akiangalia mazao aina ya Uwele ambayo inashauriwa kulimwa kwa wingi katika mikoa ya kanda ya kati kutokana na mazao hayo kustahimili ukame.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Gallawa akipokea Nyanya aina ya NOR FI toka kwa Mkuu wa kitengo cha mafunzo ya kilimo cha kisasa wa Clabu ya Vijana wasomi wa Elimu ya juu Agrikolas Masigati wakati mkuu huyo wa moa alipotembelea Banda la maonyesho la Wilaya ya Kondoa katika viwanja vya maonyesho ya nanenane jana

Nahodha wa Timu ya mpira wa miguu ya Watoto wa Town ya kijiji cha Nhinhi Babuu Abel akipokea zawadi ya Mpira toka kwa Katibu Tawala wa mkoa wa Dodoma Rehema Madenge baada ya timu yake kushika nafasi ya pili kwenye mchezo wa fainali wa maadhimisho ya siku ya unyonyeshaji ambapo nafasi ya kwanza ilienda kwa Small Boys iliyopata zawadi ya Jezi.

Baadhi ya wanawake na wanaume wakiwa na watoto wao kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Unyonyeshaji kitaifa inayoendelea mkoani Dodoma yaliyofanyika katika kijiji cha Nghwenda kata ya Nhinhi wilayani Chamwino.

PICHA NA JOHN BANDA