Wadukuzi wailiza Marekani

Mamlaka nchini Marekani imewamefungulia mashtaka ya jinai watu tisa baada ya kuhusika na wizi wa mtandaoni kabla ya kuchapishwa kwa niaba ya wafanyabiashara wa fedha.

Waendesha mashitaka walisema wadukuzi hao, walitumia mbinu kutengeneza mamilioni ya dolla ambazo hazikua halali.Miongoni mwa wanaoshitakiwa ni wadukuzi wa mtandaoni, wafanya bishara za hisa pamoja na wafanyabiashara wakubwa, ambao Walikua na matawi yao nchini Ukraine na Marekani.

Kundi hilo la wadukuzi mtandaoni, linadaiwa kudokoa zaidi ya habari mia moja na hamsini kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Mdhibiti wa masuala ya fedha wa Maekani pia amewafungulia mashtaka watu tisa na watu wengine ishirini na tatu pamoja na makampuni binafsi yakiwemo pia ya Urusi, Malta, Ufaransa na Cyprus ambao inasemekana walihusika na udanganyifu.

No comments:

Post a Comment