Palestina yapandishwa hadhi na UN


Wapalestina walisherehekea sana kufuatia tangazo hilo

Baraza la umoja wa mataifa limepitisha kwa kauli moja kwa wingi wa kura kupandisha hadhi ya eneo la Palestina.

Nchi mia moja thelathini na nane ziliunga mkono hatua ya kuitambua Palestina kuwa nchi ambayo si mwanachama wa Umoja wa mataifa lakini itaruhusiwa kushiriki katika shughuli za umoja wa mataifa.

Mataifa tisa yakijumuisha Isarael na Marekani yalipiga kura ya kupinga mpango huo huku mataifa arobaini na moja yakisusia shughuli hiyo.

Kura hiyo yenye umuhimu mkubwa sasa inaiwezesha Palestina kuwa na ushirika na umoja wa mataifa na mashirika mengine kama vile mahakama ya ICC.

Mwandishi wa BBC amesema kuwa wapelestina wanaweza kutumia nafasi hayo kuishataki Israel kwa kusababisha visa vya dhulma dhidi ya ubinadamu katika ngome yake.

No comments:

Post a Comment