Vita dhidi ya Al Shabaab vinaathiri raia-UN

Mwanajeshi wa serikali akishika doria mjini Mogadishu

Umoja wa mataifa umesema kuwa mashambulizi makubwa ya kijeshi yaliyofanywa nchini Somalia na Wanajeshi wa Umoja wa Afrika, AMISOM, dhidi ya makundi ya wapiganaji wa Kiislamu, yanaweza kuwaathiri watu milioni tatu katika maeneo ya katikati na Kusini mwa nchi hiyo.

Mashambulizi hayo yanayowahusisha maelfu ya wanajeshi wa AU, yaliyoanzishwa juma lililopita na sasa yamesambaa hadi katika maeneo ya jangwa na milima.

Umoja wa Mataifa umeongezeka kusema kuwa umo katika hali ngumu zaidi Nchini Somalia.

Kwa sasa inaisaidia Umoja wa Afrika kwa hali na mali pamoja na vifaa vinavyohitajika kupambana na wapiganaji wa Kiislamu, na pia misaada ya kibinadam.

Inaunga mkono Jeshi moja kwa moja katika kutekeleza mashambulio makali dhidi ya makundi ya wapiganaji wa kiislamu yaliyo katika vuguvugu la Al-Shaabab.

Lakini kitengo kingine cha Umoja wa Mataifa kinachoshughulikia mashirika ya utoaji misaada ya kibinadamu, sasa yanatahadharisha kuhusiana na makali yanayotekelezwa na wanajeshi hao dhidi ya wananchi.

Shambulio mjini Mogadishu

Mashirika hayo pia yanasema wapiganaji wa Kiislamu kwa upande wao wanawahamasisha wananchi dhidi ya operesheni hiyo ya kijeshi inayojumuisha wanajeshi kutoka mataifa wanachama pamoja na wanajeshi wa serikali ya Somalia.

Siku za kwanza kwanza za operesheni hiyo kali, hasa katika maeneo ya vijijini, haikuwa rahisi kwa wafanyi kazi wa Umoja wa Mataifa kujua kilichokuwa kikiendelea.

Lakini tayari maelfu ya watu wanaingia katika mji wa Baidoa ulioko katikati mwa Somalia unadhibitiwa kwa sasa na Wanajeshi wa umoja wa mataifa kukimbia mapigano au kujaribu kupanga mashambulizi.

No comments:

Post a Comment