Bi Clinton alitarajiwa kuhojiwa mwaka jana lakini akaugua
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, anatarajiwa kufika mbele ya bunge la Congress kujieleza kuhusu mashambulizi mabaya yaliyofanywa dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Benghazi, Libya, mwaka jana.
Bi Clinton atakabiliwa na maswali kutoka kwa kamati za bunge la Senate na la waakilishi kuhusu maswala ya kigeni, juu ya usalama mbovu uliosababisha mashambulizi hayo.
Balozi wa Marekani nchini Libya Christopher Stevens pamoja na maafisa wengine watatu wa ubalozi huo, waliuawa kwenye mashambulizi hayo.
Balozi huyo alifariki kutokana na moshi wakati aliponaswa ndani ya jengo lililokuwa linateketea.
Hii ni baada ya wapiganaji wa kiisilamu kuvamia ubalozi.
Mashambulizi hayo yalisababisha mvutano wa kisiasa swali likuwa nani aliyekuwa na taarifa kuhusu shambulizi hilo.
Baada ya kushambulia ubalozi wavamizi walichoma bendera ya Marekani kuonyesha kero lao
No comments:
Post a Comment