AU yazidisha vita dhidi ya Al Shabaab

Al Shabaab

Mamia ya wanajeshi wa Muungano wa Afrika wanaukaribia mji muhimu wa Koryoley, ulio umbali wa kilomita 90 Kusini Magharibi mwa mji mkuu Mogadishu.

Mji wa Koryoley, umekuwa chini ya udhibiti wa kundi la wanamgambo la Al Shabaab kwa miaka mitano iliyopita.

Mwandishi wa BBC aliye katika eneo hilo anasema kuwa wanajeshi hao wako umbali wa kilomita 10 kutoka mjini humo.

Anasema kuwa ikiwa wanajeshi hao wataukomba mji huo, utakuwa ukombozi wao mkubwa wa mji tangu kuanza harakati hizo dhidi ya Al Shabaab mwezi Machi mwaka jana wakiungwa mkono na Umoja wa Mataifa.

Wanajeshi hao wamefanikiwa kukomboa miji mingine muhimu na hata kuwatimua wapiganaji hao kutoka katika ngome zao kubwa.

Wengi wa wanajeshi wa AU ni kutoka Uganda, wakisaidiwa na wanajeshi wa Kenya, Burundi na sasa Ethiopia pamoja na wanajeshi wa Somalia.

No comments:

Post a Comment