Mauaji Darfur vita vikiendelea

Askari wa Sudan
Askari wa kikosi cha Sudan katika jimbo la Darfur

Shirika la haki za binadamu Human Rights Watch linasema makumi kadhaa ya watu waliuawa katika ghasia zinazoendelea katika jimbo la Darfur nchini Sudan.

Shirika hilo linasema viongozi wa kijamii katika vijiji viwili wametoa orodha ya majina ya raia takriban arobaini waliouawa katika wiki chache zilizopita kwenye makabiliano baina ya vikosi vinavyounga mkono serikali na vile vya waasi.

Human Rights Watch linasema wanavijiji wengine makumi kadhaa walishambuliwa, baadhi yao wakipigwa na makombora ya ndege za kijeshi. Shirika la msalaba mwekundu limesema mmoja wa wafanyakazi wake aliuawa jana.

Umoja wa Mataifa unasema mwaka huu pekee zaidi ya watu laki mbili wameyakimbia makazi yao jimboni Darfur.

No comments:

Post a Comment