'Oscar Pistorius alipenda sana Bunduki'


Pistorius akiwa mahakamani

Katika ushahidi unaoendelea kutolewa dhidi ya mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius, rafiki ya mwanariadha huyo, ameambia mahakama kuwa Pistorius alipenda sana bunduki

Darren Fresco, alisema kuwa alikuwa naye mara mbili alipokuwa na bunduki aliyoiofyatua katika sehemu ya umma.

Bwana Pistorius wakati mmoja alifyatua bunduki yake akiwa ndani ya mkahawa , ingawa yeye ndiye aliyelaumiwa kwa hilo,alisema bwana Fresco said.

Mwanariadha huyo amekanusha madai ya kumuua mpenzi wake kwa maksudi, akisema kuwa alidhania kuwa ni mwizi aliyevamia nyumba yake.

Bwana Fresco alisema kuwa katika tukio lengine, alikuwa anaendeshagari lake wakati ambapo Pistorius alipofyatua tena bunduki yake baada ya polisi kumzuia kuendesha gari lake kwa kasi.

Alisema kuwa Pistorius alikasirika baada ya polisi kuchukua dunduki yake iliyokuwa kwenye kiti cha nyuma ya gari lake na kumwambia: '' hauruhusi kugusa bunduki ya mtu mwingine, ikiwa chochote kitatokea atakuwa wa kulaumiwa.''

Mwandishi wa BBC nchini humo, Pumza Fihlani anasema kuwa Pistotius katika kikao cha Jumanne alikuwa mtulivu ikilinganishwa na Jumatatu.

Aliketi akiwa kimya na kuandika baadhi ya maneno yaliyokuwa yanasemwa.

Ushahidi wa Fresco, ulitoa taswira ya mchezaji huyo alivyopenda maisha ya kifahari akiwa na rafiki zake. Alipenda magari, wanawake warembo , bunduki na kwamba aliwashukia sana polisi.

Aliyekuwa mpenzi wa Oscar pia alitoa ushahidi sawana huo mahakamani, wiki ya kwanza ya kuzikilizwa kwa kesi hiyo.

No comments:

Post a Comment