Rais wa Marekani Donald Trump amesema kwamba kuwapatia walimu silaha kunaweza kuzuia mashambulio ya risasi katika shule kama lile lililowaua watu 17 wiki iliopita mjini Florida.

Baada ya mauaji ya watu 17 katika shule moja Florida 14 Februari, na mwaka jana kufuatia kuuawa kwa watu 59 jijini Las Vegas, Nevada watetezi wa udhibiti wa silaha nchini Marekani wameanza kuzidisha kampeni yao.
Ni kisa ambacho kinaonekana kuwa cha kawaida, kwani hilo hutokea kila baada ya mauaji kutekelezwa kwa kutumia bunduki.
Katika ngazi ya taifa, licha ya utafiti kuonyesha kwamba watu wengi wangependa kukazwa kwa sheria za kuwaruhusu watu kumiliki silaha, bado hakuna hatua iliyochukuliwa kutunga sheria kwa miongo kadha.
Miongoni mwa mambo ambayo hupendekezwa ni uchunguzi zaidi wa historia na maisha ya mtu kabla yake kuuziwa silaha.
Aidha, kupigwa marufuku kwa bunduki zenye uwezo mkubwa sawa na zile zinazotumiwa na jeshi.
Baada ya idadi kubwa ya watu kuuawa wakati huu, huenda shinikizo za kufanyika kwa mabadiliko zitazidi.
Hapa chini ni sababu nne ambazo zimezuia kufanyiwa mageuzi kwa sheria kuhusu silaha Marekani.

No comments:

Post a Comment