Profesa Mbele Na Wanaongoja Ajira Milioni Moja Walizoahidiwa Na CCM!


Huu ni mchango wa Profesa Joseph Mbelea, anasema...

"Ingekuwa bora kama hao wangekuwa maktabani kuliko kupoteza muda wao kwenye kijiwe hiki cha abracadabra. Wangetumia muda wao maktabani wakisoma vitabu na majarida wangekuwa wanajiongezea ujuzi, maarifa, na elimu kwa ujumla. Sio tu ni jambo la manufaa kwa mtu kuelimika, bali pia maandalizi ya ajira.

Kwa mfano, wangetumia muda wao maktaba na kusoma vitabu vya ki-Ingereza, hatimaye wangekuwa na uwezo wa kushindana na wa-Kenya kwenye ajira katika sekta kama utalii. Sekta hii inavyokwenda ni kwamba hata mfagiaji anatakiwa kujua ki-Ingereza kidodo, ili mtalii akiomba shuka au sabuni, aweze kujibiwa.

Lakini hao wa-Tanzania ukiwauliza habari hii ya ajira, wengine watakuambia wanangoja ajira milioni walizoahidiwa na CCM mwaka 2012. Wengine watakuambia serikali ya JK imeshindwa kuwapa ajira. Na kuna siku mhubiri atakuja eneo hili hili na kuwahubiria kuwa wamekosa ajira sababu ya mfumo Kristo. Tena hii abracadabra ya mfumo Kristo imepamba moto kweli.

Inabidi sisi wenye ufahamu wa dunia, kutokana na kutembea sehemu mbali mbali za dunia, na pia kutokana na kusoma, tufanye juhudi ya kuwamegea hao wenzetu elimu ambayo Mungu katupa fursa ya kuipata. Kwa upande wangu, naandika sana kwenye blogu, makala, na hata vitabuni, kuwa dunia ya leo haina mchezo, na njia pekee ya kuimudu na kujipatia mafanikio ni kwa kujielimisha. Ndugu zetu waache kushabikia hizo abracadabra, na badala yake wasome vitabu au kwenda shuleni, kwani. Nyerere alisema elimu haina mwisho, na ndilo fundisho la kuzingatiwa."

No comments:

Post a Comment