TPBC Yaipa Shavu BFT - Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari



                 TAARIFA KW A VYOMBO VYA HABARI


Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Nchini (TPBC) inaipa shavu BFT kwa juhudi zake za kuendeleza ngumi za ridhaa hapa nchini kama kichocheo cha maendeleo ya ngumi pamoja na michezo yote kwa ujumla.


TPBC inatambua ugumu wa maisha pamoja na matatizo yaliyopo kupata wadhamini kwenye mchezo wa ngumi. Juhudi za BFT za kuandaa mashindano ya nguni za ridhaa mwaka huu ni zenye mweleko mzuri kimaendeleo. Sisi kama Kamisheni iliyopewa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jukumu la kusimamia ngumi za kulipwa nchini tunatambua kuwa ngumi za ridhaa ni chemchem ya nguni za kulipwa hivyo tupo tayari kushirikiana na BFT kufanikisha mashindandano haya.


TPBC imefarijika na juhudi za BFT katika ushiriki wake kwenye mashindano ya Olympic yaliyomalizika hivi karibuni nchini Uingereza. Juhudi zenu zimeitangaza vyema Tanzania na kuwapatia mabondia wa Kitanzania nafasi ya kujulikana ulimwenguni.


Kushiriki katika mashindano ya Olympic sio tu kupata medali bali pia ushiriki wenyewe unaitangaza nchi kama moja ya mataifa yaliyo mstari wa mbele katika maendeleo ya michezo ulimwenguni.

Tunatoa pia pongezi kwa Kamati ya Olympic ya taifa (TOC) na baraza la Michezo la taifa (BMT) kwa juhudi zake za kuhakikisha kuwa kila mara Tanzania inakuwa moja ya nchi zinazoshiriki katika mashindano ya Olympic.

Sisi tunashiriki katika mapambano mbalimbali ya ngumi za kulipwa ulimwenguni tunajua faida za kujitangaza huku kwani tunajulikana kwa juhudi hizi. Tutatoa wito kwa wadau wa ngumi na michezo yote Tanzania ikiwa ni pamoja na watu binafsi, makampuni mbalimbali pamoja na na taasisi zisizo za kiserikali kuwasidiaBFT katika juhudi za kuendesha mashindano haya yatakayoanza hivi karibuni.

Imetolewa na:

Onesmo Ngowi

Rais wa Kamisheni ay Nguni za Kulipwa Nchini (TPBC)

Mkurugenzi wa Ngumi wa Jukuiyaya madolka (CBC)

Rais wa Shirikisho la Ngumi la Kimataifa Afrika, Ghuba ya Uarabu na Uajemi

No comments:

Post a Comment