Generali Sultani Makenga , kiongozi wa M23
Kiongozi wa kisiasa wa kundi la waasi la M23 yuko mjini Kampala kwa mkutano na wakuu wa majeshi kanda ya maziwa makuu.
Msemaji wa kundi hilo, aliambia BBC kuwa mkutano huo utaangazia ikiwa waasi hao wataondoka katika mji wa Goma.
Waasi wa M23 ni wanajeshi walioasi jeshi la Congo mwezi Aprili , na wanasema kuwa serikali imekataa kutimiza baadhi ya makubaliano waliyoafikia mwezi Machi mwaka 2009.
Uganda imekuwa ikipatanisha waasi hao na serikali ya DRC tangu mwezi Agosti.
Mwandishi wa BBC mjini Kampala Cathrene Byaruhanga anasema kuwa waasi hao wana hadi mwishoni mwa leo kuondoka Goma.
Hali ya usalama mjini Goma ni tete huku maelfu wakitoroka mwakao
No comments:
Post a Comment