Kijana atuhumiwa kunajisi kitoweo


WAKAZI wa Kata ya Bashnet,  Wilaya ya Babati, mkoani Manyara wamelaani kitendo cha mkazi mmoja wa kata hiyo kuwaingilia mbuzi, na wameitaka Serikali kumchukulia hatua kali za kisheria.

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wakiwamo wafugaji wamesikitishwa na kitendo hicho cha kijana huyo kuwaingilia mbuzi wao.

Mmoja kati ya wakazi hao, Abraham Mlundi alisema juzi ni mara ya tano kwa kijana huyo kumuingilia mbuzi wa mkazi mmoja wa eneo hilo, kitendo ambacho ni kinyume na mila na desturi.

Mlundi alisema imekuwa ni tabia ya muda mrefu kwa kijana huyo kuwaingilia mbuzi hasa nyakati za jioni na kwamba, akishafanya kitendo hicho anahama eneo hilo kwenda kujificha vijiji vya mbali.

“Hadi hivi sasa hatujatambua lengo lake anapowaingilia mbuzi hao, ingawa  wengine wanadai ni vitendo vya ushirikina na wengine wanahisi anafanya hivyo kutokana na kukosa mke hajaoa,” alisema Mlundi.

Alisema hii ni mara ya tano kwa kijana huo kuwaingilia mbuzi na kwamba, wamekuwa wakifanya jitihada kuhakikisha anakamatwa ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria.

“Siku ya mwisho kufanya tukio hilo, kijana huyo alitaka kuuawa ila alikimbia kwani alikutwa amembana mbuzi kwenye zizi,” alisema Mlundi.
Hata hivyo, Mtendaji wa Kijiji cha Bashnet, Omary Mwanditi alithibitisha tukio hilo na kwamba, kijana huyo amekuwa na tabia ya kuwaingilia mbuzi.

“Tunaendelea kumtafuta kijana huyo kwani vitendo anavyovifanya siyo vya kiungwana, pia ni kinyume cha ustaarabu kwenye mila na desturi kwa Watanzania,” alisema.

No comments:

Post a Comment