Zeidan akanusha kufutwa kazi


Aliyekuwa Waziri mkuu wa Libya Akihutubia Wanahabari

Aliyekuwa waziri mkuu wa Libya, Ali Zeidan, amepuuzilia mbali kura ya kutokuwa na imani naye iliyotangazwa na Bunge la taifa hilo mapema juma hili iliyopeleekea kufutwa kwake.

Ameiambia shirika la habari la Channel France 24 kuwa kura hiyo ya kutokuwa na imani naye illikuwa imejengwa kwa misingi ya uwongo huku pia akikanusha madai ya ufisadi dhidi ya serikali yake.

Ali Zeidan aliondolewa Ofisini mnamo siku ya Jumanne baada ya meli ya mafuta kutoka bandari inayodhibitiwa na waasi kufaulu kuvunja nanga ya wanajeshi wa wanamaji wa Libya kuingia bahari kuu na kutoroka.

Bwana Zeidan alifaullu kuondoka nchi hiyo licha ya kupingwa marufuku ya kutosafiri nje ya taifa.

No comments:

Post a Comment