NJAA CHAMWINO

Na John Banda, Chamwino

VIJIJI  vyote 77  vya Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma vimekumbwa na baa la njaa   kutokana na ukame mkali uliodumu kwa miezi miwili mfurulizo.

Ukame huo ulio ulioanza mwanzoni mwa mwezi wa kwanza mpaka mwishoni mwa  mwezi wa pili umefanya hali ya chakula kuwa mbaya Wilayani humo hali inayozidi kutishia maisha ya watu.

Akitoa taarifa ya hali ya chakula Afsa kilimo wa Wilaya ya Chamwino kwenye Baraza la Madiwani lililofanyika jana  Gofrey  Mnyamale  alisema kutonyesha Mvua kwa kipindi hicho kumesababisha  hata zao la Mtama ambalo huwa linastahimili ukame kukauka.

Alisema  katika msimu wa kilimo wa Mwaka 2012/13 wilaya ilijiwekea malengo ya kulima Hekta 118, 071 za mazao ya chakula na kutarajia kuvuna tani 105, 040 kama Mtama,  Mahindi na uwele  lakini malengo hayo yamepotea.

Aliongeza kuwa Mvua nyingi zililizonyesha katika mtiririko usioridhisha hasa Mwezi Desemba na kufuatia na ukame mkali katika miezi hiyo miwili kuliwapoteza watu waliozoea kupanda mapema kutokana na hali ya hewa ya mkoa wenyewe.

Mnyamale alitanabaisha kuwa waliamua kuwaagiza wananchi kutunza chakula kidogo walichonacho, wenye mifugo kuuza ili kununua chakula, kuzuia wafanyabiashara wasitoe nje chakula na kufanya tasmini ya kina ili taarifa ipelekwe kwa Waziri mkuu mapema iwezekanavyo.

‘’Tunataka baada ya kukamilisha Tathimini hii Taarifa itapelekwa haraka kwa Waziri Mkuu ili hatua za haraka za kunusuru watu dhidi ya janga la njaa zichukuliwe  mapema mapema iwezekanavyo ambapo tunatarajia kabla  Mei 10 mwaka huu kuwa imekamilika’’, alisema

Kwa upande wake Mjumbe wa Nec ya CCM Samwel Malecela aliitaka Selekari kuchukua hatua za Halaka ili kunusuru hali ya njaa katika Wilaya nyingi kutokana na upungufu wa chakula kuwa kila sehemu.

‘’ Janga hili ni kubwa  na Mala nyingi Selekari imekuwa ikisema inafanya upembuzi yakinifu na inatumia muda mwingi kupembua katika hili nawaambia wafanye haraka kwani hali ni mbaya mno bora kitu kingine kuliko njaa’’, alisema

Malecela Aliongeza kuwa yeye kwa nafasi yake anatembea kila wilaya na amebakiza chache ili amalize na sehemu kubwa inatatizo la kukosa chakula hivyo serekali ihakikishe inatoa kipaumbele kuanzia na wilaya zilizoathirika sana kama hiyo ya Chamwino anakotokea.

MWISHO  

No comments:

Post a Comment