WATUHUMIWA UCHOMAJI WA MAKANISA MBAGALA, WAPANDISHWA TENA KIZIMBANI

Na Musa Mateja

WATUHUMIWA 47 wanaokabiliwa na kesi ya kuharibu na kuchoma moto makanisa wakati wa vurugu za baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu Mbagala, leo wamepandishwa tena kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashitaka mbele ya Wakili Mwandamizi wa Serikali, Bw. Tumaini Kweka, yanayowahusisha na kesi ya  kula njama kwa nia ya kutenda makosa kinyume na sheria.

Askari magereza akiwafungulia pingu baadhi ya watuhumiwa  tayari kwa kusomewa mashitaka yao.

Makosa mengine yanayowakabiri watuhumiwa hao ni pamoja na kosa la  kuvunja jengo kwa nia ya kufanya uharifu, uharibifu wa mali za kanisa, wizi wa vifaa vya kanisa, kuchoma kwa makusudi jengo linalotumika kwa shughuli za ibada na kuhatarisha maisha ya mlinzi.
Mashitaka yote hayo leo yamewakilishwa mbele ya Hakimu, Bw. Binge Mashabala, ambaye alisikiliza pande zote mbili na kuahirisha kesi hiyo hadi Novemba 7 mwaka huu kwa ajili ya kukamilisha upelelezi wa kesi hizo.

Watuhumiwa wakipelekwa kizimbani.
…wakipanda ngazi tayari kwa kuelekea chumba cha mahakama.
Baadhi ya watuhumiwa 47 waliyofikishwa kizimbani wakiwa ndani ya mahakama.
Wakirejeshwa mahabusu.
Baadhi ya ndugu na jamaa wa watuhumiwa hao wakiwa nje ya mahakama.
(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL)

No comments:

Post a Comment