Rufaa ya Jerry Muro Februari mwakani

 

Rufaa ya kupinga kuachiwa huru kwa aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Jerry Muro na wenzake wawili waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya rushwa ya Sh. milioni 10 imepigwa kalenda kusikilizwa hadi Februali 18 mwakani.


Jaji Dk. Fauz Twaibu wa Mahakama ya Kuu ya Kanda ya Dar es Salaam, alipiga kalenda rufaa  hiyo baada ya upande wa Jamhuri kuomba kuibadilisha.

Hata hivyo, ombi hilo halikuweza kupingwa na upande wowote wa mawakili kwani pande zote ziliridhika na ombi hilo na zote zimekubali tarehe hiyo iliyopangwa kwa ajili ya kusikilizwa tena rufaa hiyo.

Muro na wenzake waliachiwa huru na Hakimu Frank Moshi wa Mahakama ya Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Novemba 13 mwaka jana baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao.

Mbali na Muro washtakiwa wengine walioachiwa huru ni Edmund Kapama maarufu kwa jina la Dokta na Deogratius Mgasa.

Kesi hiyo iliyoanza kusikilizwa Februali mwaka 2010 upande wa mastaka uliokuwa ukiongozwa na aliyekuwa wakili wa Serikali Boniface Stanslaus ambaye ni marehemu kwa sasa.

Kutokana na kifo cha wakili huyo ndipo wakili wa kujitegemea Richard Rwezengo alimwakilisha Muro na wakili Majura Magafu akamwakilisha mshtakiwa wa pili na wa tatu.

Awali ilidaiwa kuwa Januari 28 mwaka 2010 jijini Dar es Salaam washtakiwa wote na wengine ambao hawakuwepo Mahakamani walikula njama na kutenda kosa la kuomba rushwa.




No comments:

Post a Comment