Msekwa, Kaduma wakoleza moto CCM

Mzee Msekwa 


IKIWA zimebaki siku nane kabla ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuadhimisha miaka 36 ya kuzaliwa kwake, makada wakongwe wa chama hicho, Pius Msekwa na Ibrahim Kaduma wamesema ili kudumisha umoja ni lazima wanachama wakorofi ndani ya chama hicho wachukuliwe hatua.

Kauli za wanachama hao wakongwe zimekuja wakati ambao watu wa kada mbalimbali wamekuwa wakikilalamikia chama hicho kwa kushindwa kuwachukulia hatua baadhi ya makada wake, ambao wanatajwa katika kashfa mbalimbali, huku wakidaiwa kukigawa chama hicho.

Sherehe hizo za CCM zinazofanyika kitaifa mkoani Kigoma zitafikia kilele chake Februari 3, mwaka huu, huku kikipanga kuzitumia sherehe hizo kufanya tathmini ya uchaguzi wake mkuu uliomalizika mwishoni mwa mwaka jana.

Kwa nyakati tofauti Msekwa ambaye amewahi kuwa Kaimu Mwenyekiti wa CCM, Bara na Kaduma aliyewahi kuwa Waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere, walisema uadilifu ndiyo kitu cha kwanza kuzingatiwa ndani ya chama na taifa kwa jumla.

Msekwa alisema kuwa watu wakorofi ndani ya CCM hawawezi kukosekana kwa kuwa chama ni jumuiko la watu wengi na kwamba kila mmoja ana tabia zake.

“Hiyo ndiyo hali halisi, hata ndani ya nchi yetu kuna watu wabaya na wazuri na ndiyo maana zikawapo sheria kwa ajili ya kuwashughulikia wanaozivunja,” alisema Msekwa na kuongeza:

“Hata CCM ina kanuni na taratibu zake za kuwashughulikia watu wanaokwenda kinyume na taratibu za chama.”

Alisema kuwa chama hicho kimeweza kumitimza miaka 36 kwa ajili tu ya kufuata misingi iliyoachwa na Mwalimu Julius Nyerere.

“Hata waliopo sasa, nao wanafuata misingi hiyo na ndiyo maana unaiona CCM ipo hapa, ila kikubwa ambacho chama imekifanya ni kujali shida za watu,” alisema Msekwa.

Alifafanua: “Watanzania wanaona ni bora waongozwe na CCM kwa sababu hawajawahi kutawaliwa na chama kingine, ambacho labda wangekilinganisha utendaji wake na huu wa CCM, hivyo wanaona bora kubaki na CCM.

Kwa upande wake Kaduma ambaye katikati ya wiki hii alitoa maoni yake ya Katiba Mpya, alisisitiza kuwa alichokizungumza katika maoni yake, ndiyo kasoro za CCM.

Alisema upungufu ulio ndani ya CCM ni maaadili ya viongozi wa kada mbalimbali.

Alisema kuwa ili kumaliza suala la uadilifu, taifa linatakiwa liwe na tume huru ya maadili, ambayo itakuwa juu ya viongozi wote ikiwa ni pamoja na rais.

Alipendekeza tume hiyo iundwe na Watanzania kubainisha misingi na maadili ya taifa, pamoja na wajumbe wake kupatikana kwa kuwashirikisha wananchi, ambao ndiyo watapendekeza majina ya watu watakaokuwa viongozi wa tume hiyo.

Alisema kazi ya tume hiyo itakuwa kuchunguza mienendo wa viongozi wakuu wa mihimili muhimu ya uongozi wa taifa kama Rais, Makamu wake, Spika wa Bunge, Majaji, Mawaziri, wabunge na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama.

“Kazi nyingine ya tume hii itakuwa ni kutoa mapendekezo kwa Bunge kuhusu uadilifu wa Rais katika kutekeleza majukumu yake,

No comments:

Post a Comment