Mwanafunzi Chuo Kikuu cha Saint John auawa kinyama.

Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma David Misime

Polisi mkoani Dodoma imeshutumiwa kwa kushindwa kuimarisha ulinzi katika baadhi ya maeneo mkoani humo hatua inayodaiwa kuchangia kuaawa kinyama kwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Saint John Lidya Leo Mzima na watu wasiojulikana.

Marehemu Lidya mwenye umri wa miaka 57 anadaiwa kuuawa siku ya jumapili majira ya saa nne za usiku pembezoni mwa maeneo ya chuo hicho chenye wanafunzi 5500 akiwa anarejea nyumbani baada ya masomo ya jioni.

Ni simanzi, vilio, huzuni na majonzi katika vyunga vya chuo hiki kufuatia tukio hili la kusikitisha ambalo linadaiwa kuyaweka katika mashaka na wasiwasi mkubwa maisha ya wanafunzi hawa.

Licha ya kulitupia lawama jeshi la polisi baadhi ya mashuhuda walidai kuwa baada ya kufikwa na mkasa huo uliositisha safari ya maisha yake mwili wa marehemu Lidya uliharibiwa vibaya na mnyama asiyejulikana kwa kunyofolewa macho, masikio, pua, mguu na viuno vingine.

Kutokana na shutuma za uzembe dhidi ya jeshi hilo Kamanda wa mkoa wa Dodo,a Kamishna msaidizi wa Polisi David Misime aliwataka wakazi wa mkoa huo kuimarisha ulinzi shirikishi kwa lengo la kuwabaini wahalifu.

Wakati huo huo Kamanda Misime alisema msako mkali umeanza wa kuwatia nguvuni waliohusika na ukatili huo ili waweze kufikishwa kwenye mikono ya sheria kwa ajili ya hukumu.

Wanafunzi wa Chuo Cha Saint John walikuwa wakiripotiwa kukumbwa na vitendo vya kubakwa, kulawitiwa, kuporwa mali zao sanjari na kupewa vipigo na watu wasiojulikana pasipo sababu za msingi.

Mwili wa marehemu Lidya aliyekuwa muuguzi kitaaluma umehifadhiwa kwenye chumba cha maiti katika hospitali kuu ya Mkoa wa Dodoma ukisubiri uchunguzi wa madaktari.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, amina.

No comments:

Post a Comment