Rais Mahama alipokuwa anaapishwa mbele ya maelfu ya wananchi wa Ghana
Chama rasmi cha upinzani nchini Ghana, kimesusia sherehe za kuapishwa kwa rais mpya John Mahama kufuatia uchaguzi wa mwezi jana uliokumbwa na utata.
Chama cha New Patriotic Party (NPP) kilisema kuwa bwana Mahama hakushinda uchaguzi huo kihalali.
Kabla ya kuapishwa kwake, bwana Mahama alitoa wito wa amani na umoja nchini Ghana, nchi ambayo inaonekana kama mfano mzuri wa demokrasia barani Afrika.
Bwana Mahama alikuwa makamu wa rais wa Ghana hadi pale kifo cha ghafla cha aliyekuwa rais,John Atta Mills kutokea mwezi Julai.
Tangu hapo alihudumu kama rais wa mpito.
Rais John Mahama
No comments:
Post a Comment