Tukio hilo lilitokea Januari juzi saa 10:00 jioni baada ya mama huyo
aliyefahamika kwa jina la Tausi Saidi (29), mkazi wa kijiji cha Mbete
Kata ya Mlimani Manispaa ya Morogoro kufikishwa hospitalini baada ya
kushikwa na uchungu.
Baada ya kufika hospitalini akiwa na muuguzi wa zahanati ya Mbete pamoja
na ndugu wa mgonjwa huyo, wauguzi wa hospitali hiyo walianza kubishana
kabla ya kumhudumia mgonjwa.
Kwa mujibu wa mume wa mwanamke huyo, Kudra Khalfani, mkewe alianza
kupata uchungu akiwa nyumbani, na kumpeleka katika zahanati ya Mbete,
na baada ya kufika huko alilazimika kupelekwa katika Hosptali ya Rufaa
ya Mkoa wa Morogoro baada ya kuonekana kuwa anahitaji matibabu makubwa.
Alisema baada ya kufika wodi ya wazazi, Muuguzi waliyeambatana naye
aliingia wodini na kumtaka nesi wa wodi hiyo kwenda kumuangalia mgonjwa,
lakini hakupewa msaada.
Alisema muuguzi huyo aliwataka kumpeleka mama huyo wodi namba saba ‘B’ bila kutoa msaada wowote.
“Kabla ya kufika wodini akasema Tumshushe, akawa amejifungulia koridoni na mtoto akafariki,” akusema.
Mashuhuda waliojitambulisha kwa majina ya Mwajuma Ally na Aida Hamis
walieleza kuwa kitendo hicho ni cha udhalilishaji, kwamba kimetokana na
uzembe wa wauguzi wa wodi ya wazazi.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro, Dk. Ritha
Lyamuya, alithibitisha kutokea kwa tukio na kwamba hali hiyo ilitokana
muuguzi kumhudumia mgonjwa mingine.
Dk Lyamuya alisema mimba ya mwanamke huyo ilikuwa haijafikisha umri
wakujifungua, na kwamba alishawahi kupoteza mimba nne, kutokana na kuwa
na viashiria vya hatari vya uzazi.
Aliongeza kuwa pamoja na kupewa tahadhari hiyo, kadi lake la kliniki
linaonyesha kuwa amehudhuria mara moja tu, kitu ambacho ni hatari sana
kwa mama mjamzito.
No comments:
Post a Comment