viziwi wa mji mdogo wa kibaingwa washindwa kuchangia marekebisho ya katiba


Na John Banda,Dodoma

VIZIWI wanaoishi vijijini wa mji mdogo wa Kibaingwa Wilaya ya Kongwa wale wanaoishi vijijini ,wamesema watashindwa kuchangia mawazo yao ya marekebisho ya katiba mpya inayoendelea kwa hivi sasa kwa kuwa hawajawahi kukiona kitabu cha katiba na pia hawajawahi kukisoma bali wanasikia kupitia kwenye vyombo vya habari ikitanganzwa.

Kauli hiyo imetolewa kwa pamoja na walemavu Tito Mnyamale (33) na Paul Mnage (32) kwa niaba ya wezao wakati wanapokuwa wakichangia juu ya marekebisho yanayotakiwa yafanyike kuhusu haki zinazotakiwa kutendewa watu wenye ulemavu wa kutosikia.

Wakichangia hoja zao kwenye warsha ya mafunzo ya mkataba wa umoja wa mataifa juu ya haki ya walemavu na sheria na sera ya Taifa ya viziwi mwaka 2010 kwa viziwi wa mji wa mamlaka ya Kibaingwa Wilaya ya Kongwa.

Walemavu hao walisema wanashindwa kuchangia katiba hiyo kutokana na kutoielewa na itawasaidiaje wao wakati toka wamezaliwa hawajawahi kuiona na badala yake wanaisikia kwenye vyombo mbalimbali vya habari.

"Hapa lazima tuiambie ukweli serikali yetu kuwa sisi walemavu tunaoishi vijijini hatujakiona hiki kitabu ambacho leo hii tunaambiwa ndiyo katiba inayotakiwa kufanyiwa marekebisho mbalimbali,hii pia inatokana na kwa upande wetu kukosa kushirikishwa kwenye vikao vinavyozungumzia marekebisho hayo ya katiba"alisema Mnange.

Aidha walemavu hao walisema kutokana na viongozi wa serikali ngazi ya kata,vijiji hadi vitongoji kitendo chao cha kutowashirikisha kwenye vikao vya kujadili katiba hiyo pia kumechangia kwa upande wao kutoipata elimu ya kutosha ambayo ingetuwezesha kufahamu namna ya kuijadiri marekebisho hayo.

"Serikali yetu kwa kupitia viongozi wao wamekuwa wakiwaona wa maana sana katika kipindi cha upigaji kura tu,na wako radhi kuja kutubeba kwa usafiri wao ili waweze kupigiwa kura za kuwachangua lakini kwenye suala la kujadili mapendekezo ya marekebisho ya katiba inaonekana sisi haituhusu kabisa"alisema Tito.

Naye Meneja wa mradi wa Leonard Cheshine Disibility Dodoma Baraka Mgohamwende aliwataka walemavu hao kutoa maoni yao juu ya haki wanazotaka zifanyiwe kwa kupitia katiba hiyo mpya ambayo hivi sasa inajadiliwa na kupendekezwa na watanzania hapa nchini.

Mgohamwendo ambaye alikuwa akielimisha umuhimu wa kuitambua katiba kwenye warsha hiyo, alisema kuwa pamoja na kutoielewa maana ya katiba hiyo ambayo hivi sasa wameiona na kukabidhiwa,wanatakiwa kuisoma ili kupitisha maoni yao ambayo yanayohitajika kuwepo na haki zao zinazotakiwa waweze kufanikisha.

Naye Katibu wa Chavita wilaya ya Kongwa Anitha Masawe alisema katika eneo hilo walemavu wa Uziwi walio wengi hawaitambui katiba hiyo inatokana viongozi walio kwenye ngazi za vitongoji,vijiji na kata kwa upande wa serikali na siasa hawaoni umuhimu wa kuwashirikisha shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Anitha alisema ndiyo maana leo hii walemavu wa wilaya hiyo hususan wale wanaoishi vijijini,hawajui katiba na faida ambazo watakazoziona kama na wao watachangia katika kutoa mapendekezo ya marekebisho ya katiba hiyo.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment