Wadau wa Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi Mkoani hapa kutokana na juhudi za kupambana na uhalifu hususani kudhibiti mtandao wa majambazi sugu.

Nwaka Mwakisu  Mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Taifa kupitia Umoja wa Vijana Mkoa wa Mbeya katika mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika katika ofisi za Umoja wa Vijana CCM Mkoa wa Mbeya. hivi karibuni
Baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa Mbeya wakimsikiliza Mwakisu


 Wadau wa Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi Mkoani hapa kutokana na juhudi za kupambana na uhalifu hususani kudhibiti mtandao wa majambazi sugu.

Wadau hao walisema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani ndiye anayepaswa kupongezwa kutokana na juhudi alizozionesha za kufichua mtandao wa majambazi ikiwa ni pamoja na kuwakamata na kuwauwa wengine.

Akizungumza kwa niaba ya wadau hao Nwaka Mwakisu ambaye pia ni Mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Taifa kupitia Umoja wa Vijana Mkoa wa Mbeya katika mkutano wa waandishi wa Habari uliofanyika katika ofisi za Umoja wa Vijana CCM Mkoa wa Mbeya.

Mwakisu alisema Historia ya Mkoa wa Mbeya ilikuwa Mbaya ambapo ilikuwa ikisifika kwa matukio mabaya kama ya upigaji nondo, ubakaji, ushirikina na ujambazi ambavyo vimeanza kutoweka kutokana na juhudi zilizooneshwa na Jeshi hilo kwa kushirikiana na wananchi.

" Kutokana na hali ilivyo sioni sababu ya kutompongeza RPC Diwani kutokana na kupambana na uhalifu Mkoani Mbeya " alisema Mwakisu. 

Alisema kutokana na hali halisi ya Amani ya Mkoa wa Mbeya Wawekezaji watajitokeza kwa wingi kufanya uwekezaji tofauti na ilivyokuwa ambapo wawekezaji walikuwa wakikimbia Mkoa wa Mbeya kutokana na Vurugu zilizokuwepo. 

Aliongoza kuwa kutokana na juhudi za Jeshi la Polisi za kupambana na uhalifu alisema ni vema kila Mwananchi akatambua mchango huo na kusaidia katika kuhakikisha kuwa amani inaongezeka Mkoani Mbeya.

Mwakisu alisema pamoja na kutokomeza uhalifu Mkoani hapa pia suala la kuwatumikisha Vijana katika mambo yasiyokuwa na msingi wowote hususani kwenye vurugu ndiyo sababu ya kuongezeka kwa uhalifu.

Alisema taifa lolote duniani linalindwa na kuendelezwa na vijana hivyo alitoa wito kwa wanasiasa kuacha kuwatumia vijana vibaya ambapo aliongeza kuwa Vijana wenyewe wanatakiwa kujitambua na kujiunga kwenye vikundi mbali mbali ilikuepuka kutumika kwa maslahi ya watu wengine.

No comments:

Post a Comment