Mbunge: Askari wanaoishi uraiani wanajiingiza katika uhalifu


Mbunge wa Viti Maalumu Mariam Msabaha (Chadema) amesema, kitendo ha baadhi ya askari kukaa uraiani kinasababisha askari hao kujiingiza katika masuala ya uhalifu.

Msabaha alitoa kauli hiyo alipouliza swali la nyongeza bungeni, ambapo alihoji kuwa hali hiyo ya askari kuishi uraiani ni kutokana na upungufu wa nyumba za askari unaosababishwa na Serikali kutotoa kipaumbele kwa kada hiyo.

“ Je, Serikali inasema nini katika kuhakikisha nyumba za askari zinajengwa nchi nzima ili watumishi hao wakae kambini na kujiepusha na kujiingiza kwenye masuala ya uhalifu?” alihoji Msabaha.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alisema polisi wawapo chuoni wanafundishwa mambo yote isipokuwa yanayotokea wawapo kazini ni makosa ya kibinadamu ambayo wizara hiyo inayafanyia kazi.

Alisema Serikali kupitia polisi, haioni haja ya kuongeza muda au mitalaa ya mafunzo ya awali kwani muda unatosha.

kuwapatia ujuzi na weledi wa kutosha.

Kuhusu ujenzi wa nyumba za askari nchini, alisema tatizo hilo limekuwa kubwa kutokana na kutochukuliwa hatua mapema lakini hivi sasa linashughulikiwa.

Kiongozi huyo alisema Serikali ina mpango wa kuboresha makazi ya askari kwa kukarabati na kujenga nyumba mpya ili wote waishi kambini, lakini akabainisha kuwa ufinyu wa bajeti unachangia.

 

No comments:

Post a Comment