elimu inayotolewa na uhamiaji ya kuwatambua wahamiaji haramu yaleta matunda

Na John Banda,Dodoma.

 IDARA ya Uhamiaji Mkoa wa Dodoma imesema  elimu inayotolewa na vyombo vya habari kuhusu kuwafichua wahamiaji haramu wanaoingia nchini kinyemela bila kibali halali.

 Imefanikiwa kutokana na  mahusiano mazuri na Halmashari ambazo zimeamua kutekeleza kwa kuziangiza ngazi zote za vijiji,kata hadi tarafa ziwe na kitabu cha kuhodheresha wageni wote wanaoingia katika maeneo yao.

hayo yamesemwa na Naibu Kamishana wa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma Norah Masawe alipokuwa akivishukuru vyombo vya habari, kwa kushirikiana katika utoaji wa taarifa ya elimu inayotolewa na idara hiyo kwa taasisi,mashirika na wakazi wa mkoa huo.

 Norah alisema elimu hiyo inayotolewa kwa kupitia vyombo vya habari,aidha imeleta mwitikio kwa watendaji wa ngazi zote za serikali na wananchi kuwa na utayari wa kwenda mahakamani kutoa ushahidi tofauti na kipindi cha miaka ya nyuma.

 Naibu Kamishana huyo alisema kuwa hivi sasa elimu hiyo inayotolewa na Idara hiyo ya Uhamiaji imeweza kuzifanya Halmashauri kuangiza watendaji wake kuwa na kitabu cha kuandikisha wageni wanaoingia kwa lengo la kuwabaini wahamiaji haramu.

 Alisema hivi sasa watendaji kwa kushirikiana na wananchi wanashirikiana na Idara ya Uhamiaji katika kuwabaini watu wanaoingia nchini kinyemela na kuamua kukaa nchini huku wengine wakijishughulisha na kazi mbalimbali bila kibali halali.

 “Unajua hapo mwanzo utaratibu huu ulikuwepo kwa kila balozi wa nyumba kumi alikuwa na kitabu cha kuhodheresha wageni wanaoingia katika maeneo yao na ndivyo inavyotakiwa kwa hivi sasa kwa hali hiyo ili kuwabaini wahamiaji haramu”alisema Norah.

 Norah alisema kuwa Mkoa wa Dodoma umekuwa na matukio mengi ya uingiaji wahamiaji haramu na hatimaye kufanikisha kuwakamata,hii inatokana na wakazi hao kuwa na mahusiano mazuri baada ya kupatiwa elimu ya jinsi ya kuwatambua wageni hao.

 Aidha Naibu huyo wa  idara ya uhamiaji ameendelea kuwataka wananchi wa mkoa huo kutoa ushirikiano katika kuwatambua wahamiaji hao haramu kwa kuwa watu hao wanaishi kwenye maeneo yao.

 

Mwisho.

No comments:

Post a Comment