MBOWE: ACHENI KUINGILIA TUME YA WARIOBA

MWENYEKITI wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema), Taifa Freeman Mbowe, amesema Kitendo cha baadhi ya vyama vya siasa kuingilia tume ya jaji Joseph Warioba iliyoteuliwa na rais ili kuleta katiba mpya yenye neema kwa watanzania ni Uoga wa kuondolewa madarakani.
Amesema tume ya jaji Warioba haikujitengenezea maoni yake ili kuwafurahisha wananchi bali maoni yaliyomo kwenye rasmu ya katiba ni maoni ya wananchi ambayo hayatakiwi kuingiliwa na chama chochote.
Mbowe amesema hayo jana jumatatu kwenye uwanja wa Magereza mjini Geita ikiwa ni ziara yake ya vuguvugu la mabadiliko''M4C''Pamoja Daima akitokea wilayani Biharamulo mkoani Kagera.
Amesema kuingilia tume ya mabadiliko ya katiba kuhusu maoni ya wananchi yaliyokusanya na tume unatokana na kubaini mapema kwamba kufikia mwaka 2015 chama kilichoko madarakani ccm itang'oka madarakani.

Mbowe amesema endapo serikali haitalifanyia marekebisho daftari la wapiga kura Chadema kitwahamasisha wananchi nchi nzima wasishiriki kupiga kura za maoni ya katiba.

Aidha ameitaka serikali kurekebisha daftari hilo ili kutoa fursa kwa watanzania wengi kushiriki kuipigia kura maoni ya katiba na chaguzi mbalimbali zijazo ikiwemo uchaguzi wa serikali za mitaa,na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment