Majibizano kati ya Marekani na Urusi UN


Mabalozi wa Marekani na Urusi wameshambuliana katika Umoja wa mataifa.
Majibizano makali yameshuhudiwa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambapo mataifa mengi yameshutumu
uamuzi wa Urusi kunyakua eneo la Crimea,kilele hatahivyo ilikuwa majibizano makali baina ya mabalozi wa Marekani na

Urusi .

Balozi wa Urusi, Vitaly Churkin, alisema kuwa watu wa Crimea walikuwa wamefanya maamuzi yao juu ya siku zao za

usoni.

Naye Balozi wa Marekani, Samantha Power akajibu akisema kile kinachotajwa na Urusi kama kura ya maoni ni kura

bandia.

Akikasirishwa na matamshi ya Power, Bwana Churkin alisema kuwa Balozi Power alikuwa amejishushia hadi kufikia

kiwango cha magazeti ya udaku.

Balozi huyo wa Urusi pia alitisha kuwa huenda Urusi ikakataa kushirikiana na Marekani katika maswala mengine muhimu

ya kimataifa iwapo Marekani itaendelea na msimamo wake juu ya Ukraine.

Majibizano hayo makali yanaendelea wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon anapoelekea Urusi kufanya

mashauriano na Rais Putin kwa lengo la kutafuta suluhu ya kidiplomasia.

Mkuu wa Majeshi nchini Ukraine, Andriy Parubiy, amesema Serikali yake inafanya kila juhudi kuwarejesha nyumbani

wanajeshi wake na familia zao walio eneo la Crimea, kufuatia hatua ya Urusi ya kunyakua Crimea.

No comments:

Post a Comment