63 wafariki katika ajali ya treni DRC

Treni hiyo ilikuwa imebeba idadi kubwa ya watu baadhi wakiwa wamekaa juu ya treni

Takriban watu 63 wamefariki baada ya treni iliyokuwa imebeba abiria kupoteza mwelekeo Kusini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Msemaji wa serikali Lambert Mende alisema kuwa polisi wanahofia kuwa idadi ya watu waliofariki huenda ikaongezeka. Pia alisema kuwa polisi watafanya uchunguzi kubaini chanzo cha ajali.

Ajali hiyo ilitokea karibu na eneo la Kamina katika mkoa wenye utajiri wa madini wa Katanga.

Treni hiyo ilikuwa imebeba idadi kubwa ya watu kupindukia wengine wakiwa wameketi juu ya treni yenyewe.

Waziri wa mambo ya ndani katika mkoa huo Jean Marie Dikanga Kazadi, aliambia BBC kuwadereva wa treni hiyo alikuwa anaiendesha kwa kasi .

Watu 80 walijeruhiwa vibaya huku wengine saba wakiwa bado wamekwama ndani ya treni vifusi.

Treni ilianguka Jumanne asubuhi lakini waokozi waliweza tu kuwasili nyakati za jioni.

Sehemu kubwa ya njia ya reli ya DRC, imesalia katika hali yake tangu enzi za ukoloni na ni nadra kufanyiwa ukarabati.

Treni hiyo ilianguka wakati dereva alipokuwa anajaribu kupunguza kasi.

No comments:

Post a Comment