Marekani yakerwa na ziara ya Assad Moscow

Assad na Putin


Marekani imeshutumu Urusi kwa kumpa mapokezi ya taadhima Rais wa Syria Bashar al-Assad mjini Moscow.

"Tunatazama mapokezi ya zulia jekundu aliyopewa Assad, aliyetumia silaha za kemikali dhidi ya watu wake, kuwa kinyume na lengo lililoelezwa wazi na Urusi la kutaka kuwepo na shughuli wa mpito kisiasa Syria,” msemaji wa ikulu ya White House Eric Schultz amewaambia wanahabari.

Afisa wa wizara ya masuala ya ndani ya Marekani alisema taifa hilo halijashangazwa na ziara hiyo, lakini wasiwasi mkubwa kwa Marekani ni Urusi kuendelea kumsaidia kivita Assad.

Alisema hilo litaipa nguvu zaidi serikali ya Assad na hivyo kuendeleza mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

Ziara hiyo ya kiongozi huyo wa Syria Jumanne ilifanyika wiki tatu baada ya Urusi kuanza kushambulia kwa ndege ngome za wapiganaji wa Islamic State na makundi mengine yanayopinga utawala wa Assad.

Ilikuwa ziara ya kwanza kabisa kwa Assad nje ya nchi baada ya mapigano kuzuka Syria 2011. Mapigano hayo ya wenyewe kwa wenyewe yameua watu 250,000.

Akiwa jijini Moscow, Assad alitoa shukrani zake kwa Urusi kuingilia kati kijeshi nchini mwake.

Alisema operesheni hiyo ya Urusi ilikuwa imezuia ugadi kueneza zaidi na kuwa madhara makubwa Syria.

Kwa upande wake, Bw Putin alisema matumaini ya Moscow ni kwamba suluhu ya muda mrefu itapatikana kupitia mchakato wa kisiasa na kwa kushirikisha makundi yote ya kisiasa, kikabila na kidini.

Mwandishi wa BBC aliyeko Moscow Steve Rosenberg anasema kuwa kwa kumkaribisha kiongozi huyo wa Syria mjini Moscow, Putin alikuwa akituma ujumbe mkali kwa mataifa ya Magharibi kwamba Moscow ni mhusika mkuu katika mzozo huo Mashariki ya Kati na kwamba suluhu haiwezi kupatikana bila kuhusisha Urusi.

Daktari bandia aliwaambukiza Ukimwi watu 100


Mwanaume mmoja aliyejidai kuwa daktari na kuwaambukiza watu zaidi ya mia moja virusi amefikishwa mahakamani nchini Cambodia.

Yamkini daktari huyo bandia alikuwa akiwadunga wagonjwa wake kwa sindano aliyokuwa ameitumia kwa mgonjwa aliyekuwa na virusi vya Ukimwi.

Yem Chhrin anakabiliwa na kosa la kuua na kuambukiza watu ugonjwa huo kwa kukusudia.

Aidha Bw Yem anashtakiwa kwa kuwalaghai watu kuwa ni daktari ilhali hana vyeti halali vya kuhudumia umma.

Iwapo atapatikana na hatia mahakama ya nchi hiyo huenda ikamhukumu kifungo cha maisha jela.

Waathiriwa walioambukizwa maradhi ya Ukimwi wanatokea katika kijiji cha Roka kilichoko Kaskazini Magharibi.

Mmoja wao ni kiongozi wa kidini wa madhehebu ya Buddha na mtoto wa miaka mitatu.

Takriban 10 kati ya waathiriwa hao wanakisiwa kuwa wameshakata roho.

Kwa mujibu wa ripoti za mahakama daktari huyo bandia amekiri kuhudumu bila vyeti maalum ila anakana kukusudia kuwaambukiza watu hao 100 virusi vinavyosababisha maradhi ya Ukimwi.

Assad afanya ziara ya ghafla Moscow

Assad na Putin


Rais wa Syria Bashar al-Assad amefanya mashauriano na Rais wa Urusi Vladimir Putin baada yake kufanya ziara ya kushtukiza Moscow.

Msemaji wa Rais wa Urusi Dmitry Peskov amesema Assad "alikuwa kwenye ziara ya kikazi Moscow" Jumanne na alifanya mazungumzo na Bw Putin.

Mwishoni mwa mwezi jana, ndege za kijeshi za Urusi zilianza kushambulia maeneo yanayodhibitiwa na wapinzani wa Assad nchini Syria.

Urusi imejitetea na kusema inashambulia tu makundi ya kigaidi na wapiganaji wa Islamic State.

Bw Peskov ameambia wanahabari kwamba viongozi hao wawili walijadiliana kuhusu viva hivyo alivyosema ni dhidi ya magaidi.

Aidha, walizungumzia kuendelea kwa mashambulio ya ndege za Urusi na mpango wa Syria kuhusu wanajeshi. Haijabainika iwapo Bw Assad bado yuko Moscow au amerejea Damascus.

Hiyo ndiyo ziara ya kwanza kabisa kufanywa na Bw Assad nje ya nchi tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria 2011, runinga ya serikali nchini Syria imesema.

Taarifa kuhusu mazungumzo hayo iliyotolewa na Kremlin inaonyesha Bw Putin akieleza Syria kama “rafiki” na kusema Urusi iko tayari kuchangia “sio tu kijeshi…bali pia katika mchakato wa kisiasa” kurejesha Amani nchini humo.

MHE. CHIKU GALLAWA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUSISITIZA AMANI NA UTULIVU WAKATI WA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 25

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=15089a284161b429&attid=0.1&disp=inline&realattid=f_ifzdor3g0&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ_0ZZFy9et6HUs4A6LKnhB0gMl8R03ISTH3JaXIkzS_f_rNqCgm78qTlFe1R8Etle97KfC71-WjtTejLJO0ppkcW8c3xU91bzFRYtHunPaLygsQcOslphtJo_a_xnk0d7NsuAFYOMWPLeIJUZgvx0mnOGx8wqD94WdGnU6LVcOQYJqEHZgX9IQzbo8-M3YQPjfXUn3Pj4yeznRC7jhuYMJNAMmj4OFkix0qxaqLkLxl7KUn8Q87aeIIA_L4Qs9GMc8Mr1jiCqMwjiw5qCZcXSKN9jhPXZyaF5LdLwuZJqp4hSFgLyobTwWFmViOpbpiBZwGvAiXz0hnR2ZxtzvVrgbJItnw2ijad2mgz9HFsiuJ3_dPFtxnI84vd4CX0d9xAmlNMI52zJdJoBQP2NdDbE_0AQt9Fz5GccxYJycWfAr-Dgst0Z4Ts2ZdclBoI2spcg_9IP04t7AcdP8RS4c5a-6v0obwrKJfXSkQuzys_MVv7szXcZqm06Z4DIcnYltQ5rpKVzzhzgqXXC0RrVkzdpoDsOA6ELRsdepveyYFiaGmgQ_oyF6UbnXnUzwfvrNBdY9yx4A-VwxpOR6qiuzHIEScMeazgtJjjy5aVgJGvWO41rYqf74p2FYXCBwMkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Gallawa akifungua Mkutano wa viongozi wa dini mkoani humo uliojadili masuala ya amani na utulivu wakati wa  uchaguzi Mkuu Oktoba 25


 https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=15089a284161b429&attid=0.2&disp=inline&realattid=f_ifzdorfh1&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-keXo4YPC0GMZkmLS5Ay-RJJx4XLvLnK7lilTnOmiCzjNf3rZKySnO1ZzlkrxeKgO2WVZfTAfvBdE1TTohDVWhdtHm_f4pc8yREFzf8RaaO-nZBUbINjOFL-E2jOwNF9f7TKk0MpgWeLfy0nJcFDoZpqQoMGARtm-SgkMWm0HKcv0UlqAokuCFBHDVsg8mkfwTCnfwMT01UU7805RXaKG26gU1-vh-UhbSOg5kEEkrRUcYhxwH9bNGeAPO-cxFf4P_-FacbK9arLtXHtzkfhN9V80DU6NaI_gw_QlwQxrsiOPKmPkzb-FL2gKL7ujfKZUkAfBN_FF45mnkI4j57UKJ07OWnhzYHHArFRDY1iLz4v5pTqtEwRhk1piOL-mwF1P5yF7IczaCYkEE_tj_4E7R3WwyiLDtFQ-4CJUVB52Kt2gAS1T9zpEuJeG4WiC8Ls7LIW9xNXSfMDeJ9Wm0P3AB0XpS057usoXp1mGKfY9yu5KHzPYVDkFaTR-AqWFzl6u-GoYemzSPDU1zAMhvsUjNU3HD14mA9vevRAvZ_fiZ6FfPrnaR5cj7p3_DZq0ZtqiuYMwPU1LpispmCSjGn_aKf8QvfeU9Tfq7PzolMBJnimCtaG6EubnPMCwhttps://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=15089a284161b429&attid=0.3&disp=inline&realattid=f_ifzdorjo2&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-_xxcQ2x-xSoOR8-XHgkoiwGksjtxX_NaOGRNG2Lq5iWzkrO045rCj6MXO3zJCDnmRPrxK2UP3PWRXtFpoal28qE3-Tzw7AIRl6vWk9nY04jRqXBVs038Zm5pQuMVSY_-JZBsaoFO00YHSEqa0PjxYxpPWs_cZCKKSvBrVW9qBku4SZQCKkrBXR9amrJHm5FjyT3QV5oRcQ_hXz6X3Li4cbFI1YuKYNhtD9pf4-ZK_27M2zZPxHqXm-jQqnh95ZsPWIRvgSN3tm9x4gJvL_39QtYzKcojP_IGV-HRvfyKE6rO8U5QJAXBvcFD9mZVIXoZ-1td189-JBVghbvnx2nam9nWvIIOrIf6OrSOQMqdspNaT2Co5rCBhEdO35_rTiUjlhVPa9n5v6rWlvWdNfiVo6GeP95rTwnKlTN7zJ4HMCRwZ2-FIlXfX-CxzE3-U8I22qQ7hJLF1sr2c4eoWeotMK37W-lJQVB8EhAyQSCuAqpkP8a6ntW3LacdCugrW4uZICItPQClFWy-t20BKxN3vNfLsj6ny7ywoWMNi4QcgeCmqs0DUZn8Lk9D9K-1nZZrX2qZp-A4v1g-QhYsHiGRFPSBW5zQ4yDJb7MasI58uj0WxVU3CsXbMkck Viongozi wa dini waliohudhuria Mkutano ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mapema leo kujadili masuala ya amani na utulivu wakati wa  uchaguzi mkuu oktoba 25.

 
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=15089a284161b429&attid=0.4&disp=inline&realattid=f_ifzdormw3&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ92_ttW4lvyP1IWNyJCL0VtQgLnZbVyb70wOEvPyieWZ9GJff5igHNi3c5lN2FSOHxq91SlGwqRjT0Q04yTkZjlXSOFZwqkHdfjaC-_I2bpTgSeK3kK2pGWJZzJQORqcVjmtR8k52v9wGVXF8uTTzD6pwOJ3qu8Yip__aWMF-NuXnSEKDbbbmLn1O-1Q1f2UogTLK2rXoweuu2I6Bff_2U_RY4D0OFpXKpjfEfO4mzt33vu0kjT84dbqlJ7ghYgkcsoHuc4yATA2gh7xttGI_HlZp-iHKIlBJkh0QEQzSBh6UlFgI-fAbBRtE6uvUqiVwfjd6YJDpmwD_DOgL6YSVE81qhgK_bksKLZvgalS_QPnR16gIOT9LgQTZ5oAGjh6dXyJAcGb-ItoGZBPurK9hdaiQYjWFO38q4RVsXRW3Qu88N1EBH1HBFjG33xwDtSw06WvfbuB5_rTZMKiYfbf_v3-WLpmmQM9MrdYvtgiUB3fLle2XFIGTv3qKrQvCGyMeAtS8XB1-_-6R5g5vJYV3gGBRS5aPbCLLZc9cE2NLDbEI5O9WV2lqiF3l6hFn1pwh-gi2ECSe0PGzZ4TAfuAU2A07ZZckBT1JMc95VigWg-gUZKgMtUvi3-rPE 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma SACP David Misime akifafanua jinsi jeshi la polisi Dodoma lilivyojipanga kusimamia amani na utulivu wakati wa uchaguzi mkuu oktoba 25 mapema leo kwenye kikao cha viongozi wa dini kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.