CHAVITA YAZITAKA HALMASHAURI NCHINI KUWAPA MGAO WAO WA FEDHA ZA WALEMAVU WENYE VVU

CHAMA cha Viziwi Tanzania Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kimeitaka Halmashauri ya wilaya hiyo kutoa fedha zinazotengwa na serikali kwa ajili ya mfuko wa walemavu wa Ukimwi.

Hayo yamebainishwa  na Mratibu wa mradi wa mafunzo yalugha ya alama Wilaya Kondoa Mustaph Shabani, kwenye mafunzo ya lugha ya alama yaliyofadhiliwana shirika la The Foundation for Civic Society (FCS)
kwa ajili ya watumishi wataasisi mbalimbali za kiserikali iliyofanyika Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma.

Shabani amesema chama cha viziwi kinashangazwa kuona Halmashauri hiyo ikishindwa kuwapatia fedha hizo ambazo zimekuwazikitengwa na serikali kila mwaka kwa ajili ya maendeleo ya walemavu.

Amesema Chavita inatambua serikali kwa kupitia Halmashauri zake hapa nchini imekuwa zikitenga fungu hilo kwa ajiliwalemavu lakini Katibu Tawala wa Wilaya ya Kondoa Dorosta Katokwa upande wake aliwataka watumishi wa idara ya Afisa Maendeleo na Jamii naAfisa

Maendeleo ya Jamii walifikishe suala hilo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kama kuna fungu hilo kwa ajili ya jamii wasiojiweza.

Dorosta amesema fungu hilo kama lipo kwa Mkurugenzi nihaki yao hivyo hakuna sababu ya kutolifuatilia wakati viziwi hao wanamahitajimengi wanayokabiliana nayo yakiwemo ya ugonjwa wa ukimwi.

Kwea upande wao wazazi na Walezi wa watoto wenye ulemavu wa kutosikia (viziwi) wameomba mradi wa mafunzo ya lugha ya alama unaofadhiriwa na shirikalisilo la kiserikali la the Foundation for Civic Society, kuwapatia mafunzoya muda mrefu yatakayo warahisishia uwelewa zaidi wa elimu ya mawasiliano pindiwanapokuwa na

familia zao.

Mmoja wa wazazi haoFatuma Raffa alisema wametoa ombi hilo kutokana na muda unaotolewa wa mafunzo ya lugha ya alama kuwa mdogo kwa kuwa wazazi walio wengi hawana elimuya uwelewa wa mawasiliano

No comments:

Post a Comment