DRC kuimarisha uhusiano na Rwanda

Rais Joseph Kabila wa DRC kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa

Rais wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ameambia BBC, kwamba atajitahidi kuimarisha uhusiano kati ya nchi yake na Rwanda,

Lakini alisema kuwa hana uhakika ikiwa awe na matumaini kuhusu mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa utakaojadili hali katika Maziwa makuu baadaye leo.

Bwana Kabila ameituhumu Rwanda kwa kusaidia waasi wa M23 Mashariki mwa Congo ambao wamekuwa kwenye mapambano na jeshi la Congo.

Rais Kabila na mwenzake wa Rwanda, Paul Kagame wamepewa onyo kali na Marekani kuwa lazima watatue mgogoro uo.

Kauli hii inakuja baada ya uamuzi wa Marekani mwezi Julai kusitisha msaada wa dola laki mbili kwa jeshi la Rwanda.

No comments:

Post a Comment