Uwanja wa ndege wa Goma utafunguliwa ili kuwafikishia chakula watu walioachwa bila makao
Ripoti ya Umoja wa mataifa iliyofichuliwa inasema wanajeshi kutoka Rwanda walihusika moja kwa moja na utekaji wa mji wa Goma katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo uliotekelezwa na waasi.
Ripoti hiyo iliyokusanywa kwa ajili ya baraza la usalama, inasema wanajeshi mia tano wa Rwanda, walihusika katika utekaji huo wa kundi la M23.
Wanajeshi wa Congo walirudi Goma hapo jana siku mbili baada ya waasi kuondoka kutoka mji huo wa Goma mwishoni mwa wiki baada ya mkataba wa amani uliofikiwa kwa usaidizi wa nchi za ukanda wa Maziwa Makuu.
Lakini waasi wameonya kuwa watauteka tena mji huo ikiwa serikali haitatimiza matakwa yao katika muda wa siku mbili.
Waasi hao waliondoka Goma siku kumi na moja baada ya kuuteka mji huo kutoka kwa wanajeshi wa DRC wakiungwa mkono na wanajeshi wa amani wa Umoja wa Mataifa
Mnamo Jumatatu mamia ya wanajeshi wa DRC waliwasili katika kambi zao mjini Goma baada ya waasi kuondoka kutoka mji huo mkuu wa mkoa wa Kivu Kaskazini siku ya Jumamosi.
Jean-Marie Runinga (Katikati) ni kiongozi wa kisiasa wa M23
No comments:
Post a Comment