Haramia nchini Somalia
Kiongozi mmoja wa kijamii nchini Somalia, ameiambia BBC kuwa, mtu mmoja ambaye ametanjwa na Umoja wa Mataifa, kuwa kinara wa utekaji nyara, ametangaza kuwa amestaafu rasmi kutoka kwa uharamia.
Mohamed Abdi Hassan, ambaye anajulikana kwa jina la utani kama "afweyneh" ikiwa na maan mtu mwenye usemi mkubwa nchini Somalia, amewaambia waandishi wa habari kuwa anastafu kutoka kwa biashara hiyo baada ya miaka minane.
Bwana Hassan aliyasema hayo katika kikao kilichofanyika mjini Abado, kati kati mwa Somalia, eneo ambalo maharamia hao wamekuwa wakiwazuilia mateka wao.
Ulinzi umeimarishwa Somalia
Mashambulio ya kiharamia katika pwani ya Somalia, yalipungua kwa kiasi kikubwa mwaka uliopita.
Baadhi ya maharamia waliokamatwa
Wachanganuzi wanasema hali hiyo iliyokana na kuongezeka kwa meli za kijeshi zinazoshika doria katika eneo hilo na pia kujumuishwa kwa walinzi wanaosindikiza meli za mizigo.
Afisa mkuu wa utawala katika eneo hilo amesema kuwa maharamia wengine katika eneo hilo wamekubali kusalimisha silaha zao.
''Tumewashawishi wao kutomiliki silaha na pia kusalimisha zile wanazomiliki ikiwa ni pamoja na mashua na silaha'' Alisema Bwana Mohamed Adan, ambaye ni kiongozi wa Utawala katika eneo hilo la Adado.
'' Wao wamegundua kuwa kwa sasa hawawezi kuendeleza uharamia kama ilivyokuwa hapo awali bila kuzingatia sheria na pia Uharamia kwa sasa haina faida kama ilivyokuwa'' Aliongeza afisa huyo wa utawala.
Ripoti ya Umoja wa Mataifa
Moja ya meli iliyokuwa imetekwa nyara
No comments:
Post a Comment