Wanawake wanaotumia njia za kisasa uzazi wa mpango waongezeka

PSI Tanzania

Idadi wanawake wanaotumia njia za kisasa za muda mrefu za uzazi wa mpango, zinazotolewa na Shirika la PSI imeongezeka mara mbili kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Akizungumza na  Wahariri na Waandishi waandamizi kutoka vyombo vya habari nchini, Mkurugenzi wa Programu ya Afya ya Uzazi ya PSI Tanzania,  Dk. Nguke Mwakatundu, alisema ongezeko hilo ni zaidi ya asilimia 100 katika kipindi cha mwaka mmoja.


Alisema kipindi cha mwaka jana, jumla  ya wanawake waliopatiwa huduma hiyo ilikuwa 102,778 wakati mwaka 2011 waliopatiwa huduma ya uzazi wa mpango walikuwa 48,518.

Dk. Mwakatundu alisema kwa upande wa programu yao ni mafanikio ya kujivunia ingawa wangependa kuona idadi hiyo inaongezeka zaidi mwaka huu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Romanus Mtung’e, alisema wamejipanga kuhakikisha wanawake nchini wanapatiwa huduma bora na za kisasa za uzazi wa mpango.


Alisema ni kipindi mwafaka kwa wananchi kutambua umuhimu wa kupanga familia zao ili watoto wanaozaliwa wapate malezi mazuri na huduma bora toka kwa wazazi, jamii na serikali.

No comments:

Post a Comment