Tume ya uchaguzi ingali inatangaza matokeo ya urais eneo bunge moja baada ya nyingine
Mahakama ya juu nchini Kenya hii leo itatoa uamuzi ikiwa ina uwezo wa kusikiliza kesi iliyowasilishwa kwake na makundi ya kijamii yakitaka tume huru ya uchaguzi nchini Kenya kusitisha shughuli ya kuhesabu kura za urais inayoendelea katika ukumbi wa Bomas.
Makundi hayo yanadai kuwa tume inakwenda kinyume na katiba ambayo ambayo inasema kura zinapaswa kuhesabiwa kwa njia ya elektroniki.
Hapo jana Muungano wa CORD ulielezea malalamishi kuhusu shughuli yakujumlisha kura za urais na kusema hauna imani nayo kwani ina ushahidi kuwa hujuma imefanyika wakidai wizi wa kura.
Pia wanadai kuwa katika baadhi ya maeneo, kura zilizopigwa ni nyingi kuliko idadi ya wapiga kura waliosajiliwa.
Madai haya waliyatoa hapo jana ingawa mkuu wa tume ya uchaguzi aliyakanusha vikali na kusema hakuna mahala popote ambapo wameshuhudia matokeo kuhujumiwa.
Chama hicho pia kilidai kuwa baadhi ya matokeo yalikuwa juu ikilinganishwa na idfadi ya wapiga kura.
Na kwa hilo, mkuu wa tume ya uchaguzi Isaack Hassan pia alikanusha vikali akisema hawajapata matokeo kama hayo.
Tume hiyo imesisitiza kuwa shughuli ya kuyahakiki matokeo inafanywa mbele ya maajenti wa vyama vyote.
Tume ya uchaguzi ingali inaendelea na shughuli ya kujumlisha kura za urais
No comments:
Post a Comment