AMUUA MAMA YAKE KWA KUMPIGA MTALIMBO KICHWANI

Habari zilizotufikia punde zinasema kuwa Kijana Fransis Chiza, mkazi wa Kiluvya A, Wilaya ya Kisarawe anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kumuua mama yake mzazi kwa kumpiga kwa mchi au mtalimbo kichwani na kufa papo hapo.

Inadaiwa kuwa kijana huyo ambaye ni mototo wa pili wa mama huyo alifika jana usiku na kumgongea mlango mama yake lakini mama yake hakuweza kumfungulia kutokana na kuwa na mlemavu jambo hilo lilimkasirisha na hivyo ilipofika asubuhi ya leo aliamua kutuliza hasira yake kwa kumpiga mama yake.

Baada ya kufanya tukio hilo kijana huyo alikimbia na baadaye kukamatwa na wanakijiji. Jeshi la polisi wilaya ya kisarawe wameshafika eneo la tukio na kwa taarifa zaidi juu ya tukio hili zitakujia muda si mrefu….

No comments:

Post a Comment