Na John Banda, Dodoma

WANANCHI wa katongoji cha Njedengwa wamefurahishwa na hatua zilizochukuliwa na viongozi wa juu wa serekali ngazi ya Wilaya baada ya kuingilia kati malalmiko waliyoulalamikia uongozi wa kata kutoingilia kati Swala la kuitisha mkutano kitongojini hapo.

 

Wananchi hao waliokuwa wakidai kuitishwa kwa mkutano ili waweze kutoa kelo mbalimbali zinazowasumbua kitongojini hapo walisema wamefurahishwa na hatua yaserekali kusikia kilio chao na kuamuru mkutano uitishwe.

 

Mwenyekiti wa Uhamasishaji wa madai hayo Khatibu Mayuni alisema  kutokana na barua walioandikiwa viongozi wa kata hiyo ya kutakiwa kuitisha mkutano mkuu wa kitongoji jumanne ijayo imewapa faraja na kuona kumbe serekali inaweza kusikiliza kilio cha wananchi.

 

Mayunini aliongeza kuwa kutokana na usumbufu waliokuwa wanaupata toka kwa viongozi hao wa kata walikuwa wameadhimia kuomba kibali na kufanya maandamano mpaka bungeni ili wakatetewe na wabunge waliowachagua kutokana na kukosa haki ya kuuliza wala kutoa maoni ya mapato na matumizi.

 

  ‘’Mwanangu unadhani tungeweza kutolea maoni yetu wapi

   kama si katika mikutano ambayo viongozi wamegoma

   kuiitisha kwa kipindi cha miaka mitatu sasa bora sasa

   nadhani kitaeleweka kwa sababu hata mkurugenzi           atakuwepo ili ajionee mwenyewe wananchi unavyotafunwa’’, alisema

 

Wakati huohuo Barua iliyoandikwa na afsa utumishi wa Manispaa Lawrence Malangwa Kwa niaba ya Mkurugenzi imemtaka afsa mtendaji wa kata hiyo Magreth Songolo kushiriki kuuandaa na kuhudhuria mkutano huo ambao  mkurugenzi  atasikiliza kelo za wananchi hao.

 

Barua hiyo Iliyoandikwa Tar 11 APR 213 yenye kichwa habari kuitisha Mkutano Mkuu wa Kitongoji cha njedengwa na nakala zake kupelekwa kwa Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Manispaa, Mkuu wa Polisi Wilaya [OCD], Diwani wa kata hiyo na Mwenyekiti wa kitongoji cha njedengwa ilisisitiza mkutano huo kufanyika Saa 9:30 alasili.

 

Kero za wananchi hao ni pamoja na Kutoitishwa kwa mikutano kwa kipindi cha miaka mitatu, Kutoshirikishwa Ugawaji wa viwanja 99 vilivyopimwa na CDA katika ugawaji, kubinfsishwa kisima cha maji na zaidi ya nyumba 119 zilizobomolewa tangu 2010  ili kupisha muwekezaji  huku wakiahidiwa kupewa eneo jingine la makazi.

No comments:

Post a Comment