HATARI:MSICHANA WA MIAKA 16 APIGWA RISASI BAADA YA KUKUTWA ANASHIRIKI TENDO LA NDOA NDANI YA GARI NA MWANAUME JIJINI DAR ES SAALAM


JESHI la polisi limekumbwa na

 kashfa nyingine baada ya askari wake

 kudaiwa kumpiga risasi msichana wa

 miaka 16 baada ya kumkuta akivunja amri ya sita ndani ya gari.

Msichana huyo..

(Jina tunalihifadhi) alikumbana na mkasa huo

 Jumatano usiku eneo la Mbagala Zakhem

 jijini Dar es Salaam, ambapo alipigwa

 risasi sehemu ya makalio wakati

 akijaribu kuwakimbia polisi kwa 

kutumia gari la mpenzi wake.

Mpenzi huyo (jina linahifadhiwa), 

alikamatwa na kuwekwa mahabusu na

 kufunguliwa kesi ya ubakaji.

Akizungumza na NIPASHE Jumapili jana katika wodi

 ya Hospitali ya Temeke alikolazwa, msichana

 huyo alisema siku ya tukio alikutana na

 kijana huyo majira ya saa 8:00 usiku

 katika baa moja inayoitwa Kindau na

 kukubaliana kwenda kushiriki 

tendo la ndoa kwa malipo ya Sh 20,000.
Alisema kutokana na muda huo kuwa

 usiku sana hawakuweza kwenda katika

 nyumba ya kulala wageni na badala yake

 walikwenda eneo la Zakhem na kisha

 walipaki gari kwenye uchochoro na

 baadae walianza kubanjua amri ya sita.
Wakiwa kwenye kilele cha mapenzi yao

, ghafla walishtukia gari la polisi likiwajia 

kwa kasi kwa nia ya kuwakamata.

“Tuliagana anilipe elfu ishirini wala

 hakunibaka kama anavyodai, wao 

polisi walitukuta tayari tunamaliza

 lakini kutokana na woga 

tulikimbia ili tusikamatwe,” alisema msichana huyo.

Alisema wakati wanakimbia 

kwa kutumia gari la mpenzi wake

 askari mmoja alifyatua risasi

 iliyopenya kwenye taa ya gari na

 kwenda kumjeruhi sehemu ya makalio yake.

“Nilisikia mlio mkubwa wa bunduki,

 ghafla nilihisi kitu kimeingia mwilini

 mwangu na kuishiwa nguvu,” alisema kwa uchungu.

Alisema kwa kuona hali hiyo, 

mpenzi wake alisimamisha gari kwa 

kujisalimisha na polisi walipowafikia

 walimtaka mpenzi wake huyo atoe pesa

 kama malipo ya kitendo chao cha 

kukutwa wakifanya mapenzi

 ama sivyo watampeleka kituoni.

Alieleza kuwa mpenzi wake hakuweza

 kutoa pesa hizo ndipo walipoamua

 kumpiga na kumpeleka kituo cha

 polisi cha Mbagala na yeye alifikishwa 

hospitalini hapo kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo, ndugu na jamaa wa mpenzi

 wake wanapinga hatua ya polisi hao

 kutumia nguvu kubwa kama watu hao

 walikuwa watuhumiwa wa ujambazi.

Wakizungumza wakiwa kwenye kituo 

cha Polisi cha Mbagala kufuatilia

 hatma ya ndugu yao, ndugu hao

 ambao hawakutaka majina yao 

yatajwe gazetini walisema hatua ya

 polisi kupiga risasi huku wakitambua

 watu hao sio majambazi ni kitendo cha kinyama.

“Tunachoshangaa ni kwa nini polisi

 wapige risasi wakati wakijua hawakuwa

 majambazi ila walikuwa wakifanya 

mapenzi, hata hilo jalada la kesi 

walilofungua wanataka kuficha maovu

 yao na sio vinginevyo,” alisema ndugu

 mmoja ambaye alijitambulisha kuwa shemeji yake.

Alisema kimsingi tukio hilo lilikwenda 

katika makubaliano yao na sio ubakaji

 kama wanavyodai, ila kinachofanyika

 kwa sasa ni kutaka kumlinda askari

 mwenzao aliyejeruhi kwa risasi.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke,

 David Misime, alipopigiwa simu kuelezea 

tukio hilo, alisema kwa sasa hawezi

 kulizungumza kwa kuwa yupo nje ya Mkoa kikazi.

No comments:

Post a Comment