Simulizi ya askari aliyemuua bin Laden

 

Tangu kuuawa kwa kiongozi wa Kundi la Al-Qaeda Osama bin Laden kumekuwa na fununu nyingi zinazoeleeza mazingira ya kifo chake pamoja na ujumla wa maisha yake wakati akiwa mafichoni. Katika mfulilizo wa makala haya, Mwandishi George Njogopa amepitia simulizi za askari aliyemuua kiongozi huyo kama alivyozungumza na mwandishi mmoja wa habari nchini Marekani.

Akiwa mtu mwenye tabasamu na ucheshi wa mbali, askari (jina linahifadhiwa) anatoa maelekezo kwa mwandishi wa habari aliyetaka kujua historia ya maisha yake jeshini. Ndani ya mgahawa uliofurika watu waliochangamka kwa vinywaji, askari mwanamaji anaanza kueleza namna alivyojiunga na Jeshi la Wanamaji la Marekani hadi kufikia nafasi ya kuwa mlenga shahaba mkuu.

Anasema anakumbuka kile kilichomsukuma kuchukua uamuzi wa kujiunga na jeshi ni kama sehemu ya hasira iliyomkumba baada ya kuachwa na mpenzi wake al iyedumu naye kwa kipindi kirefu.

“Unajua tukio la kuachwa na mpenzi wangu lilinivunja moyo sana… na ndiyo nikachukua uamuzi kwenda jeshini.

Anasema kuwa siku yake ya kwanza alipokwenda kuomba kazi anakumbuka alimwambia ofisa mmoja wa jeshi kuwa alikuja hapo kuomba kazi ya kulenga shahaba (sniper).

“Pale nilimkuta askari mfukuzi, mkufunzi akaniuliza unataka nini… nikamwambia nataka kuwa mlenga shahaha, lakini yeye akaniambia kuwa tayari walikuwa na walenga shabaha.

Hata hivyo alifaulu kuandikishwa na baadaye kupelekwa kwenye mafunzo yaliyimwongezea ujuzi wa kazi na hatimaye kuungana na vikosi vya wanajeshi wa maji vilivyosafiri sehemu mbalimbali duniani. Kama ilivyo kwa askari wengi wanamaji, askari huyu alishiriki kwenye operesheni mbalimbali za kijeshi ikiwemo zile zilizohusu katika nchi za Afghanistan na Iraq.

Anasema operesheni yake kubwa ya kijeshi ilikuwa nchini Afghanistan ambako vikosi vya Marekani vilivamia katika eneo hilo katika kile kilichoelezwa na kukabiliana na utawala wa Taliban ambao ulitajwa kuwa na ushirikiano wa karibu na Kundi la Kigaidi la Al-Qaeda.

“Uzoefu mkubwa wa kijeshi niliupata wakati nikiwa Afghanistan ambako nakumbuka nilishiriki kikamilifu kukabiliana na wanamgambo wa Taliban. Tulipofaulu kuwafurusha wanamgambo hao tuliendelea kubakia nchini huko kuimarisha hali ya usalama na kusaidiana na wananchi wa eneo lile kurejesha hali ya usalama.

“Kichwa changu kilikuwa tayari kimeshazoea mizinga na makombora, maana wakati mwingine umekaa sehemu ghafla unasikia kombora linavurumishwa mbele yako… Ghala nyuma unasikia mlio wa bunduki.. Kusema kweli nilijifunza mengi wakati nikiwa Afganistan.

Wakati huo Marekani ilianzisha operesheni za kukabiliana na Kundi la Al-Qaeda ambalo lililodaiwa kutekeleza tukio la kigaida katika majengo yake mjini New York na Washington.

Shabaha ya Marekani ilikuwa kukabiliana na kiongozi wa kundi hilo, Osama bin Laden ambaye wakati huo ilisemekana amejichimbia mafichoni katika Milima ya Afghanistan.

 

Marekani haikuishia kuingia kijeshi nchini Afghanistan pia iliivamia Iraq na hatimaye kuuangusha utawala wa Saadam Husen aliyekuwa akiongoza Chama cha Baath ambacho kilikuwa na uhusiano pia na baadhi ya makundi ya kigaidi.

Anakumbuka kuwa jinsi alivyorejea nyumbani Marekani na kisha kuungana na wanamaji wenzio ambao waliunda kikundi cha wataalamu wachache walikuwa na shabaha ya kuleta mageuzi ya utendaji ndani ya vikosi vya wanamaji hasa kwa kutumia uzoefu waliopata wakati wakiwa kwenye operesheni za kijeshi katika nchi za kigeni.

“Unajua ukishajiingiza kwenye mambo haya ya kulenga shabaha hujali tena lolote, wewe unachoona ni kwamba umeletwa duniani kwa kazi maalumu na hiyo kazi lazima uitekeleze kwa wakati uliopangwa,” anasema askari huyo akimwelezea mwandishi mmoja wa habari namna alivyoshiriki kwenye kikosi maalumu kilichoshiriki kwenye operesheni ya iliyofanikisha kuuawa kwa kiongozi wa Kundi la Al-Qaeda, Osama bin Laden.

Kwa masharti ya kutotajwa jina wala kuonyeshwa picha yake, askari huyo anasema kuwa, “Tulipomaliza kazi nchini Afghanistan tulirudi nyumbani na kuendelea na mazoezi yetu ya kuogelea katika Ufukwe wa Miami. Tukiwa kule ghafla tukapata taarifa baadhi yetu tulihitajika kwenda Virginia kwa ajili ya kazi maalumu.

“Kusema kweli hatukujua nini tunachokwenda kukifanya maana tulielezwa kuwa kuna kazi ya dharura. Wengi wetu tukabaki tunahisi labda tunataka kupelekwa Libya, wengine wakasema labda tutaenda Japan kukabiliana na athari za kimazingira baada ya tetemeko kubwa la ardhi kulikumba taifa hilo.

Katika siku ya kwanza tulivyopata taarifa, kusema kweli walitudanganya. Tulizungushwa maeneo mbalimbali na kila mara maofisa wetu walikuwa wakitupa maelezo ya kutia matumaini wakisema kuwa tusiwe na wasiwasi tutaarifiwa punde kwani kulikuwa hakuna jambo lolote la kutisha.”

Anasema kuwa baada ya kukaa kwa siku kadhaa walipelekwa moja kwa moja hadi yaliko makao makuu ya upelelezi CIA, ambako walipokewa na maofisa wa ngazi juu aliyewagawanya kwenye vitengo bila kuwapa maelekezo yoyote.

“Wakati tunakwenda tuliambiwa tungekutana na Waziri wa Ulinzi, maofisa wa ngazi za juu wa jeshi pamoja na wataalamu wengine wa kijeshi. Tulipata hisia jambo tulioloitiwa huko huenda likawa kubwa. Tulipofika pale tulikusanywa kwenye chumba kimoja na baada ya muda alitokeza mwanamke mmoja ambaye kwa sura alionekana kuwa mtu jasiri na mwenye kuelewa kile anachokizungumza.

“Tuliona tumeletewa televisheni..vifaa vya kivita na pembeni kulikuwa na ramani kubwa ambayo hata hivyo ilifunikiwa na kitambaa . Hatukujua kile kilichokuwa kinaendelea. Yule mwanamke aliposimama ndipo pumzi ikatushuka,” Anaelezea kuwa walipatiwa maelekezo kuhusiana na sehemu ambayo inasadikika Kiongozi wa Al-Qaeda, Osama bin Laden ndiyo ilikuwa makazi yake.

“Yule askari wa kike akiwa katika hali ya kujiamini, alituonyesha ramani na kutufafanulia shabaha ya kuitwa kwenye chumba kile. Nilishtuka lakini kadiri nilivyomtazama yule askari niliamini kile alichokuwa akikisema. Tulionyeshwa nyumba moja ambayo iko pekee yake katika eneo la Abbottabad.

Baada ya hapo tukaingia kwenye mazoezi makali tukijifunza namna ya kuingia kwenye nyumba ile na namna tukavyoweza kumudu purukushani zozote zinazoweza kujitokeza.

Mafunzo yetu yalidumu kwa muda wa wiki kadhaa na kisha tulipangiwa siku ya kuondoka kuelekea Pakistan.

Anasema kuwa msafara wa kuelekea Pakistan alianzia nchini Ujerumani walikoweka kituo na kisha kuruka moja kwa moja hadi nchini Pakistan kupitia eneo la Jalalabad.

“Unajua wakati tunakatiza anga ya Pakistan niliingiwa na hofu sana pengine vikosi vya pale vingeilenga ndege zetu na kuzitungua maana kulikuwa hakuna taarifa zozote kwa Serikali ya Pakistan kuwa Majeshi ya Marekani yalikuwa yakiingia nchini humo.

Tulipita eneo lile na hatimaye kufika Abbottabad. Tulikuwa tumejipanga vya kutosha. Msafara wetu ulikuwa na helikopta, ndege za kivita pamoja na vifaru kukabili hali yoyote korofi ambayo ingejitokeza.

Nilishangaa kuona kile nilichoonyeshwa kwenye picha za satelaiti wakati nikiwa kwenye mazoezi Marekani ndicho nilichokishudia pale.

Tulishuka kwenye helikopta haraka na kisha kuizingira nyumba mara moja. Kuna wengine walitanda juu ya paa, wengine madirishani na wengi walikuwa angani kwenye helikopta.

Tulipofika mlangoni tulikuta tundu la risasi, tukashtuka kidogo, nikamwambia mwezangu acha woga hebu twende, nikasukuma mlango hadi ndani.

Wakati kabla hatujaingia ndani tulisikia sauti ikiita bla, blab la,,, kumbe ilikuwa sauti ya mmoja wa walinzi wa Osama ambaye alikuwa amevalia fulana nyeupe na pajama nyeupe pia.

Tulimdhibiti na kupanda hadi ghorofa ya pili ambako tuliwakuta kina mama wakiwa wanahangaika na kupiga kelele.

Hatukutaka kuwadhuru tuliwaweka chini ya ulinzi, nami nikaendelea kupanda juu hadi ghorofa ya tatu.

“Nilipofika chumba cha juu nilimwona mtu mmoja mrefu kupita wote, ndevu zake alikuwa ameonyoa kiasi. Alikuwa ameweka mikono yake begani kwa mwanamke mmoja ambaye baadaye nilikuja kugundua alikuwa mkewe Jamal.

Nadhani alikuwa anafanya vile kama njia mojawapo wa kujikinga. Alikuwa amevalia kofia na kuendelea kuzunguka huku na kule na yule mwanamke.

Nakumbuka alikuwa mwembamba. Pembeni yake kulikuwa na silaha aina ya AK 47, ambayo baadaye aliishika mkononi.

Binafsi sikutaka kupoteza muda, nilinyanyua bunduki yangu na kumiminia risasi mbili usoni na kisha nikamshudia namna alivyoanguka chini na kukata roho. Sikujali kama amekufa ala nilimmiminia risasi nyingine moja.

Itaendelea Kesho    

No comments:

Post a Comment