Uhuru kuapa kama Obama


Uhuru Kenyatta 


Mke wake ndiye atamshikia Biblia na yeye atakuwa anaishika kwa kuweka mkono kama  alivyofanya Rais Obama wa Marekani

Nairobi. Rais Mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema kwamba wakati wa kuapishwa hataapa kwa kuinua Biblia bali atasaidiwa na mkewe kama alivyoapishwa Rais Obama wa Marekani.
Mkuu wa Majeshi ya Kenya (KDF), Jenerali Julius Karangi alisema jana kuwa Kenyatta aliomba  mkewe Margaret Kenyatta amshikie Biblia atakapokuwa akiapishwa.

“Hili ni ombi la rais mteule na itakuwa vyema tukubali ombi lake katika siku hii ya kihistoria,” alisema Jenerali Karangi.
“Mke wangu atanishikia biblia kisha nitaweka mkono kama alivyofanya Omaba,hakuna Rais wa Kenya aliefanya hivyo” alisema

Kenyatta ataweka  tu mkono wake wa kushoto juu ya Biblia ikishikiliwa na mkewe, katika kile anachotaja hatua ya kuachana na mtindo wa awali wa kuapisha marais wa Kenya wakiinua Biblia.

Kenyatta ataiga mfano wa Rais Barack Obama wa Amerika, alipoapishwa hadharani mjini Washington DC mnamo Januari 21, 2013, ambapo aliomba mkewe Michelle Obama amshikie Biblia.

Siku hiyo Rais Mwai Kibaki atamkabidhi katiba mpya Kenyatta, ambayo ilianza kutumika mnamo Agosti 2010. Mtindo huu utakuwa wa kwanza tangu nchi hiyo kupata Uhuru. Sherehe hiyo itafanywa katika Uwanja wa Michezo wa Moi Kasarani, ambapo pia Naibu wa Rais William Ruto ataapishwa.
Shughuli hiyo inatarajiwa kumalizika saa 7.45. Kamati ya Mamlaka ya Ofisi ya Rais tayari ina ratiba ya mpangilio wa shughuli hiyo.
Ratiba hiyo ina picha ya rais anayeondoka katika ukurasa wa pili na ya  Kenyatta katika ukurasa wa tatu. Kamati hiyo imeteua Rais Yoweri Museveni kuzungumza kwa niaba ya wageni wote waalikwa siku hiyo.

Hapo jana asubuhi, kamati hiyo inayoongozwa na Mkuu wa Utumishi wa Umma, Francis Kimemia, ilisema kwamba shughuli itaanza rasmi 5:45 asubuhi Rais Kibaki atakapowasili uwanjani.

Kulingana na mpangilio uliopo, wageni watahitajika kusimama Rais Kibaki akiwasili, wakati wa sherehe ya kuapishwa, saluti ya mizinga 21 itakapopigwa nje ya uwanja na wimbo wa taifa utakapoimbwa kabla ya Rais Kibaki na rais mpya kuondoka uwanjani.

Siku hiyo,  Kenyatta atapambwa kwa vifaa vya mamlaka ambavyo ni pamoja na Mkuu wa Nakshi (CGH), pia atapokea mkuki, ngao na katiba.

Zana hizo zinaashiria mamlaka; kwa mfano Katiba inasimamia Kenya na watu wake, mkuki unasimamia Amiri Jeshi Mkuu ilhali CGH ni heshima kubwa zaidi Kenya.

Wadau wa Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi Mkoani hapa kutokana na juhudi za kupambana na uhalifu hususani kudhibiti mtandao wa majambazi sugu.

Nwaka Mwakisu  Mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Taifa kupitia Umoja wa Vijana Mkoa wa Mbeya katika mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika katika ofisi za Umoja wa Vijana CCM Mkoa wa Mbeya. hivi karibuni
Baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa Mbeya wakimsikiliza Mwakisu


 Wadau wa Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi Mkoani hapa kutokana na juhudi za kupambana na uhalifu hususani kudhibiti mtandao wa majambazi sugu.

Wadau hao walisema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani ndiye anayepaswa kupongezwa kutokana na juhudi alizozionesha za kufichua mtandao wa majambazi ikiwa ni pamoja na kuwakamata na kuwauwa wengine.

Akizungumza kwa niaba ya wadau hao Nwaka Mwakisu ambaye pia ni Mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Taifa kupitia Umoja wa Vijana Mkoa wa Mbeya katika mkutano wa waandishi wa Habari uliofanyika katika ofisi za Umoja wa Vijana CCM Mkoa wa Mbeya.

Mwakisu alisema Historia ya Mkoa wa Mbeya ilikuwa Mbaya ambapo ilikuwa ikisifika kwa matukio mabaya kama ya upigaji nondo, ubakaji, ushirikina na ujambazi ambavyo vimeanza kutoweka kutokana na juhudi zilizooneshwa na Jeshi hilo kwa kushirikiana na wananchi.

" Kutokana na hali ilivyo sioni sababu ya kutompongeza RPC Diwani kutokana na kupambana na uhalifu Mkoani Mbeya " alisema Mwakisu. 

Alisema kutokana na hali halisi ya Amani ya Mkoa wa Mbeya Wawekezaji watajitokeza kwa wingi kufanya uwekezaji tofauti na ilivyokuwa ambapo wawekezaji walikuwa wakikimbia Mkoa wa Mbeya kutokana na Vurugu zilizokuwepo. 

Aliongoza kuwa kutokana na juhudi za Jeshi la Polisi za kupambana na uhalifu alisema ni vema kila Mwananchi akatambua mchango huo na kusaidia katika kuhakikisha kuwa amani inaongezeka Mkoani Mbeya.

Mwakisu alisema pamoja na kutokomeza uhalifu Mkoani hapa pia suala la kuwatumikisha Vijana katika mambo yasiyokuwa na msingi wowote hususani kwenye vurugu ndiyo sababu ya kuongezeka kwa uhalifu.

Alisema taifa lolote duniani linalindwa na kuendelezwa na vijana hivyo alitoa wito kwa wanasiasa kuacha kuwatumia vijana vibaya ambapo aliongeza kuwa Vijana wenyewe wanatakiwa kujitambua na kujiunga kwenye vikundi mbali mbali ilikuepuka kutumika kwa maslahi ya watu wengine.

JE VIONGOZI WA SERIKALI KATA YA ILEMBO MBEYA VIJIJINI MMEIONA BENDERA HII AU SIYO YA TAIFA LETU?

HII NI BENDERA YA TAIFA LETU LA TANZANIA BENDERA HII TUMEIKUTA KATIKA SHULE YA MSINGI HAZINA KATA YA ILEMBO MBEYA VIJIJINI TUNAAMINI KABISA SHULE HUWA HAITEMBELEWI NA KIONGOZI YEYOTE YULE WA CHAMA NA SERIKALI

HIVI NDIYO INAVYOONEKANA BENDERA HII SHULENI HAPO
MASKINI WANAFUNZI HAWA HAWAJAWAHIONA BENDERA MPYA WAMEZOEA KUONA BENDERA ILIYOCHANIKA TANGU WAANZA SHULE HIYO YA HAZINA 

Watuhumiwa 11 kizimbani

Mtuhumiwa namba moja wa mashtaka 24 ya kuua bila kukusudia, Raza Hussein Ladha (kushoto) akipelekwa chini ya ulinzi wa polisi kuingia katika chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam jana. 

Dar es Salaam. Mfanyabiashara Radha Hussein Ladha wa jijini Dar es Salaam, Diwani katika Manispaa ya Kinondoni, Ibrahim Mohamed maarufu kama Kisoki (59) na wenzao 9, jana walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka 24 ya kuua bila ya kukusudia.


Katika kundi hilo pia wamo vigogo wa Manispaa ya Ilala ambao ni Mhandisi Mkuu, Mhandisi Charles Salu (48), Mhandisi wa Majengo Godluck Sylivester (35) Mbaga na Mkurugenzi Mkuu wa Mkaguzi wa Majengo, Willibrod Wilbard (42).


Washtakiwa wengine ni Mhandisi Mohamed Swaburi (61), Mhandisi Mshauri, Zonazea Oushoudada (60), Mkadiriaji Majenzi, Vedasto Nziko (59), Msanifu Majengo, Michael Hema (59), Msajili Msaidizi AQRB, Albert Mnuo na Ofisa Mkuu Mtekelezaji OQRB, Joseph Ringo.


Akisoma hati ya mashtaka jana mbele ya Hakimu Mkazi, Devotha Kisoka, Wakili wa Serikali, Tumain Kweka akisaidiana na mawakili wenzake watano, alidai kuwa washtakiwa walifanya makosa kinyume na kifungu cha 195 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho 2002.


Kweka anasadiana na wenzake Benard Kongora, Ladslaus Komanya, Neema Haule, Joseph Maugo na Mutalemwa Kishenyi.


Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa washtakiwa hao kwa pamoja Machi 29, mwaka huu katika Mtaa wa Indira Gandhi, Wilaya ya Ilala waliwaua bila ya kukusudia Yusuph Mohamed, Kulwa Khalfan na Hamada Mussa.


Mbali na watu hao, pia wanadaiwa kuwaua bila ya kukusudia Kessy Manjapa, Khamis Mkomwa, Boniface Benard, Suhail Ally, Salmani Akbar, Seleman Haji, Seleman Mtego, Sikudhani Mohamed, Ahmed Milambo, Salum Mapunda, Suleiman Rashid na John Majewa.


Wengine ni Mussa Mnyamani, David Severin Herman, William Joackim, Abdulrahman Mwiha, Emmanuel Christian, Mmanyi Ngadula, Adivai Desiki, Emmanuel Greyson na Augustino Kasiri.
Washtakiwa wote hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mashtaka yanayowakabili Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza hadi Mahakama Kuu.


Mawakili wa utetezi wakiongozwa na Wakili wa Kujitegemea, Jerome Msemwa waliiomba mahakama kutoa dhamana kwa wateja wao kwa sababu mashtaka ya kuua bila ya kukusudia yanayowakabili yanadhaminika.


Wakili wa Serikali, Kongora alipinga maombi hayo, huku wakili mwenzake Komanya akisema kuwa wakati huu si wa kutoa dhamana kwa kuzingatia mazingira ya tukio lililosababisha kuwepo kwa kesi hiyo.


Kutokana na hoja hizo, Hakimu Kisoka aliiahirisha kesi hiyo hadi Aprili 16, mwaka huu atakapotoa uamuzi iwapo washtakiwa wapate dhamana ama la.
Naye Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka ametangaza kiama dhidi ya wamiliki wenye maghorofa yaliyojengwa kinyume cha utaratibu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwenye Ofisi ndogo ya Bunge, Profesa Tibaijuka alisema kwa kuanzia angesaini hati ya kuamuru kubomolewa kwa jengo lililokuwa karibu na lile lililoanguka wiki iliyopita na kuua idadi kubwa ya watu.
Alimwonya mmiliki wa jengo hilo anatakiwa kufanya ubomoaji mara moja tena kwa gharama zake.


“Serikali ikibomoa jengo hilo ina maana atatakiwa kulipia gharama za zoezi hilo,” alionya Profesa Tibaijuka, ambaye aliapa kuanza leo ukaguzi wa maghorofa mbalimbali ya jijini Dar es Salaam.

JICHO LETU KATIKA MAGAZETI APRIL 4

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC03823
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC03834

Mvutano kuhusu haki ya kuchinja wanyama wazua vurugu Tunduma

 

Tunduma. Vurugu kubwa zilizuka jana katika Mji wa Tunduma ambao ni makao makuu ya Wilaya ya Momba, Mkoa wa Mbeya, baada kutokea mvutano mkali kuhusu nani anayepaswa kuchinja mifugo baina ya waumini wa dini mbili; Waislamu na Wakristo.


Mamia ya polisi kutoka wilaya zinazouzunguka Mji wa Tunduma walimwagwa na walilazimika kutumia mabomu ya machozi na maji ya kuwasha ili kuwatawanya waandamanaji pia, kutuliza vurugu zilizodumu kwa zaidi ya saa nne.

Vurugu hizo ambazo zinahatarisha amani, zimetokea siku tatu tu tangu Rais Jakaya Kikwete aonye kwamba kwamba vurugu zenye sura ya kidini ni hatari na zinaweza kuvuruga amani na utulivu uliodumu kwa miaka mingi nchini.


Mijadala kuhusu vurugu hizo ilitawala katika mitandao ya kijamii ikiwamo facebook, Mabadiliko Forum na Jamii Forums ambako watu mbalimbali walionyesha kukerwa nazo, huku wakiitaka Serikali ichukue hatua za kudhibiti.


Kutokana na vurugu hizo zilizoanza saa 4:30 asubuhi, wakazi wa mji huo walijifungia ndani kwa kuhofia usalama wa maisha yao, huku maduka na shughuli za biashara nazo zikifungwa.
Mwandishi wa Mwananchi aliyekuwa katika eneo la tukio anaripoti kwamba katika vurugu hizo, watu zaidi ya 35 wamekamatwa wakiwamo Diwani wa Kata ya Tunduma Frank Mwakajoka na Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Gidion Mwamafupa.


Habari zaidi zinasema barabara za mji huo zilifungwa, umeme ulizimika baada ya moto kulipuka kwenye moja ya nguzo za umeme. Pia mpaka wa Tanzania na Zambia ulifungwa kwa muda.


Magari ya abiria na yale ya usafirishaji yaliyokuwa yakitoka na kuelekea Zambia, Dar es Salaam, Sumbawanga na Mbeya Mjini pia yalikwama na kusababisha usumbufu mkubwa kwa abiria. Msikiti ulivunjwa na watu wawili akiwamo askari polisi walijeruhiwa.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athuman alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kwamba tukio hilo limetokea wakati Serikali ikiwa kwenye mazungumzo na baadhi ya wahusika katika mgogoro wakiwamo viongozi wa dini na wachinjaji wa nyama.


“Mgogoro wa kuchinja umedumu kwa siku tatu, jana kamati ya ulinzi na usalama chini ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro ilikutana na baadhi ya viongozi wa dini na wadau wa kuchinja nyama na kuna mambo matatu ambayo yalitolewa katika mkutano huo,” alisema Diwani.


Alisema katika mkutano huo Kandoro aliagiza kuwa wananchi wanatakiwa kuwa wavumilivu katika kipindi hiki, ambacho Serikali ngazi ya kitaifa inalishughulikia na kuwataka kuendelea na hali uchinjaji kama ilivyokuwa awali na kila mmoja afanye kile anachoamini katika dini yake wakati wa kula.


Hata hivyo, baadhi ya Wakristo waliafikia lakini wengine hawakuafiki. Hivyo jana asubuhi walihamasisha maandamano katika mji huo ambayo yalisababisha vurugu hizo.


“Pamoja na hayo yote uchunguzi wa kitaalamu tumebaini kuwa vurugu hizo siyo za kidini, bali zimehusishwa siasa kwani hata viongozi wa dini waliohusika ni baadhi siyo wote ambao wanajishughulisha na suala hili,” alisema Diwani.

 Alisema kwa upande mwingine vurugu hizo zinafanywa na baadhi ya vijana wenye nia ya kuzitumia kwa lengo la kufanya uporaji.

Maafa juu ya maafa, Dar 36 Arusha 20


 

Kile kilichodhaniwa kuwa kilele cha sikukuu ya pasaka, kimegeuka msiba baada ya wachimba kokoto 20 kufukiwa katika kifusi Jijini Arusha.

Hiyo ilikuwa ni kama ndimu katika kidonda kibichi, kwani ni ijumaa iliyopita tu wakati watu wakijiandaa kwa sikukuu ya Pasaka jengo la ghorofa 16 lilidondoka Jijini Dar es Salaam na kuua watu 36.

Vifo hivi vilivyotokea katika msimu wa sikukuu vimeweka idadi ya watu waliopoteza maisha kufikia 56 hivi, ndani ya  siku nne tu.

Watu waliofukiwa na kifusi mkoani Arusha, walikuwa wakichimba kokoto katika eneo la Moshono.

 Imeelezwa kuwa ni maiti 14 tu ndizo zilizoopolewa na watu wengine bado wanahofiwa kuwa ndani ya kifusi hicho.

 Ilikuwa ni saa tano asubuhi, juzi, gema la kokoto liliporomoka kisha kuwafunika wote waliokuwamo ndani, sababu kubwa ikielezwa kuwa ni mvua kubwa zilizokuwa zikinyesha mjini Arusha.

 Vilevile magari mawili yaliyokuwa yamepaki pembeni kwa ajili ya kubeba mzigo huo yalizama ndani ya shimo hilo kubwa la kokoto.

Watu saba walikufa 1997

Inaelezwa kuwa hii ni mara ya pili kwa mgodi huu kuua watu kwani mwaka 1997 wachimbaji wa kokoto walifukiwa na saba kati yao walipoteza maisha.

Tukio la Dar

Mlinzi wa msikiti wa Shia, aliyeshuhudia kudondoka kwa ghorofa hilo amesema  alianza kuona mashine ya zege ikianguka kutoka ghorofa ya 17 ambapo ujenzi wa sakafu ya ghorofa hiyo ulikuwa ukiendelea.

Mlinzi huyo, Athuman Salum Mnere anasema alisikia sauti ya kukatika kwa kitu, ghafla sauti kubwa ya maporomoko, kisha mashine ya zege na baada ya sekunde kadhaa, jengo lote likawa chini.

Anasema walionusurika walianza kuwaokoa watoto waliokuwa wakicheza mpira katika uwanja wa ndani ya msikiti uliokaribu na jengo hilo.
Aliwakanya watoto waliopoteza maisha

Anasema aliwaambia watoto waliokuwa  wakicheza mpira katika uwanja huo waende nyumbani lakini hawakusikia.

Hata kabla ya dakika tano kwisha, jengo hilo liliporomoka na wale wanne waliokuwa wamekaa katika benchi walifunikwa na jengo.

“Wengine waliumia vibaya, ndiyo hao walioko hospitali. Wale waliokuwa kwenye benchi walikufa palepale”anasema.

 Shughuli za uokoaji zilimalizika juzi na eneo lilipokuwepo ghorofa hilo kubaki mithili ya shimo.

 

Ajifungua mtoto kwa mshtuko

Sumbawanga. Katika hali isiyokuwa ya kawaida mwanamke,  mkazi wa kitongoji cha Chemka ,Kata  ya Chanji Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa amejikuta akipata  uchungu  wa  ghafla na kujifungua   mtoto  wa kiume   chooni, nyumbani  kwake  kutokana  na mshtuko  alioupata  baada ya  kutolewa  kwa nguvu   katika  nyumba  hiyo  na dalali  wa mahakama.

Katika  tukio  hilo ambalo   mwanamke huyo (jina linahifadhiwa) alipata mshtuko  mkubwa  baada ya  dalali wa mahakama  kufika nyumbani  kwake  na kuanza  kutoa  nje vyombo vyake vyote  kwa madai kuwa nyumba hiyo  ilikuwa na mgogoro.

Kwa mujibu  wa  mwanamke huyo  baada ya dalali   kuwatoa  kwa nguvu  katika nyumba  hiyo  kwa  kutoa  nyombo  vyao vyote  nje  na kufunga  nyumba  hiyo  kwa makufuli  baada ya   kuhaha  na kukosa  sehemu ya kuhifadhi vyombo  hivyo  yeye  na familia yake  walilazimika  kulala  nje ya nyumba hiyo na kunyeshewa na mvua  usiku  kucha.

Alisema baada ya kutaabika  usiku kucha  kwa kunyeshewa na mvua  ilipofika  saa tano  asubuhi  alibanwa  na uchungu mkali  alipolazimika  kukimbilia  chooni  na kujifungua  mtoto  wa kiume akiwa hai.

Nauli ni Kiama: Sumatra yapandisha nauli za daladala, mabasi ya mikoani, treni na meli

Abiria wakigombania kuingia katika daladala. 

Dar es Salaam. Mamlaka ya Udhibiti wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), imepandisha nauli za daladala, mabasi ya kwenda mikoani, usafiri wa reli na tozo za majini kuanzia Aprili 12, mwaka huu.Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Ahmad Kilima alisema jana kuwa nauli za daladala zimeongezeka kwa asilimia 24.46 kwa kuzingatia maoni ya wadau na gharama za uendeshaji.


Kwa upande wa usafiri wa daladala nauli zimepanda kwa umbali tofauti kutoka Sh300 hadi 400, Sh350 hadi 450, Sh500 hadi 600, Sh650 – 750 na kwa wanafunzi kutoka Sh150 hadi 200 katika sehemu yoyote watakayokwenda.


Nauli za usafiri wa mabasi makubwa ya masafa marefu nauli hizo zimeongezeka kwa viwango tofauti. Mathalan kwa basi la kawaida kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya ni Sh30,700, njia ya vumbi kutoka Kigoma hadi Sumbawanga Sh25,400 na basi la hadhi ya kati (Semi Luxury) kati ya Dar na Mwanza ni Sh61,400, wakati basi la hadhi ya juu (Luxury) kati ya Dar na Arusha ni Sh 36,000.


Kilima alisema: “Kuanzia Aprili 12 mwaka huu, kati ya kilometa 0 hadi 10, nauli ya daladala itakuwa Sh400 badala ya Sh300 zinazolipwa hivi sasa.
“Pia nauli za mabasi ya kwenda mikoani zimeongezeka kwa asilimia 20.3 kwa mabasi ya kawaida, mabasi ya kati kwa asilimia 16.9 na mabasi ya daraja la juu kwa asilimia 13.2,” alisema.


Kilima alisema nauli za mabasi ya mikoani zimepanda kutoka Sh30.67 hadi Sh36.89 kwa kilometa kwa mabasi ya daraja la kawaida katika njia za lami.
Kwa upande wa mabasi ya kawaida kwa njia ya vumbi imepanda kutoka Sh37.72 hadi Sh 46.11 kwa kilometa na kwamba mabasi ya hadhi ya kati, nauli zimepanda kutoka Sh45.53 hadi Sh 53.22 kwa kilometa.


Alisema mabasi ya hadhi ya juu nauli zimepanda kutoka Sh51.64 hadi Sh58.47 kwa kilometa.
“Kupanda kwa nauli kunatakiwa kwenda sambamba na huduma bora na kwamba Sumatra imepiga marufuku kutumia wapigadebe kuuza tiketi za safari”alisema.

Usafiri wa Reli
Katika uamuzi huo, usafiri wa reli pia umepanda ambapo daraja la kwanza Dar es Salaam hadi Morogoro, nauli mpya na ya zamani katika mabano ni Sh21,100, (Sh16,852), Dar hadi Dodoma Sh34,700, (Sh27,788), Dar es Salaam-Tabora Sh54,800, (Sh43,859).
Dar es Salaam-Isaka Sh62,100, (Sh49,662), Dar- Shinyanga Sh65,300 (Sh52,229) Dar –Mwanza Sh74,800 (Sh 59,818), Dar- Kigoma Sh75,700, (Sh60,599)


Daraja la pili, Dar es Salaam-Morogoro Sh16,600, (Sh13,280), Dar es Salaam-Dodoma Sh26,400 (Sh 21,092), Dar es Salaam-Tabora Sh40,500 (Sh 32,364), Dar es Salaam-Isaka Sh45,800, (Sh36,605), Dar es Salaam-Shinyanga Sh48,000 (Sh38,390), Dar es Salaam- Mwanza Sh54,700 (Sh43,747), Dar es Salaam-Kigoma Sh55,400 (Sh44,305).


Daraja la tatu, dar es Salaam-Morogoro Sh8,800 (Sh6,138), Dar es Salaam-Dodoma Sh13,500 (Sh9,374), Dar es Salaam-Tabora 20,400 (Sh14,173), Dar es Salaam-Isaka Sh22,800 (Sh15,847), Dar es Salaam –Shinyanga Sh24,000 (Sh16,628), Dar es Salaam-Mwanza Sh27,200 (Sh18,860), Dar es Salaam- Kigoma Sh27,500 (Sh19,084).


Akizungumzia tozo za majini, Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mamlaka hiyo imeridhia ongezeko la tozo la asilimia 34.3 kwa vyombo vinavyotumia bandari za Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).


Alisema awali TPA walipendekeza tozo hizo kuongezeka kati ya asilimia saba hadi 400 kulingana na aina ya huduma zinazotolewa kwa meli zinazotumia bandari za mamlaka hiyo.